Posts

Showing posts from August, 2015

UKAWA WAZINDUA KAMPENI ZA UCHAGUZI

Image
Na. mwandishi wetu DAR ES SALAAM. MGOMBEA Uraisi kupitia umoja wa Katiba ya wananchi Ukawa Mh: Edward Lowasa amesema endapo atapewa ridhaa ya kuongoza nchi ataipa kipaumbele elimu, Pamoja na afya.

CHADEMA WAPINGA TAMKO LA POLISI VIKUNDI VYA ULINZI NDANI YA VYAMA VYA SIASA ,CCM WAKUBALI

Na.Issack Gerald-MPANDA Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Wilayani Mpanda Mkoani Katavi kimepinga kauli ya jeshi la Polisi Mkoani hapa kupiga marufuku vikundi vya ulinzi katika vyama vya siasa wakati wa kampeni na uchaguzi.

CWT MPANDA YAKANUSHA KUWEPO MGOMO WA WALIMU JUMATATU AGOSTI 30

Na.Issack Gerald- MPANDA CHAMA  cha Walimu CWT Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi Kimekanusha taarifa za Kuwepo kwa Mgomo wa Walimu siku ya Jumatatu wa Kuishinikiza serikali kuwalipa  Madai yao. Akingumza jana na P5 TANZANIA Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Mpanda bwana Jumanne Msomba amesema Ofisi yake haina taarifa za Mgomo huo na kuwataka walimu kusubiri tamko la Rais wa Chama cha Walimu taifa. Wakati   taarifa za kuwepo kwa  Mgomo wa walimu Wilayani Mpanda zikikanushwa  Kesho  Viongozi wa Chama cha Walimu taifa wanatarajia Kukutana na Viongozi wa Serikali ili kutafuta suluhisho la Madai hayo.

WANAFUNZI WAOMBA KUENDELEZWA ELIMU

Image
Wanafunzi wakiwa darasani Shule ya msini Mpanda iliyopo Manispaa ya Mpanda NA.Issack Gerald-Mpanda Wanafunzi wa shule ya msingi Mpanda  iliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamewaomba wazazi na walezi kuwaendeleza kielimu wanapokuwa wamehitimu masomo ya darasa la saba na kufaulu kujiunga na kidato cha kwanza.

VIKUNDI VYA ULINZI VYAMA VYA SIASA VYAPIGWA MARUFUKU

Na.Issack Gerald-KATAVI Jeshi la Polisi Mkoani Katavi limevitaka vyama vya siasa na wafuasi wao kuzingatia kanuni,sheria na taratibu za vyama vyao kudumisha amani ya nchi na kuepuka makosa ya jinai yanayoweza kuwatia hatiani.

SIDO KUFUNGUA OFISI ZAKE KATAVI

Na.Issack Gerald-KATAVI Shirika la viwanda vidogovidogo SIDO Mikoa ya Ruka na Katavi, linatarajia kuanzisha ofisi Mkoani Katavi kusogeza huduma na kutatua changampoto mbalimbali   zinazowakabili wafanyabiashara zikiwemo mikopo na masoko

MARUFUKU VITUO VYA POLISI KUCHOMWA MOTO

Image
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limekaririwa likisema linawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kuchoma kituo kidogo cha Polisi kilichopo Mofu wilayani Kilombero baada ya kukivamia kwa lengo la kutaka polisi wawape mtuhumiwa wa mauaji ili wamuue. IGP ERNEST MANGU Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alibainisha kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 20, mwaka huu na chanzo ni wanakijiji wapatao 100 kufika katika kituo hicho wakimtaka mtuhumiwa wa mauaji ya mkewe. Tukio la kuchomwa kwa kituo hicho limetokea ikiwa ni siku chache baada ya wananchi wenye hasira kuvamia Kituo cha Polisi Bunju A kilichopo Dar es Salaam na kukichoma moto kwa kile kilichoelezwa ni dereva kumgonga mwanafunzi na kupoteza maisha. Tuseme tu hapa kuwa utamaduni huu wa kuchoma vituo vya Polisi ni lazima ukomeshwe kwa sababu si suluhu la wananchi kupata kile wanachodai zaidi ya kuisababishia Serikali hasara na wakati huo huo kukwamisha huduma nyingine za kijamii. Kama kuna tatizo limetokea ni

VIJANA WATAKIWA KUTOUZA UTU WAO KATIKA MASUALA YA SIASA

Image
  Vijana katika picha ya pamoja Na.Stanley Msigwa-Mpanda. VIJANA Mkoani Katavi wametakiwa kutouza utu wao kwa kutumiwa na wanasiasa kwa maslahi yao na badala yake watathmini hatima ya maisha yao.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA SITA-JAMII YATAKIWA KUWATAMBUA WATOTO WENYE ULEMAVU

Na.Issack Gerald -MPANDA. JAMII Mkoani Katavi imeombwa kutambua uwepo wa watoto wenye ulemavu, ili kuwapatia haki za msingi sawa na  watoto wengine.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA TANO- 20,162 KATI YA 22,596 WAJIANDIKISHA MAKAZI MAPYA KATUMBA

Image
Wakazi wa makazi mapya ya Katumba wakijandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura Na.Agness Mnubi NSIMBO. WANANCHI 20,162 kati ya 22,596 sawa na asilimia 89 ya wakazi wapya, Wilayani Nsimbo Mkoani Katavi wamejiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA NNE,UBAKAJI WA WANAWAKE,WIZI WAKITHIRI POLISI JAMII WAKACHA ULINZI

NA . Issack Gerald- MPANDA Kukosekana kwa uongozi imara katika sekta ya ulinzi na usalama,kumeababisha vitendo vya wizi na ubakaji kwa wanawake kukithiri katika mtaa wa Msasani Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA TATU KATIKA SISA MGOMBEA UBUNGE CUF MPANDA ASHINDWA KUREJESHA FOMU,AFISA UCHAGUZI ALONGA

NA . Meshack Ngumba- MPANDA Chama cha Wananchi Cuf Kimeshindwa Kurejesha fomu ya Mgombea wa Ubunge Kupitia chama hicho Katika Jimbo la Mpanda Mjini Katika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi manispaa ya Mpanda.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA PILI-WANNE WASHIKILIWA NA POLISI KATAVI KWA KUPORA ZAIDI YA MILIONI 7,SILAHA ZA KIVITA PIA ZAKAMATWA

Na.Issack Gerald - KATAVI Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu wanne wanaosadikika kuwa majambazi Wilayani Mpanda kwa tuhuma za kujeruhi na kupora kiasi cha shilingi milioni saba.

MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA KWANZA-MWANAMKE AKATWA PUA,ACHANWA SIKIO MMEWE AKATAA KUELEZA SABABU

Na.Issack Gerald - MPANDA. Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Magdarena Joseph Mkazi wa Mwamkulu Senatalumbanga Ma n ispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amekatwa pua na kuchanwa sikio na mme wake Lukona Machimba,Kutokana na ugomvi wa kifamilia.

JESHI LA POLISI KATAVI LASISITIZA KUTUNZA SIRI ZA RAIA WEMA KUPAMBANA NA UHARIFU

Na.Issack Gerald-KATAVI JESHI la Polisi Mkoani Katavi limesema linaendelea na utaratibu wa kutunza siri za raia wema wanaoshirikiana na Polisi kuwafichua waharifu wanaopelekea kusababisha madhara kwa wananchi.

20,162 KATI YA 22,596 WAJIANDIKISHA DAFTARI LA MPIGA KURA MAKAZI MAPYA YA KATUMBA

Image
  Wakazi wakijiandikisha katika daftari mpiga kura NA . Agness Mnubi-Nsimbo WANANCHI 20,162 kati ya 22,596 sawa na asilimia 89 ya wakazi wapya, Wilayani Nsimbo Mkoani Katavi wamejiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura.

CHAMA CHA MADEREVA WAFANYAKAZI TANZANIA (TADWU) KUTOA TAMKO LEO KUHUSU MADEREVA NA WAAJIRI WAO

Image
CHAMA cha Madereva Wafanyakazi Tanzania (TADWU), kimesema madereva nchi nzima watakuwa mapumziko kwa wiki moja au zaidi kwa ajili ya kujiunga na mafunzo ya udereva.

MAJAMBAZI YAPORA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI SABA,YAJERUHI PIA

Na.Issack Gerald-KATAVI Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu wanne Wilayani Mpanda kwa tuhuma za kujeruhi na kupora kiasi cha shilingi milioni saba.

SERIKALI,JAMII WAOMBWA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA

NA.Issack Gerald-NSIMBO Serikali na Jamii kwa ujumla Mkoani Katavi imeombwa   kutoa misaada kwa watoto yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

YASIKUPITE,MATUKIO WIKI HII KATAVI KATIKA SIASA,UCHUMI,MAKUNDI MAALUMU

SUALA LA SIASA Na.Issack Gerald-Katavi WAGOMBEA wa nafasi mbalimbali za uongozi Mkoani Katavi  wameaswa kuacha kutoa rushwa ili kujipatia ushindi katika uchaguzi ujao.

IGP MANGU AHIMIZA AMANI KATAVI

NA.Issack Gerald-Katavi MKUU wa jeshi la polisi nchini Inspekta jenerali Ernest Mangu, amesema kila mtu atimize wajibu wake ili kuhakikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, unafanyika kwa amani na utulivu.

WAKULIMA,WAFUGAJI MPANDA WATOA MAONI KUHUSU SHEREHE ZA NANENANE

NA.Issack Gerald-Mpanda SIKU mbili baada ya maonesho ya kilimo na ufugaji   maarufu kama nane nane, baadhi ya wakulima   pamoja na wafugaji Mkoani Katavi wametoa maoni na mapendekezo kuhusu sekta ya kilimo.

UHAKIKI DAFTARI LA MPIGA KURA NSIMBO WAFANYIKA

NA. Agness Mnub- KATAVI ZOEZI la Kuhakiki taarifa katika daftari la Kudumu la Mpiga Kura limeanza Katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi Kufuatia Tangazo lililotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi juu ya Zoezi hilo.

WANASIASA KIKWAZO UTEKELEZAJI AGIZO LA MKURUGENZI

NA. Alinanuswe Edward-Katavi Wanasiasa wamedaiwa kuchangia kukwamisha utekelezaji   wa agizo la Manispaa ya mpanda lilitolewa mwishoni mwa mwezi mei likiwataka watu wote wanwanaosafisha magari yao katika mto misunkumilo kuacha mara moja.

BREAKING NEWS- IGP ERNEST MANGU KUWASILI MKOANI KATAVI LEO AGOSTI 09 KWA ZIARA YA SIKU MBILI MKOANI KATAVI

Image
IGP Ernest Mangu NA.Issack Gerald-Katavi Mkuu wa jeshi la polisi Tanzania anatarajia kuwasili mkoani katavi leo Agosti 09 kwa ziara ya kikazi. Akiwa katika zaiara jioni atakula chakula cha pamoja na wadau wa masuala ya ulinzi >>>>>>>>>>Endelea kuwa nami kufahamu kila kitakachojili<<<<<<<<<<<<<

PITIA VICHWA VYA MAGAZETI LEO AGOSTI 08,2015 UPATE HABARI KUBWA TANAZANIA NA NJE YA TANZANIA

Image

UVAMIZI OFISI ZA CCM SUMBAWANGA RUKWA,SAMANI ZA MWENYEKITI VYATUPWA NJE

Na.Mwandisi wetu-SUMBAWANGA. Baadhi ya wakazi wa manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa wanaosadikiwa kuwa ni wanachama wa chama cha Mapinduzi, juzi wameivamia ofisi ya chama hicho ya wilaya ya Sumbawanga mjini.

IGP MANGU ZIARANI KATAVI KESHO NA KESHO KUTWA

Image
Mkuu wa Jeshi  la polisi Tanzania IGP Ernset Mangu Na.Issack Gerald-Katavi MKUU wa jeshi la polisi nchini Inspekta Jenerali Ernest Mangu anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Katavi kuanzia tarehe 9 hadi 11 mwezi huu. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Katavi,ASP. Dhahiri Kidavashari, imesema kuwa katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, IGP Ernest Mangu,  atakuwa na fursa ya kuzungumza na wadau mbali mbali katika hoteli ya Lyamba Lya Mfipa majira ya jioni. Katika hafla hiyo waalikwa watapata chakula cha jioni pamoja na Inspekta Jenerali wa polisi hapa nchini.

UNAMFAHAMU MAGUFULI NA MAISHA YAKE TANGU KUZALIWA HADI SIASA?ONGEZA CHAKULACHA UBONGO NA P5 TANZANIA

Image
Mhandisi John Pombe Magufuli JOHN POMBE MAGUFULI Magufuli ni Nani? Lakini je Daktari John Magufuli ni Nani? Mgombea wa urais wa chama cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2015 Daktari John Pombe Joseph Magufuli ni mbunge wa jimbo la Chato lililoko mkoa wa Geita na ni waziri wa ujenzi wa Tanzania. Alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 wilayani Chato Mkoani Kagera. Kielimu, daktari Magufuli ana Stashahada ya elimu ya sayansi akibobea kwenye masomo ya Kemia, Hisabati. Mgombea huyo wa urais ana shahada ya umahiri wa Sayansi na shahada ya uzamivu ya kemia. Aidha daktari Magufuli amewahi kufundisha katika shule ya sekondari Sengerema miaka ya themanini kisha akajiunga na mafunzo ya JKT . Alizaliwa Oktoba 1959 Mhandisi John Pombe Magufuli wakati akijiunga na ccm 1995  Alipohitimu, daktari Magufuli na aliaanza kufanya kazi katika kiwanda cha ‘Nyanza Cooperative Union akiwa Mkemia kabla ya kuondoka hapo na kuwania ubunge. Magufuli alianza mbio za ubunge mwaka 1995

WAKAZI MPANDA WANDELEA KUWA GIZANI UMEME KUKATIKA,VIWANDA VYAKOSA UMEME SHUGHULI ZASIMAMA KWA MWEZI SASA

NA.Issack Gerald TATIZO la kukatika Umeme mara kwa mara Mkoani Katavi   limesababisha kuzorota kwa biashara ya mchele, kutokana na kukwama kwa ukoboaji wa mpunga zao linalotegemewa na wakazi wengi   mkoani Katavi.

MGOGORO WA ARDHI MTAA WA NSEMULWA BADO MBICHI,MKURUGENZI ATOA JIBU BILA SULUHU

NA.Issack Gerald-Katavi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imesema haijapokea malalamiko ya wakazi wa mtaa wa Nsemulwa kutopimiwa viwanja vyao na kutozwa kiwango kikubwa cha pesa tofauti na kilichopangwa kupitia mikutano.

UHAKIKI MAJINA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MANISPAA YA MPANDA WAKWAMA,MKURUGENZI KUTOA TAARIFA BAADA YA VIFAA KUAWASILISHWA

NA.Issack Gerald-KATAVI ZOEZI la uhakiki wa taarifa katika daftari la kudumu la mpiga kura limeelezwa kuchelewa kuanza katika Manispaa ya Mpanda kutokana na kucheleweshwa kwa vifaa, zikiwemo mashine za BVR.

WAKAZI NSEMULWA KUWASHTAKI MAAFISA ARDHI MANISPAA YA MPANDA KWA WAZIRI WA ARDHI WAKIPINGA USUMBUFU UPIMAJI WA VIWANJA

NA.Issack Gerald-KATAVI WAKAZI wa mtaa wa Nsemulwa Kata ya Nsemulwa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamekusudia kumuita Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi kutatua migogoro ya ardhi, wakiwatuhumu maafisa ardhi Wilayani Mpanda kushindwa kutatua migogoro hiyo kwa miaka mitatu sasa.

P5 TANZANIA INAKULETEA WASIFU WA WAGOMBEA KITI CHA URAIS WA TANZANIA,TUNAANZA NDANI YA UKAWA,Mh.Edward Lowassa

Image
  Edward Lowassa aliyeshika maikikrofoni na aliyevaa shati jeupe Edward Ngoyai Lowassa Edward Ngoyai Lowassa Mbunge Bunge la Tanzania Jimbo la uchaguzi Monduli ( Arusha ) Tarehe ya kuzaliwa 26 Agosti 1953 Chama CHADEMA (tangu 28/07/15) Tar. ya kuingia bunge tangu 1990 Alirudishwa mwaka 2005 Waziri Mkuu wa Tanzania Alingia ofisini 2005 Alitanguliwa na Frederick Sumaye Dini Mkristo Elimu yake Chuo Kikuu Digrii anazoshika MA (Development Studies) University of Bath (Uing.) Kazi mwanasiasa Edward Ngoyayi Lowassa (amezaliwa 26 Agosti 1953 ) ni mwanasiasa nchini Tanzania . Alichaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kumi wa nchi hiyo tarehe 30 Desemba 2005 akajiuzulu tarehe 7 Februari 2008 kwa kutajwa katika kamati ya bunge ya uchunguzi katika utoaji wa tenda kwa kampuni ya umeme

UKAWA WAMPITISHA RASMI LOWASSA KUGOMBEA URAIS WA TANZANIA

Image
  Edward Lowassa Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema kupitia Ukawa NA MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM Chama cha demokrasia na maendeleo chadema   leo kimemuidhinisha Edward lowasa kuwa mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika   mwezi Oktoba mwaka huu.  Wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema uliofanyika   leo Jijini   Dar Es salaam wamepiga kura ya   kuridhia kiongozi huyo aliyejiunga na upinzani akitokea chama tawala CCM kuwa mgombea   Kiti hicho cha   urais   Kupitia chama hicho.  Mwanasiasa huyo Mkongwe hapa Nchini amekuwa   akiyagawa   maoni ya Watanzania tangu akihame chama cha Mapinduzi na Kuhamia chama cha   chadema   tang u vikao vya uteuzi vya ccm   kumpitisha mgombea wa urais kulikata jina lake. Hata hivyo katibu mkuu wa chadema Wilbroad Slaa hakuhudhuria mkutano huo mkuu Kutokana na kuwepo kwa taarifa kuwa hakufurahishwa   na uamuzi wa chadema kumpokea Lowasa. SOMA HAPA KUMFAHAMU LOWASSA

VIONGOZI WA UMMA TANZANIA WATAKIWA KUWA WAZALENDO KUPITIA WANAOWAONGOZA

  Na.Issack Gerald-KATAVI Viongozi wa umma hapa nchini wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia Uzalendokatika kutekeleza mahitaji ya wanaowaongozana siyo kwa maslahi binafsi.