Posts

Showing posts from January, 2016

AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA UHARIBIFU WA MALI,YUMO PIA ALIYETISHIA KUUWA KWA MANENO

Na.Boniface Mpagape-Mpanda MTU mmoja mkazi wa Kapalangeo-kazima katika manispaa ya Mpanda Bw. Joseph Saleh kajunja amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuharibu mali.

ASKARI POLISI KATAVI APIGWA RISASI YA TUMBONI AFA PAPOHAPO ENEO LA TUKIO- P5 TANZANIA INAKULETEA UNDANI ZAIDI

Na.Issack Gerald-Mpanda Askari wa jeshi la polisi Mkoani Katavi H305PC Nobert Stanslaus Chacha amekufa baada ya kupigwa risasi maeneo ya Kapanda juu kata ya Machimboni Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda.

BIL.31 ZAPITISHWA NA BALAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA MWAKA WA FEDHA 2016/2017

Na.Lutakilwa Lutobeka-Mpanda Jumla ya madiwani 20 katika halimashauri ya wilaya ya Mpanda wamepitisha bajeti ya shilingi bilioni 31 ya mwaka 2016/2017 iliyopendekezwa na halmashauri hiyo.

TAARIFA KAMILI YA POLISI KUHUSU WATU KUFA MAJI KATAVI BAADA YA GARI KUSOMBWA NA MAJI HII HAPA,POLISI WASUBIRI MIILI IELEE NDIPO IOKOLEWE

Na.Issack Gerald- Katavi Miili mitano ya watu walikufa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji katika Mto Koga uliopo mpakani mwa Mkoa wa Katavi na Tabora imepatikana huku miili mingine mitano ikiwa hajajulikana ilipo.

TANZANIA YATANGAZA MIKAKATI ZAIDI UJENZI MIUNDOMBINU YA BARABARA KATAVI

Na.Issack Gerald-Dodoma Serikali imesema kuwa inaendelea na mikakati ya kuhakikisha inatenga fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi barabara za Mkoa wa Katavi kwa kiwango cha lami kuunganisha na maeneo mengine jirani kwa ajili ya kukuza uchumi mkoani Katavi.

SITA WAFA MAJI BAADA YA GARI KUSOMBWA NA MAJI KATAVI, ZAIDI YA WATANO BADO KUPATIKANA,MKUU WA MKOA APIGA MARUFUKU MAGARI KUSAFIRI KUPITA MTO KOGA

Na.Issack Gerald-Katavi Watu wapatao 6 wameripotiwa kupoteza maisha katika daraja la mto Koga lililopo mpakani mwa mikoa ya Katavi na Tabora, baada ya maji yaliyotokana na mvua kufurika na kusababisha watu hao kusombwa na maji.

MKUU WA WILAYA NKASI ATOA RAI KWA MADIWANI WILAYANI HUMO KUHAKIKISHA WANATATUA CHANGAMOTO YA MAPATO YA HALMASHAURI

Na.Issack Gerald- Nkasi. MKUU wa Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa Idd Hassan Kimanta amewaasa madiwani wa Wilaya hiyo kuhakikisha suala la kukuza mapato ya Halmashauri inakuwa ajenda ya kudumu kwao.

BREAKING NEWS : WAHAMIAJI HARAMU 8 RAIA WA ETHIOPIA WANASWA IRINGA-P5 TANZANIA INAKUSOGEZEA HIYO

Image
Na.Issack Gerald-Iringa Jeshi la polisi Mkoani Iringa limewakamata wahamiaji haramu 8 Raia wa Ethiopia waliokiuwa wakisafiri isivyo halali na bila kibali cha kuingia nchini wakiwa wamepakiwa na gari lililokuwa limebeba magazeti.                                                Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa Peter Kakamba

ACHOMWA KISU WILAYANI MPANDA UTUMBO WATOKA NJE,MHUSIKA ATOKOMEA KUSIKOJULIKANA POLISI KUMSAKA MHUSIKA.

Na.Issack Gerald-Katavi Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Elia Edward(40), makazi wa mchangani alichomwa tumboni na kitu chenye ncha kali na kisha utumbo wake kutoka nje na mtu asiyemfahamu.

UJENZI WA BARABARA KIWANGO CHA LAMI KUTOKA MPANDA HADI SUMBAWANGA KUKAMILIKA 2016

Image
Na. Issack Gerald -Dodoma SERIKALI imesema ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Sumbawanga kwa kiwango cha lami unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2016.                                                       Bungeni Dodoma                                                       Jengo linalotumika katika vikao vya bunge Mjini Dodoma

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUPATA KIPIGO KIKALI-P5 TANZANIA MEDIA INAKUSOGEZEA HIYO

Na.Issack Gerald-Mlele Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ramadhani Ally (20), mkazi wa Kalovya Inyonga,amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya Inyonga kufuatia kipigo kikali alichokipata toka kwa Ntemwa Kabembenya(26) mkazi wa Ipwaga.

MKUU WA MKOA WA KATAVI ATAKA KILA MKAZI KUWA MLINZI WA MAZINGIRA YANAYOMZUNGUKA

Na.Issack Gerald-Mpanda Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk.Ibrahim Msengi,amemtaka kila wakazi wa Mkoa wa Katavi kuwa mlinzi wa mazingira yanayomzunguka.

MAMA AMUUA MTOTO WAKE AMFUNGA KAMBA SHINGONI AMTUNDIKA JUU YA MWEMBE MPANDA.

Na.Issack Gerald-Katavi Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linamshikilia Sado Roket (26) mkazi wa Mnyakasi kwa kumuua mtoto wake Nchambi Tungu (11) mkazi wa Mnyakasi   kwa kumpiga kwa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake.

WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA,MMOJA KUTISHIA KUUWA KWA MANENO MWINGINE KUUZA KIWANJA KWA ZAIDI YA MTU MMOJA

Na.Issack Gerald-Mpanda MTU mmoja amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda jana, akikabiliwa na shtaka la kuuza kiwanja kwa gharama ya shilingi laki sita na baadaye kukiuza kwa mtu mwingine.

WANAWAKE WAISHI KWA MIGOGORO KATIKA NDOA KISA UCHAGUZI OKTOBA 25,2015

Image
Na.Issack Gerald-Mpanda BAADHI ya wanawake Mkoani Katavi wameiomba Serikali na wadau mbalimbali kuelimisha   jamii kwa chaguzi zijazo ili kukomesha tabia ya ukandamizaji unaofanywa na baadhi ya wanaume kwa kuwachagulia vyama vya siasa wake zao.                                                          Baadhi ya wanawake ambao wamezungumza na P5 TANZANIA (Picha na Issack Gerald)

MATUKIO YA WIKI MKOANI KATAVI NA TANZANIA KWA UJUMLA KUANZIA JANUARI 18-23,2016.

Tuesday, 19 January 2016 WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA MAKOSA MBALIMBALI LIKIWEMO SHAMBULIO LA MWILI. Posted By: Issack Gerald | At: Tuesday, January 19, 2016 Na.Issack Gerald-MPANDA VIJANA watatu wakazi wa Mpanda mjini jana wamefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda, wakikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili.

UDSM YAENDESHA KONGAMANO LA TAFAKURI YA UCHAUZI WA MWAKA 2015,MENGI YAIBULIWA.

Image
Na.Mwandishi wetu-Dar es salaam Watanzania wametakiwa kuacha ushabiki wa vyama vya siasa na badala yake wajikite kutatua matatizo ya kitaifa.                                                       Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Jajji Joseph Sinde Warioba

AFISA MTENDAJI WILAYANI MPANDA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KWA TUHUMA ZA RUSHWA

Na.Boniface Mpagape-Mpanda TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Katavi, imemfikisha katika mahakama ya wilaya ya Mpanda   Afisa mtendaji wa mtaa wa Kawajense akikabiliwa na shtaka la kushawishi na kupokea rushwa ya shilingi elfu thelathini.

