WIKI YA SHERIA MKOANI KATAVI KUADHIMISHWA

Wananchi wilaya ya mpanda mkoani katavi wametakiwa kujenga tabia ya kutembelea sehemu zinazotoa haki ili kupata uelewa wa masuala mbalimbali yanayohusu mahakama.

Rai hiyo imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi Omar Hassan wakati akizungumza na mpanda redio ambapo ameeleza kuwepo mazoea kwa wananchi  kuhitaji msaada mahakamani pindi wanapokuwa na matatizo ya kisheria.

Aidha amebainisha njia ambazo mahakama imekuwa ikitumia katika utoaji elimu na msaada wa kisheria kwa wananchi ikiwemo mabango na kuwaalika wananchi kuhudhuria kusikiliza kesi mbalimbali zinazoendeshwa katika mahakama ya wazi.

Katika hatua nyingine amesema maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani katavi yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya mahaka ya manspaa ya mpanda kuanzia tarehe 27 hadi 31 na kilele kufanyika tarehe mosi February huku kauli mbiu ikiwa ni “matumizi ya Tehama katika utoaji haki kwa wakati na kuzingatia maadili”.

Kila mwaka mahaka ya Tanzania huadhimisha siku ya sheria ambayo huashiria kuanza rasmi kwa shughuli za mahakama kwa mwaka.


Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA