Posts

Showing posts from August, 2017

MKOANI KATAVI SIMBA AVAMIA KIJIJI MTOTO ANUSURIKA KUTAFUNWA-Agosti 31,2017

Image
MTOTO mmoja mwenye Umri wa miaka 13 Mkazi wa Isinde kata ya Mtapenda,Halmashauri ya Nsimbo Mkoani Katavi,amenusurika kufa baada ya kushambuliwa na Simba akiwa nyumbani kwao. Inaelezwa kuwa smba huyo alivamia kijijini hapo majira ya saa kumi usiku wa jana mpaka alipoanza kumshambulia mtoto huyo anayejulikana kwa jina la Nyutuliangila Madirisha.

POLISI,JAJI MKUU WATOA ONYO MGOMO WA MAWAKILI HAPA NCHINI-Agosti 28,2017

Image
Kaimu  Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Jeshi la Polisi nchini,wamelionya Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS),kutoingilia vyombo vya uchunguzi na upelelezi,vinavyochunguza tukio la mlipuko,uliotokea kwenye ofisi za Kampuni ya Mawakili ya IMMMA usiku wa kuamkia juzi jijini Dar es Salaam.

POLISI WAWEKA WAZI MAJIBU YA UCHUNGUZI OFISI ZA MAWAKILI IMMMA KULIPULIWA-Agosti 28,2017

Image
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo limesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu wasiojulikana utambulisho wao na idadi yao walifika katika ofisi za Mawakili wa IMMMA Advocates wakiwa katika magari mawili na kujifanya ni maaskari na kuwarubuni walinzi na kuondoka nao katika gari mojawapo kabla ya kulipua jengo hilo.

RAIS MAGUFULI AWATAKA TAKUKURU KUTOKUWA NA KIGUGUMIZI DHIDI YA WAHUSIKA VITENDO VYA WA RUSHWA-Agosti 28,2017

Image
Rais Magufuli akiwa ndani ya Ofisi ya Takukulu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU ) kutokuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua pale wanapokuwa na ushahidi dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.

OFISI ZA WANASHERIA AKIWEMO MTOTO WA RAIS FATUMA KARUME NA LAURENCE MASHA ZATEKETEA KWA MOTO USIKU WA KUAMKIA LEO-Agosti 26,2017

Image
Sehenu ya majengo ya Ofisi Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya amethibitisha kushambuliwa ofisi za wanasheria za IMMMA saa 8 usiku wa kuamkia leo.

MANISPAA YA MPANDA YAPATA HATI SAFI UDHIBITI HESABU ZA SERIKALI,RC APONGEZA-Agosti 26,2017

Image
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Msaafu Raphael Mugoya Muhuga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral mstaafu Raphael Muhuga  ameipongeza halmashauri ya manispaa ya Mpanda kwa kupata hati nzuri  ya udhibiti wa hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30 mwaka 2016.

HOFU JUU YA EBOLA YATANDA MKOANI RUKWA-Agosti 26,2017

Image
Kirusi cha Ebola WAKAZI mkoani Rukwa wametakiwa kuondoa hofu kutokana na kuwepo kwa taarifa juu ya uwepo wa ugonjwa wa ebola baada ya mgonjwa mmoja kulazwa na kuendelea kupatiwa matibabu Katika hospital ya mkoa ya Sumbawanga anaeugua ugonjwa wenye dalili kama za homa ya Ebola.

RC RUKWA AZUIA UUZWAJI NJE MADINI YA CLINKER -Agosti 26,2017

Image
Bandari ya Kasanga RC-Rukwa-mbele-ya-Madini-ya-Clinker- Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amekamata na kuzuia uuzwaji wa tani 2,143 za madini aina ya “Clinker” yanayotumika katika kuzalishia saruji kutokana na wingu la ubabaishaji uliogubika usafirishaji wa madini hayo kwenda nje ya nchi hadi hapo atakapojiridhisha na utaratibu wa uuzwaji huo.

CHAMA CHA ACT WAZALENDO CHALAANI UCHOMAJI MOTO MAKAZI YA WATU KATAVI-Agosti 25,2017

Image
CHAMA cha ACT Wazalendo mkoa wa Katavi kimelaani kitendo cha uchomaji wa makazi ya watu wanaodhaniwa kuwa wanaishi katika hifadhi ya misitu na kuitaka serikali kutafakari upya  suala hilo.

TFS WASISITIZA KUWATIMUA WANANCHI WANAOVAMIA HIFADHI ZA MISITU-Agosti 23.2017

WAKALA wa huduma za misitu nchini TFS  Mkoani Tabora imeendelea kusisitiza azma yake ya kuwaondoa wananchi wote waliovamia kwenye maeneo ya hifadhi kufuatia uharibifu mkubwa unaofanywa na wananchi hao kutokana na kuendesha shughuli mbalimbali za kibinadamu ambazo zimekuwa zikichangia uharibifu.

TAMKO LA DED NKASI KUWALINDA WANAFUNZI WENYE UALBINO DHIDI YA JUA KALI-Agosti 23.2017

MKURUGENZI wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa Julius Kaondo amewapiga marufuku walimu wa shule za msingi na sekondari kuacha tabia ya kuwafanyisha kazi ngumu na kwenye jua kali wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi albino kwa kuwa kufanya hivyo wanawahatarisha afya zao na kupelekea kupata saratani ya ngozi.

WAZIRI NCHEMBA ATISHIA KUWAFUTIA URAIA WATANZANIA WABAGUZI-Agosti 23.2017

Image
WAZIRI wa mambo ya ndani Mh.Mwigulu Nchemba ametishia kuwafutia uraia watanzania wapya wa Katumba mkoani Katavi ambao walikuwa wakimbizi kwa muda mrefu kutokana na tabia ya ya baadhi yakubaguana kitaifa na kikanda. Waziri Mwigulu Nchemba

HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA YATENGA EKARI 2400 KWA AJILI YA UWEKEZAJI,SEKTA YA UFUGAJI,KILIMO,BIASHARA,UTALII,HUDUMA ZA JAMII NA MAKAZI YA WATU KUPEWA KIPAUMBELE-Agosti 21,2017

HALMASHAURI ya wilaya ya Mpanda mkoani katavi imesema  imetenga eneo la Luhafwe lenye ukubwa wa  ekari  2400  kwa ajili ya uwekezaji.

UGOMVI WA MKULIMA NA MFUGAJI WASABABISHA MAJERUHI KATAVI-Agosti 21,2017

WATU wawili wilayani Mpanda Mkoani Katavi wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao baada ya kuzuka ugomvi uliosababishwa na  kile kilichodaiwa ni kupishana kauli kati ya mkulima na mfugaji katika kijiji cha mbugani kata ya Kakese iliyopo manispaa ya Mpanda.

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA FUNGUZI WA MKUTANO WA 37 WA SADC MJINI PRETORIA-Agosti 19,2017

Image
Viongozi wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa  mkutano wa  37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika mjini Pretoria, Afrika ya Kusini .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan leo amehudhuria  ufunguzi rasmi wa Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika – SADC mjini Pretoria Afrika Kusini akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli.

SERIKALI YA TANZANIA YASEMA UJIO WA NDEGE MPYA UKO PALEPALE-Agosti 19,2017

Image
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bibi. Zamaradi Kawawa  Serikali imethibitisha na kuwahakikishia Watanzania kuwa ujio wa ndege mpya ya tatu aina ya Bombardier Q400-Dash 8 upo pale pale licha ya baadhi ya wanasiasa wasio wazalendo kutumia kila njia kukwamisha ujio huo.

WANAFUNZI 22 WA SHULE YA SEKONDARI MIRAMBO MKOANI TABORA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUFANYA VURUGU-Agosti 19,2017

Image
JUMLA ya wanafunzi 22 wa shule ya sekondari Mirambo Mkoani Tabora,wamefikishwa na kusomewa mashtaka 12 yanayowakabili ikiwemo kufanya vurugu katika kata ya Chemchemi.

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI,WAMO WAWILI WA VYUO VIKUU,MWENYEKITI WA KAMPUNI YA KUHIFADHI MAFUTA,MWENYEKITI WA BARAZA LA USHINDANI -Agosti 18,2017

Image
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe Magufuli,amefanya uteuzi wa viongozi mbali mbali akiwemo Mkuu wa chuo kikuu cha Ardhi.

MADAKTARI BINGWA KUTOKA DAE SES SALAAM WATOWEKA BILA TAARIFA KWA WAGONJWA MKOANI KATAVI,WAGONJWA WAHAHA KUPATA MATIBABU,MGANGA MKUU MKOA WA KATAVI ASHIKWA KIGUGUMIZI KUSEMA HALI ILIVYO-Agosti 18,2017

Image
Mh.Anna Lupembe Mbunge viti Maalumu Katavi(PICHA na.Issack Gerald) WAGONJWA ambao wamewasili  Mjini Mpanda wakitokea maeneo mbalimbali Mkoani Katavi kwa lengo la kupimwa na kutibiwa na madaktari bingwa wameeleza kusikitishwa na hatua ya madaktari hao kuondoka ghafla bila kutoa taarifa hatua ambayo imesababisha wagonjwa kupoteza muda na gharama za usafiri.

BARAZA LA MADIWANI MKOANI MARA LAWAADHIBU WATUMISHI WANNE KWA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA-Agosti 17,2017

Image
Baadhi ya madiwani Mkoani Mara Baraza la Madiwani la Halmashauri ya mji wa Tarime mkoani Mara leo Alhamisi, Agosti 17 limewakuta na hatia na kuwachukulia hatua za kisheria watumishi wanne kwa kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia halmashauri hiyo hasara ya mamilioni ya fedha.

MKURUGENZI MANISPAA YA MPANDA AWATOLEA UVIVU WAKUU WA IDARA WASIOTOA USHIRIKANO KWA WAANDISHI WA HABARI KATIKA KUTOA HABARI-Agosti 17,2017

Image
Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu(PICHA NA Issack Gerald) Mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Maiko nzyungu amewataka wakuu wa idara mbalimbali ndani ya manispaa,kutoweka ugumu katika utoaji wa Taarifa kwani ni kinyume cha Sheria iliyopitishwa na bunge.

JESHI LA POLISI MKOANI KATAVI LAWAPIGA MARUFUKU WAPIGA DEBE KATIKA STENDI ZA MABASI-Agosti 17,2017

Image
JESHI la Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani Katavi,limepiga   marufuku shughuli za upigaji debe katika stendi zote Mkoani Katavi.

SERIKALI MKOANI TABORA YATEKETEZA SHAMBA LA MIHOGO YA MWANANCHI-Agosti 17,2017

Image
Mhogo Serikali ya mkoa wa TABORA imeteketeza shamba la mihogo la mkazi mmoja wa kata ya IPULI mjini TABORA baada ya kushindwa kutii agizo la mkuu wa mkoa wa TABORA la kuondoa mazao yake katika  eneo la Chuo Kikuu cha Askofu Mkuu MIHAYO cha TABORA-AMUCTA.

SERIKALI KUJENGA BENKI TANO ZA DAMU SALAMA KATIKA MIKOA MITANO UKIWEMO MKOA WA KATAVI -Agosti 17,2017

Image
Damu salama baada ya uchangiaji Mkoani Katavi(PICHA NA.Issack Gerald) SERIKALI imesema imepata fedha kwa ajili ya ujenzi wa benki za damu salama katika mikoa mitano hapa nchini ukiwemo Mkoa wa Katavi ili kutatua matatizo ya watanzania yanayotokana na ukosefu wa damu salama inapohitajika kwa wagonjwa.

KITUO CHA AFYA INYONGA CHAPANDISHWA HADHI KUWA HOSPITALI YA WILAYA-Agosti 17,2017

Image
Sehemu ya Majengo ya Kituo cha Afya Inyonga ambacho kimepandishwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Mlele(PICHA NA.Issack Gerald Agosti 17,2017 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,wazee na watoto Mh.Ummy Mwalimu amekipandisha hadhi kituo cha afya cha Inyonga kilichopo katika halmashauri ya wilaya ya mlele kuwa hospitali ya wilaya hiyo.

SUMATRA KATAVI YATOA MIEZI 3 KWA BODABODA KUKATA LESENI-Agosti 16,2017

Mamlaka ya uthibiti na usafiri wa nchikavu na  majini mkoani   katavi umetoa muda wa miezi mitatu kwa waendesha pikipiki maarufu kama boda boda  katika halmashauri ya wilaya ya mlele wawe wamekamilisha ukataji wa lesen za vyombo vyao vya moto pamoja na lesen za udereva.

SERIKALI KUAJIRI WATUMISHI 3100 WA SEKTA YA AFYA KABLA YA SEPTEMBA 30 MWAKA HUU-Agosti 16,2017

Image
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu SERIKALI imesema inatarajia kuajiri watumishi wa sekta ya Afya 3100 wakiwemo 35 katika Halamshauri tano za Mkoani Katavi kabla ya Septemba 30 mwaka huu.

MADAI YA WAKAZI WA KITONGOJI CHA MGOLOKANI MKOANI KATAVI KUDAI KUWAMIWA NA SERIKALI NA KUBOMOLEWA MAKAZI YAO WAKATI WA OPARESHENI YA KUWAONDOA WAVAMIZI WA HIFADHI ZA MISITU KUWAKUTANISHA VIONGOZI WA WILAYA YA MPANDA KUSAKA SULUHU-Agosti 15,2017

Image
HALMASHAURI ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi ijumaa ya wiki hii,inatarajia kukutana na Uongozi wa Wilaya ya Mpanda pamoja na viongozi wa hifadhi ya misitu Wilayani Mpanda, kujadili madai ya wananchi wa kitongoji cha Mgolokani kilichopo kijiji cha Matandalani kata ya Sitalike halmashauri ya Nsimbo wanaodai kuvamiwa na Serikali na kuharibu makazi yao kwa madai yanayotolewa na serikali kuwa wakazi hao wamejenga makazi yao katika eneo la hifadhi ya misitu.

WAZIRI WA AFYA MH.UMMY MWALIMU KUWASILI KESHO MKOANI KATAVI KUZINDUA ZOEZI LA UPIMAJI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA-Agosti 15,2017

Image
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu WAZIRI wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh.Ummy Mwalimu anatarajia kuwasili kesho mkoani Katavi kwa ajili ya kuzindua zoezi la siku  tano la upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza.

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MKURUGENZI MKUU WA NHIF-Agosti 12,2017

Image
Katibu mkuu kiongozi balozi John Kijazi(by P5 TANZANIA) Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania John Magufuli amemteua Bw.Benard Hezron Konga kuwa mkurugenzi mkuu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF.

SERIKALI YA MTAA MKOANI KATAVI YAHOFIA MAFURIKO YA WANAFUNZI-Agosti 12,2017

SERIKALI ya mtaa wa Kampuni kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda,Imeiomba Manispaa ya Mpanda kuandaa miundombinu ya madarasa ya kutosha katika shule ya msingi Nsambwe,ili kukidhi idadi ya wanafunzi itakayoongezeka katika shule hiyo baada ya wakazi wa mtaa wa msasani na tambukareli kuhamia eneo hilo wakiwa na wanafunzi.

RAIS UHURU KENYATTA ATANGAZWA MSHINDI WA URAIS KENYA-Agosti 12,2017

Image
Uhuru Kenyatta, baada ya kutangazwa mshindi, ametoa wito kwa wananchi kudumisha umoja Tume ya taifa ya uchaguzi Kenya imemtangaza Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Jumanne.

IEBC YASEMA MFUMO WAKE HAUKUDUKULIWA-Agosti 10,2017

Image
Afisa mkuu tume ya Uchaguzi Kenya Ezra Chiloba Tume ya IEBC imesema kuwa hakuna udukuzi wowote uliofanyiwa mfumo wake wa kutoa matokeo ya uchaguzi kielektroniki.

RTO KATAVI:WAMILIKI IMARISHENI MAGARI YENU KABLA YA SAFARI-Agosti 9,2017

Wamiliki wa magari katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani katavi wametakiwa kuhakikisha magari yao yanakuwa imara kabla ya kuyaigiza barabarani.

RC KATAVI ATAKA WATENDAJI WA VIJIJI KUWA NA DAFTARI LA WAKAZI-Agosti 9,2017

Mkuu wa Mkoa wa katavi meja jenerali mstaafu  Raphael muhuga  amewataka watendaji wote wa vijiji mkoani hapa  kuwa na daftari la wakazi katika maeneo yao.

OPARESHENI BOMOABOMOA YAENDELEA KULIZAWAKAZI MKOANI KATAVI-Agosti 9,2017

WAKAZI wa kitongoji cha Mgolokani Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,wameiomba serikali kurejeshewa ardhi yao au kuwatafutia maeneo ya kuweka familia zao kufuatia kufukuzwa na nyumba zao kubomolewa ambapo serikali imedai kuwa wakazi hao wanaishi ndani ya misitu ya hifadhi.

MGOMO WA SIKU 2 WA WAENDSHA BAJAJI MANISPAA YA MPANDA MKOANI KATAVI WASITISHWAAgosti 9,2017

WAENDESHA pikipiki za tairi tatu maarufu kama bajaji manispaa ya Mpanda Mkoani,wameruhusiwa kusafirisha abiria bila mipaka kwa kupita katika barabara walizokuwa wamezuiliwa ambapo barabara hizo ni pamoja na barabara ya Mpanda-Kigoma,Mpanda Sumbawanga na Mpanda Nsimbo.

SHIRIKA LA INTERNATIONAL AID SERVICES LATOA MSAADA WA MAFUTA KWA AJILI YA WENYE ULEMAVU WA NGOZI-Agosti 8,2017

SHIRIKA la International Aid Services(IAS) limetoa msaada wa mafuta yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino ili kuzuia mionzi mikali ya jua inayochoma ngozi zao.

MADEREVA BAJAJI WILAYANI MPANDA MKOANI KATAVI WAGOMA,SUMATRA WATOA TAMKO KALI WASISITIZA HAKUNA BAJAJI KUPITA BARABARA KUU KUANZIA KESHO AGOSTI 8,2017

Image
WAENDESHA pikipiki za tairi tatu maarufu kama bajaji Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,leo wamegoma kutoa huduma ya usafiri wakilalamikia hatua ya Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi kavu SUMATRA kuwazuia kutumia barabara kuu zinazotoka mpanda mjini na kusafirisha abiria kupitia barabara kuu.  

SHULE YA MSINGI NSAMBWE YAKABILIWA NA UPUNGUFU VYUMBA VYA MADARASA-Agosti 3,2017

Zaidi ya wanafunzi 250 wa shule ya msingi Nsambwe iliyopo kata ya Misunkumilo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wanalazimika kusomea nnje k utokana na upungufu wa vyumba vya madarasa.

WILAYA YA MLELE YAZINDUA MKAKATI WA MAENDELEO WA MIAKA MITANO-Agosti 3,2017

Halmashauri ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi imezindua mpango mkakati wa miaka mitano wa maendeleo ya mwaka 2016/2017 hadi mwaka 2021.

WAHAMIAJI HARAMU WILAYANI MLELE MKOANI KATAVI KUANZA KUSAKWA-Agosti 2,2017

Mkuu wa wilaya ya mlele mkoani Katavi Rahel Kasanda amewaagiza watendaji wa idara mbalimbali kataka Halmashauri hiyo kushirikiana vema na wananchi katika kuwabaini wahamiaji haramu wanaoingia katika wilaya hiyo. 

WAKAZI MANISPAA YA MPANDA WAUNGA MKONO DAWA ZA CHANJO KWA WATOTO ZICHUNGUZWE KUTOKANA NA WATOTO KULEWA,KUANGUKA NA KUZIMIA WANAPOTUMIA DAWA HIZO-Agosti 2,2017

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wameunga mkono hoja ya baadhi ya madiwani waliotaka ziangaliwe upya dawa za chanjo zinazosababisha wanafunzi wa shule za msingi kuanguka na kuzimia baada ya kunywa dawa hizo.

WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI YAANZA,WAZAZI KATAVI WAASWA KUNYONYESHA KWA MUDA WA KUTOSHA KWA AJILI YA AFYA ZA WATOTO-Agosti 2,2017

Ikiwa ni wiki ya unyonyeshaji duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo mwezi wa nane,wazazi  mkoani Katavi  wametakiwa kuwanyonyesha watoto mpaka wafikiapo umri wa miaka miwili ili kulinda afya zao.  Muuguzi wa kituo cha afya cha Town Clinic katika halmashauri ya  Manispaa ya Mpanda Mkoani  Katavi Lugalata Elias amesema  ikiwa ni wiki ya unyonyeshaji maziwa,  wazazi wanatakiwa kufuata ushauri wanaopewa na watoa  huduma ili kuepuka kudhoofika kwa afya ya mtoto.