Posts

Showing posts from November 10, 2017

RAIS MAGUFULI AMEKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO NCHINI UGANDA

Image
Na.Issack Gerald Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli amekutana na Watanzania waishio nchini Uganda katika Mji wa Masaka na kuwahakikishia kuwa hatua zilizoanza kuchukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuleta mabadiliko zimeanza kuzaa matunda. Mhe. Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Mawaziri na viongozi wakuu wa taasisi za Serikali ametaja baadhi ya matokeo hayo kuwa ni kusimamia vizuri uchumi unaokuwa kwa wastani wa asilimia 7, kudhibiti mfumuko wa bei hadi asilimia 5.1, kuokoa Shilingi Bilioni 238 walizokuwa wanalipwa watumishi hewa kwa mwaka na kuondoa watumishi wenye vyeti feki waliokuwa wakilipwa Shilingi Bilioni 142 kwa mwaka. Matokeo mengine ni kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka Shilingi Bilioni 850 hadi wastani wa Shilingi Trilioni 1.2 kupitia Mamlaka ya Mapato ( TRA ), kuanza ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa ( Standard Gauge ) kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma umbali wa kilometa 726 amba

MAHAKAMA KUU IMETENGUWA KUFUKUZWA WABUNGE 8 NA MADIWANI 2 WA CUFU

Image
Mahakama Kuu leo imetengua kufukuzwa kwa Wabunge 8 na Madiwani 2 wa Chama cha Wananchi,CUF na kusitisha pia mchakato wa kuwafukuza uanachama mpaka shauri la msingi litakaposikilizwa na kutolewa maamuzi. Aidha Mahakama hiyo pia imemzuia Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa,Prof.Ibrahim Haruna Lipumba, Magdalena Sakaya na Bodi ya Wadhamini ya CUF kujadili kuhusu uanachama wa Wabunge na Madiwani hao. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari, Uenezi Na Mahusiano Na Umma ya CUF Taifa, imeeleza kuwa, Mahakama Kuu imekubaliana na Hoja za Wabunge 8 wa chama hicho na imeona hoja za msingi za madai yao zinazopaswa kuangaliwa kuhusu uhalali wa masuala yote yaliyowasilishwa mbele ya Mahakama hiyo. Imefafanua kwamba, Mahakama Kuu pia imeyatupilia mbali mapingamizi mengine yote yaliyowekwa na Prof. Lipumba na Wenzake katika shauri hilo. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

MARAIS MAGUFULI NA MSEVEN WAMETOA MAAGIZO KWA MAWAZIRI WA NCHI ZOTE MBILI

Image
Na.Issack Gerald Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe.Yoweri Kaguta Museveni wamewaagiza Mawaziri wa nchi hizi mbili kujadiliana juu ya namna ya kuongeza biashara kati ya nchi hizi ili kupata manufaa makubwa zaidi ya uhusiano na ushirikiano wa kidugu uliopo. Viongozi hao wametoa kauli hiyo leo baada ya kufanya mazungumzo rasmi na kisha kuzungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ndogo ya Masaka nchini Uganda ambako Mhe.Rais Magufuli ameendelea na ziara yake rasmi ya kiserikali ya siku 3. Mhe. Rais Magufuli amesema kwa muda mrefu biashara kati ya Tanzania na Uganda imekuwa ni takribani shilingi Bilioni 200 kwa mwaka kiasi ambacho ni kidogo mno ikilinganishwa na fursa zilizopo, uhusiano na ushirikiano wa kidugu uliojengwa tangu enzi za Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere. Kuhusu hatua ambazo Tanzania imeanza kuchukua Mhe.Rais Magufuli amesema pamoja kuanza ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango

SUALA LA BOMOABOMOA KATA YA SITALIKE LIMEFIKA BUNGENI

Image
Na.Issack Gerald Wizara ya Mali asili na Utalii imesema haina mpango wa kuruhusu shughuli za kilimo katika Kijiji cha Matandalani na Igongwe kata ya Stalike iliyopo mkoani Katavi. Kauli hiyo imetolewa na naibu Waziri wa Mali asili na Utalii Japhet Hasunga alipo kuwa akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Nsimbo mkoa wa Katavi Richad Mbogo ambaye amehoji kwanini maeneo hayo yasi idhinishwe kisheria kwa shughuri za kibinadam. A kijibu swali hilo amesema serikali imetenga maeneo mengine kwa ajili ya wakazi walio ondolewa katika maeneo hayo yanayotajwa kuwa hifadhi za misitu. Katika hatua nyingine amefafanua uwepo wa mpango wa kuyapitia upya maeneo hayo ili kuona uwezekano wa kubadilisha matumizi pale itakapo onyesha ulazima huo. Mara kwa mara mamia ya wakazi mkoani Katavi wamekuwa wakiondolewa kinguvu katika maeneo mbali mbali ya vitongoji na Vijiji kwa madai ya kuvamia misitu. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

JESHI LA POLISI RUKWA:VIONGOZI WA DINI UOMBEENI MKOA WA RUKWA MAUAJI YAPUNGUWE

Image
Na.Issack Gerald JESHI la polisi mkoani Rukwa limewaomba viongozi wa dini wazidi kumuomba Mungu ili lifanikiwe kumaliza vitendo vya mauaji ya nayotokana na imani za kishirikina mkoni humo. Kamanda wa polisi mkoani humo George Kyando ametoa ombi hilo kwa uongozi wa kanisa la Pool Of Siloam wakati akipokea msaada wa matairi Saba ya magari yaliyotolewa na kanisa hilo kwa lengo la kulisaidia jeshi hilo kukabiliana na uhaba wa vitendea kazi.  Amesema kuwa miongoni mwa changamoto zinazoukabili mkoa wa Rukwa ni mauaji yanayotokana na imani za kishirikiana hivyo amewaomba viongozi wa dini kuuombea mkoa huo ili mauaji hayo yaishe.  Kamanda Kyando amesema jitihada zimefanyika za kutosha katika kukabiliana na kumaliza vitendo vya uhalifu lakini changamoto iliyopo ni mauaji yanayotokana na imani Za Kishirikiana. Katika hatua nyingine amesema jamii bila kumtegemea mwenyezi Mungu ni ngumu kuacha matendo maovu hivyo taasisi za dini zina jukumu hilo na iwapo wakiamua inawezekana kabi