Posts

Showing posts from July 19, 2017

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU 14 KWA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KUFUNGA MASHINE ZA KIELECTRONIKI ZA KUTOA RISITI-Julai 19,2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa siku 14 kwa wamiliki wa vituo vyote vya mafuta nchini kufunga na kutumia mashine za kielektroniki za kutolea risiti ( Electronic Fiscal Petrol Printer ).

WILAYA YA UYUI YAANZA KUTOA MIKOPO KWA VIJANA NA WANAWAKE-Julai 19,2017

HALMASHAURI ya wilaya ya Uyui mkoani Tabora,imeanza kutoa mikopo kwa vikundi vya ujasirimali vya wanawake na vijana katika kata ya Ilolangulu wilayani humo ili kuwasaidia wananchi maskini kujikwamua kiuchumi.

KITUO CHA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU MPANDA WAOMBA MSAADA KUKIDHI MAHITAJI YAO MUHIMU-Julai 19,2017

KITUO cha Gethsemani cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu kilichopo kata ya Katumba Halmashauri ya Wilaya Nsimbo Mkoani Katavi,kimeomba mchango wa hali na mali kutoka kwa jamii ili kupata pesa kukidhi mahitaji muhimu ya watoto wanaoishi katika kituo hicho.

WAJASIAMALI KATAVI WASEMA KUHAMIA ENEO JIPYA KUMEWAONGEZEA MAPATO,WAIOMBA SERIKALI KUBORESHA HUDUMA MUHIMU KAMA MAJI ENEO LA KAZI-Julai 19,2017

WAJASILIAMALI wanaojihusisha na utengenezaji wa vitu vya thamani vikiwemo Vitanda,kabati na meza waliopo kata ya Misunkumilo  halmashauli ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi,wameiomba serikali kuboresha miundo mbinu katika eneo hilo.

MKUU WA MKOA WA KATAVI MEJA JENERAL MSTAAFU RAFAEL MUHUGA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA KUZALISHA MAZIWA MKOANI KATAVI-Julai 19,2017

Image
Katika picha,Wa tatu kutoka Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga akisikiliza maelezo kuhusu kiwanda kutoka kwa mwenyekiti wa Kashaulili Livestock Keepers Bw.Andrea Fumbi(wa pili kutoka kushoto) (Picha na P5tanzania.blogspot.com) Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga ameweka jiwe la msingi katika kiwanda cha maziwa cha  Kashaulili Livestock Keepers Saccos kinachojengwa katika kata ya Makakanyagio Halmashauli ya  Manispaa Mpanda. Jiwe la Msingi katika mtaa wa Mpadeco Kata ya Makanyagio kinapojengwa kiwanda cha kuzalisha maziwa Katika uzinduzizi huo,Mkuu wa  Mkoa ametoa wito  kwa wakazi wa Mkoa  wa Katavi  kujitokeza kwa wingi kuwekeza viwanda ili kujenga Tanzania ya viwanda kama serikali ya awamu ya tano ilivyoagiza. Kwa upande wake Mwenyekiti wa kiwanda hicho chenye wanachama zaidi ya 50 Andrea Fumbi amesema,kiwanda hicho kitagharimu zaidi ya shilingi milioni 600 kwa udhamini wa Benkya TIB,ambapo kinatarajia kuzalisha