Posts

Showing posts from January 26, 2018

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA UJUMBE WA PAUL KAGAME AAGANA NA BALOZI WA ZIMBABWE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli jana amekutana na Mjumbe Maalum wa Rais wa Rwanda na aliyewahi kuwa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt.Donald Kaberuka na kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya Tanzania na umoja wa Afrika (AU). Baada ya mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa Dkt.Kaberuka amesema uchumi wa Tanzania unakua vizuri na amempongeza Mhe.Rais Magufuli kwa jinsi anavyosimamia ukuaji wa uchumi huo. Dkt.Kaberuka amesema katika mazungumzo hayo pia amewasilisha ujumbe wa Rais wa Rwanda Mhe.Paul Kagame ambaye kuanzia mwezi huu atakua Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na ndiye aliyekabidhiwa majukumu ya kufanya mabadiliko ndani ya umoja huo. Wakati huo huo,Mhe. Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Zimbabwe hapa nchini anayemaliza muda wake Mhe. Edzai Chimonyo na kumpongeza kwa uwakilishi mzuri alioufanya kwa miaka 10 aliyoiwakilisha Zim

MAAMUZI YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA ZANZIBAR

KAMATI ya Ulinzi na Usalama  Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman imelazimika kutengua makubaliano ya zamani ya uchukuaji wa mizigo katika bandari ya Wete. Kamati hiyo imesema imetengua makubaliano hayo baada ya kubaini  kuwepo na mgogoro kati ya vikundi vya uchukuzi bandarini hapo. Vikundi vya uchukuzi ambavyo vilikuwa katika mgogoro wa uchukuzi  wa mizigo bandarini hapo ni Shikamana na Dausheni ambapo makubaliano hayo yalikuwa ni kwa wanachama wa Shikamana kubeba mizigo kwenye meli wakati Dausheni kubeba mizigo inayoingia bandarini hapo kwa njia ya majahazi  . Baada ya kufuta maamuzi hayo,Serikali imeutaka uongozi wa Shirika la bandari Tawi la Pemba kusimamia mgawanyo sawa wa uchukuzi wa mizigo  wa meli na majahazi. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

THAMINI UHAI WATOA MSAADA WA VIFAA TIBA MKONI KIGOMA

Shirika la Thamini uhai limejitolea dawa na vifaa tiba takribani aina 50 katika vituo vya afya 46 ndani ya mkoani Kigoma huu vyenye thamani ya shiling million 127 lengo likiwa ni kusaidia vituo hivyo kutoa huduma stahiki na kupunguza vifo kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga. Akizungumza katika makabidhiano ya vifaa hivyo daktari Bingwa wa magonjwa ya akina mama ya uzazi kutoka shirika hilo Dkt.Sande Dominick amewataka watoa huduma kutumia dawa na vifaa hivyo kwa lengo lililokusudiwa. Kwa miaka kadhaa sasa idadi ya akina mama wanaojifungulia katika vituo vya afya imeongezeka kutoka asilimia 38 hadi kufikia asilimia 60 yote ni kutokana na jitihada za mashirika binafsi ambapo  Meneja mahusiano na mawasiliano kutoka shirika la thamini uhai Viktoria Marijani amesema wamekuwa wakifanya hivyo ili kuokoa maisha ya mama na mtoto. Akimwakilisha Kaimu katibu tawala Mkoani Kigoma mhandisi Aziz Mtabuzi ,Dkt Lameck Mdengo ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake baada ya kup

