Posts

Showing posts from April 4, 2018

WAZIRI MKUU AWASILISHA TAARIFA YA MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA KAZI ZA SERIKALI

Image
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mpa akufikia Februari 2018 Serikali ya Awamu ya Tano imeanzisha viwanda vipya 3,306. Ametoa kauli hiyo leo Bungeni mjini Dodoma,wakati akiwasilisha taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa kazi za Serikali kwa mwaka 2017/2018 na mwelekeo wa kazi za Serikali kwa mwaka 2018/2019 kwenye mkutano wa 11 wa Bunge.

RC KATAVI AZINDUA VIKAO VYA KIELIMU ATOA MAAGIZO KWA WARATIBU WA ELIMU

Image
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga,amewaagiza viongozi mbalimbali wa elimu mkoani Katavi kuhakikisha wanashirikiana na wadau wa elimu katika maeneo yao ili kutatua tatizo la Mkoa wa Katavi kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa kwa elimu ya msingi,kidato cha nne na sita. Miongoni mwa viongozi ambao wamelengwa na agizo la Mkuu wa Mkoa ni pamoja na waratibu elimu kata,wakuu wa shule,walimu wakuu,bodi na kamati mbalimbali za shule.