WANAFUNZI 1137 WATOKOMEA KUSIKOJULIKANA,AFISA ELIMU KUTANGAZA MSAKO NYUMBA KWA NYUMBA.

Na.Issack Gerald-Nkasi. WANAFUNZI wapatao 1137 kati ya 2257   hawajaripoti shule kuanza kidato cha kwanza mwaka huu katika Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa licha ya serikali kutoa elimu bure.

TAMISEMI YAAGIZWA KUSIMAMIA VIZURI HALMASHAURI

Na.Issack Gerald-Katavi WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo kitovu cha nchi na kwamba kila Mtanzania ameelekeza jicho lake pale kwa sababu anasubiri kupata huduma ya msingi.

MAAFISA ELIMU NSIMBO WAPEWA SIKU 6 KUHAKIKISHA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUINGIA SEKONDARI WANARIPOTI

Na.Agness Mnubi-Nsimbo. MAAFISA elimu sekondari katika halmashauri ya wilaya ya Nsimbo wamepewa siku 6 kuanzia jana, kuhakikisha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza wanaripoti.

JAMII NSIMBO YAOMBWA KUSHIRIKI MATENGENEZO YA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Na.Vumilia Abel-Nsimbo JAMII wilayani Nsimbo mkoani katavi imeombwa kushiriki katika matengenezo madogo madogo ya miundombinu ya barabara.

MKOA WA KATAVI KUTOA SEMINA KWA VIONGOZI WA NGAZI ZA MITAA ILI KUTAMBUA MAJUKUMU YAO

Na.Boniface Mpagape:Mpanda SERIKALI Mkoani katavi inatarajia kutoa semina kwa viongozi wa serikali kuanzia ngazi za vijiji, kata na tarafa ili watambue vyema majukumu yao.

WACHIMBAJI DHAHABU ZAIDI YA 200 MPANDA WAPIGWA MARUFUKU UCHIMBAJI,VITENDO VYA WIZI VYAIBUKA

Na.Issack Gerald-Mpanda Wachimbaji   wadogowadogo wa dhahabu katika mgodi wa Kampuni Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamesikitishwa na kitendo cha serikali kuwapiga marufuku uchimbaji wa madini katika mgodi huo kwa madai kuwa eneo hilo ni miliki ya makambi ya jeshi.

WANAFUNZI WANYESHEWA MVUA WAKISOMEA CHINI YA MIEMBE WILAYANI MPANDA,WAZAZI WAISHIWA NGUVU WAIOMBA SERIKALI KUSAIDIA

Image
Na.Issack Gerald-Mpanda Wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika Shule ya Msingi Sambwe iliyopo mtaa wa Kampuni   Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda,wameiomba serikali kuwasaidia kumalizia ujenzi wa madarasa katika shule hiyo ili wanafunzi hao waondokane na adhaa ya kunyeshewa na mvua   inayoambatana na radi wakiwa chini ya miembe.                                                          Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Sambwe wanavyoonekana katika picha katika madarsa yaliyokuwa yakitumika mwezi septemba mwaka jana ambao hata hivyo miti hiyo unayoiona hakuna mti hata mmoja wanasomea chini ya mwembe                                               Moja ya mwembe unaotumiwa na wanafunzi kama darasa ukitumika kama ukumbi wa mikutano ya wazazi Shule ya msingi Sambwe

WAKAZI KATAVI WATAKIWA KUWA MAKINI NA MVUA KUEPUKA MAFURIKO PIA IDARA ZA MAAFA KATIKA HALMSHAURI ZOTE ZAAGIZWA KUJIPANGA KIKAMILIFU

Na.Boniface Mpagape-Mpanda MKUU wa Mkoa wa katavi Dk. Ibrahim Msengi amewataka wakazi wa mkoa huo,kuchukua tahadhari kutokana na uwezekano wa kuwepo kwa mafuriko kama ilivyotabiriwa na wataalam wa hali ya hewa.

AMPA UJAUZITO DADA YAKE WA MIAKA 14 SUMBAWANGA POLISI WAMDAKA,IDARA YA ELIMU NAKO KALAMBO HARAKATI KWA KWENDA MBELE

Na.Issack Gerald-Sumbawanga POLISI wilayani Sumbawanga Mkoani Rukwa inamshikilia mkazi wa kijiji cha Ulinji, Manispaa ya Sumbawanga mwenye umri wa miaka 28 kwa tuhuma za kumpa ujauzito dada yake mwenye umri wa miaka 14 anayesoma darasa la saba.

WANAOGOMBANIA ARDHI NSIMBO WATAKIWA KUTOKA,ELIMU BURE BADO KUELEWEKA IPASAVYO KWA WANANCHI MKUU WA WILAYA YA MLELE ATOA NENO

Na.Agness Mnubi-Nsimbo. WADAU wa Elimu katika halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wametakiwa kuelimisha wazazi na walezi juu ya Mfumo wa elimu bure.

RADI YAUA WAWILI YAJERUHI WATATU KATAVI

Na.Issack Gerald-Katavi Watu wawili waliofahamika kwa majina ya Kupiwa Julius (28) na Lemmy Madirisha wote wakazi wa Mkazi wa Ilebura wamepigwa na radi na kufariki dunia papo hapo.

WATATU KATA YA MPANDA NDOGO WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA WAKITUHUMIWA KUJIPATIA SHILINGI MIL.3,400,000/= KWA NJIA YA UDANGANYIFU

Na.Issack Gerald-Mpanda WATU wawili wakazi wa kata ya Mpanda ndogo wilayani Mpanda mkoani Katavi, jana wamefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda wakikabiliwa na shtaka la kujipatia fedha shilingi milioni tatu na laki nne kwa njia ya udanganyifu.

WAZIRI MKUU AELEZA MIKAKATI YA SERIKALI KUFUNGUA VIWANDA VYA NGOZI DAR, GEITA NA SHINYANGA

Image
Issack Gerald-DAR ES SALAAM WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema,Serikali imepanga kufungua viwanda vya kusindika ngozi kwenye mikoa ya Shinyanga, Geita na Dar es Salaam ili kutoa soko kwa ngozi za wanyama wanaochinjwa kwenye machinjio ya mikoa hiyo.                                              Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watanzania waishio Botswana baada ya kuhudhuria mkutano wa SADC mjini Gaborone Januari 18, 2016. Waziri

AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA KUDHURU MWILI

Na.Boniface Mpagape-Mpanda MTU mmoja mmoja mkazi wa Kasokola wilayani Mpanda Bw. Godfrey Kipyela, jana amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kudhuru mwili.

WAKURUGENZI WAWILI WATUMBULIWA MAJIPU YUMO WA SULEIMANI LUKANGA WA MANISPAA YA MPANDA

Image
Na.Mwandishi wetu-DAR ES SALAAM MKURUGENZI Mtendaji Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Suleiman Lukanga,amesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuridhia na kutekeleza uamuzi ulioisababishia serikali hasara na upotevu wa fedha.                                                         Waziri George Simbachawene

WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA MAKOSA MBALIMBALI LIKIWEMO SHAMBULIO LA MWILI.

Na.Issack Gerald-MPANDA VIJANA watatu wakazi wa Mpanda mjini jana wamefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda, wakikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili.

KATAVI YAPOKEA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 80 ZA KUGHARIMIA ELIMU BURE.

Na.Issack Gerald-Katavi Mkoa wa Katavi umepokea Zaidi ya Shilingi Milioni 80 kwa ajili ya kugharimia mpango wa serikali wa elimu bure kwa wanafunzi kuanzia Chekechea hadi   kidato cha nne.

HALMASHAURI ZA WILAYA KATAVI ZATAKIWA KUTATU CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU YA ELIMU KUFANIKISHA BRN

Na.Issack Gerald-MPANDA HALMASHAURI zote zilizomo ndani ya mkoa wa katavi zimetakiwa kufanya jitihada za kutatua   changamoto za miundombinu ya elimu ili kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma vizuri.