WIKI YA SHERIA MKOANI KATAVI KUADHIMISHWA

Image
Wananchi wilaya ya mpanda mkoani katavi wametakiwa kujenga tabia ya kutembelea sehemu zinazotoa haki ili kupata uelewa wa masuala mbalimbali yanayohusu mahakama. Rai hiyo imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi Omar Hassan wakati akizungumza na mpanda redio ambapo ameeleza kuwepo mazoea kwa  wananchi  kuhitaji msaada mahakamani pindi wanapokuwa na matatizo ya kisheria. Aidha amebainisha njia ambazo mahakama imekuwa ikitumia katika utoaji elimu na msaada wa kisheria kwa wananchi ikiwemo mabango na kuwaalika wananchi kuhudhuria kusikiliza kesi mbalimbali zinazoendeshwa katika mahakama ya wazi. Katika hatua nyingine amesema maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani katavi yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya mahaka ya manspaa ya mpanda kuanzia tarehe 27 hadi 31 na kilele kufanyika tarehe mosi February huku kauli mbiu ikiwa ni “matumizi ya Tehama katika utoaji haki kwa wakati na kuzingatia maadili”. Kila mwaka mahaka ya Tanzania huadhimisha siku ya sheria ambayo huashiria kuanza ra

WANANCHI WATAKA ELIMU YA USALAMA BARABARANI MPANDA

Image
Wananchi katika halmashauri ya Manispaa Mpanda mkoa katavi wamelitaka jeshi la polisi kutoa elimu juu ya alama za barabarani ili kupunguza ajali . Wakizungumza kwa nyakati tofauti watumiaji wa barabara wamesema elimu ya usalama barabarani itawasaidia watembea kwa miguu kujiepusha na ajali za mara kwa mara zinazotokea kwa kutokujua matumizi ya alama hizo. Kamanda wa usalama barabarani mkoa Katavi John Mfinanga amesema elimu ya usalama barabarani na matumizi ya alama wanazitoa kupitia radio na katika vijiwe vya bodaboda ili kuwasaidia watembea kwa miguu kuweza kuzifahamu sheria na alama hizo. Mfinanga ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi pindi semina hizona kusema kwamba semina hizo zinatolewa bure na hazina malipo. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

JSI WARUDIA KUFANYA TENA MKOANI KATAVI

Image
Manispaa Ya Mpanda mkoani Katavi imesema  itaendelea kushirikiana na Shirika la JSI la Marekani linalojihusisha na masuala ya jamii katika kudhibiti mambo yanayomkatisha mtoto kutimiza ndoto zake. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Meya manispaa ya Mpanda Oswadi Rwezana wakati akikabidhi baiskeli 15 na kabati  zilizotolewa na shirika hilo JSI kwa  wasimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya jamii kutoka kata 15 za manispaa ya Mpanda Naye mratibu wa mafunzo na msimamizi wa JSI Clarence Mkoba amesema  kupitia shirika hilo limeazimia kushirikiana na wizara ya afya katika kukamilisha mradi huo kwa halmashauri 84 ikiwemo ya Mpanda Selestin Antony Muhenga na kutoka kata ya kasokola na Frola Bruno Mwasala Kutoka kata ya kazima ni Miongoni mwa watoa huduma ngazi ya jamii waliopatiwa Vifaa hivyo wamebainisha kutasaidia kuwafikia walengwa. Januari 12 mwaka huu,shirika la JSI lilitoa msaada wa baiskeli 5 kwa  wasimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya jamii wa Manispaa ya Mpanda. Habari za

MKURUGENZI MKOANI KATAVI ATAKA TV IKANUSHE HABARI ZA UONGO ILIZOTANGAZA KUHUSU HALMASHAURI YAKE

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Michael Nzyungu,amekanusha taarifa zilizotangazwa na kituo cha Televisheni cha Azam ambacho kimeripoti kuwa Halmashauri haijafikia malengo ya makusanyo ya mapato kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Bw.Nzyungu ametoa ufafanuzi huo wakati akizungumza na Vyombo vya habari Ofisini kwake. Aidha Bw.Nzyungu pamoja na mambo mengine amevishauri vyombo vya habari kutumia waandishi wenye umahiri wa kuandika habari ili kufikisha taarifa sahihi kwa jamii. Kwa mjibu wa MkurugenziTaarifa hizo zilichukuliwa kupitia kikao cha baraza maalumu la madiwani lililokuwa likijadili rasmu ya bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED