JSI WARUDIA KUFANYA TENA MKOANI KATAVI

Manispaa Ya Mpanda mkoani Katavi imesema  itaendelea kushirikiana na Shirika la JSI la Marekani linalojihusisha na masuala ya jamii katika kudhibiti mambo yanayomkatisha mtoto kutimiza ndoto zake.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Meya manispaa ya Mpanda Oswadi Rwezana wakati akikabidhi baiskeli 15 na kabati  zilizotolewa na shirika hilo JSI kwa  wasimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya jamii kutoka kata 15 za manispaa ya Mpanda

Naye mratibu wa mafunzo na msimamizi wa JSI Clarence Mkoba amesema  kupitia shirika hilo limeazimia kushirikiana na wizara ya afya katika kukamilisha mradi huo kwa halmashauri 84 ikiwemo ya Mpanda

Selestin Antony Muhenga na kutoka kata ya kasokola na Frola Bruno Mwasala Kutoka kata ya kazima ni Miongoni mwa watoa huduma ngazi ya jamii waliopatiwa Vifaa hivyo wamebainisha kutasaidia kuwafikia walengwa.


Januari 12 mwaka huu,shirika la JSI lilitoa msaada wa baiskeli 5 kwa  wasimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya jamii wa Manispaa ya Mpanda.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA