Posts

Showing posts from September 2, 2017

TRA MKOANI RUKWA YASAKA MAPATO KWA UDI NA UVUMBA YASHTUKIZA UKAGUZI WA MAGARI HASA YA MIKOANI-Septemba 2,2017-

Image
MAMLAKA ya mapato TRA mkoani Rukwa imefanya msako maalumu kwa lengo la kukagua mabasi ya abiria pamoja na ya mizigo ambayo haijalipiwa kodi mbalimbali.

MH.LOWASSA ATOA POLE KWA RAIS UHURU KENYATTA MAHAKAMA KUFUTA USHINDI WAKE-Septemba 2,2017

Image
Mh.Edward Lowassa Mjumbe wa kamati kuu ya (CHADEMA) na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ametoa pole kwa aliyekuwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta kufutia mahakama ya juu nchini humo kufuta matokeo ya uchaguzi wa Urais uliofanyika Agosti 8 mwaka huu.

WAFANYABIASAHARA WA MITUMBA WALAANI KUONDOLEWA KWA NGUVU KATIKA SOKO LA MPANDA HOTEL-Septemba 2,2017

Image
WAFANYABIASHARA wa mitumba katika soko la Mpanda Hoteli Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamelaani kitendo cha kutaka kuondolewa katika maeneo ya biashara zao kwa kinachodaiwa kuwa hawaruhusiwi kufanya biashara katika eneo hilo.

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA NA WAUMINI KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO-Septemba 2,2017

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli leo wameungana na waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato,Usharika wa Magomeni Mwembechai Jijini Dar es Salaam kusali Ibada ya Sabato.

RAIS UHURU KENYATTA ASEMA HAKUBALIANI NA MAAMUZI YA MAHAKAMA HUKU WILLIUM RUTO NAYE AKITAKA TUME YA UCHAGUZI KUTANGAZA TAREHE MPYA YA UCHAGUZI-Septemba 2,2017

Image
Naibu wa rais wa Kenya William Ruto NAIBU rais wa Kenya,William Ruto,ameitaka tume ya uchaguzi ya Kenya kutaja rasmi siku ya kurudiwa kwa uchaguzi wa urais nchini humo. Hatua ni baada ya Ijumaa mahakama ya juu zaidi kubatilisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta wa uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita,ikisema kulikuwa na dosari kubwa zilizokiuka katiba ya Kenya. Kiongozi wa upinzani Raila Odinga aliyeusifu uamuzi huo wa mahakama,papo hapo alishutumu vikali tume ya uchaguzi ya Kenya IEBC na pia kuwalaumu waangalizi wa kumataifa kwa kile alichokitaja ' kuhalalisha udanganyifu uliotokea na kutaka uchunguzi zaidi ufanyike. Amewataka waliohusishwa na udanganyifu huo kujiuzulu , kufutwa kazi na hata kuchukuliwa hatua za kisheria wakisema kamwe hawawezi kuaminiwa kusimamia uchaguzi ujao. Rais uhuru Kenyatta akiwahutubia wafuasi wake jijini Nairobi. Alisema kuwa majaji waliobatilisha uchaguzi wkeni ni wakora Kwa upande wake Rais Uhuru Kenyatta amesema

WANAFUNZI 7 WAFARIKI DUNIA BAADA YA BWENI LAO KUTEKETEA KWA MOTO NCHINI KENYA-Septemba 2

Image
WANAFUNZI saba wamefariki na makumi wengine wakijeruhiwa baada ya moto kuchoma bweni la shule ya Moi Girls mjini Nairobi. Baadhi ya wazazi na wakaazi wa eneo la shule hiyo waliojitokeza kujaribu kuwajulia hali wanawao katika shule hiyo Magari ya kukabiliana na dharura yalifilka katika shule hiyo mapema alfajiri ili kuswanusuru walioathirika Maafisa wa polisi wakishika doria nje ya shule ya Moi Girls liliopo jijini Nairobi nchini Kenya

AKUTWA AMEFARIKI DUNIA,MAKTARI,JESHI LA POLISI LASITA KUELEZEA TUKIO WASEMA WATAELEZA BAADA YA UCHUNGUZI KUFANYIKA-sEPTEMBA 2,2017

Mtu mmoja ambaye amefahamika kwa jina moja la Tadeo amekutwa amekufa katika  bustani iliyopo pembezoni mwa mto mpanda kata ya Makanyagio manispaa ya Mpanda.

MBUNGE MTEULE WA CUF AFARIKI DUNIA-Septemba 2,2017

Image
Bi Hindu Mwenda Mmoja wa wabunge walioteuliwa kuchukuwa nafasi za wabunge nane wa chama cha wananchi (CUF) waliovuliwa uanachama na mwenyekiti wa CUF,Bi Hindu Mwenda amefariki dunia.