MATUKIO YA WIKI KATAVI NA KWINGINEKO KUANZIA JANUARI 11 – 16,2016 NA P5 TANZANIA MEDIA

ASHIKILIWA NA POLISI KATAVI KWA KUKAMATWA NA MENO   YA TEMBO KILOGRAM 50 YENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.120. Posted By: Issack Gerald | At: Tuesday, January 12, 2016 Na.Issack Gerald-Katavi Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nzuri Ndizu (44) mkazi wa kijiji cha mbede anashikiliwa   na Jeshi la Polisi akiwa na meno 08 ya tembo vyenye uzito wa kg 50 ikiwa na thamani ya Tshs 120,000,000/= ambapo ni sawa na tembo 4 waliouawa kinume cha sheria.

MWANAFUNZI DARASA LA KWANZA MWANZA AFA MAJI AKIWA NA BABAYE,ASKARI WA UOKOAJI WAKOSA MWILI

Na.Albert Kavano-Mwanza MWANAFUNZI wa Darasa la Kwanza   katika shule ya Msingi Mabatini B Jijijni Mwanza Amefariki dunia baada ya kusombwa na maji yaliyotokana na mvua kubwa iliyonyesha jana kwa zaidi ya saa 6,   jijini humo.

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SHAMBULIO LA MME WAKE

Na.Issack Gerald-Mpanda MTU mmoja mkazi wa Kawajense katika Manispaa ya Mpanda, Bi. Judith Mgawe, juzi amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili dhidi ya mmewe.

MANISPAA YA MPANDA WANG’ANGA’NIA HOSPITALI YA WILAYA YA MPANDA IWE YAO,KAKESE YAONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Na.Issack Gerald-Mpanda Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imesema kuwa mchakato wa kuhamisha Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kutoka katika utawala wa Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda kuwekwa katika utawala wa Manispaa unaendelea.

WAZIRI WA KILIMO,MIFUGO NA UVUVI ZIARANI MLELE,ATOA RAI KWA WATUMISHI WA UMMA,AZUNGUMZA NA WAKULIMA WA TUMBAKU

Na.Issack Gerald-Mlele Waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi Mheshimiwa Willium Tate Nashe,amewataka watumishi wa umma Wilayani Mlele Mkoani Katavi kufanya kazi kwa uadilifu,uaminifu sambamba na kuwa karibu na wananchi kwa ajili ya kutatua changamoto zinazowakabili wananchi hao.

BALAZA LA MADIWANI MPANDA LAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI,WAPOKEA TAARIFA NA KUJADILI CHANGAMOTO ZA WANANCHI.

Na.Issack Gerald-MPANDA Balaza la madiwani Manispaa ya Mpanda limetoa kauli ya pamoja kuunga mkono Juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli.

WAZIRI MKUU MAJALIWA ASEMA TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA RWANDA

Na.Issack Gerald WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Rwanda nchini, Eugene Kayihura. Ambapo amemuahidi kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Rwanda.

WAWILI MANISPAA YA MAPANDA WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA WAKITHUMIWA KUIBA NAKUPORA MALI ZENYET THAMANI KARIBU MIL.2.

Na.Boniface Mpagape-MPANDA MKAZI wa Makanyagio katika Manispaa ya Mpanda, Bw. Reuben Remi amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuvunja duka na kuiba nguo zenye thamani ya shilingi milioni moja na laki nne na elfu arobaini.

MABALAZA YA MADIWANI MPANDA KUANZA VIKAO VYAKE LEO

Image
Na.Issack Gerald-Mpanda Balaza la madiwani Manispaa ya Mpanda leo linatarajia kuanza vikao vyake kujadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya wananchi.                                              Moja ya mambo yanayoifanya Mpanda kupewa Manispaa ya Mpanda

BABA NA MAMA WA KAMBO WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA MANYANYASO NA KUMNYIMA CHAKULA MTOTO WAO

Na.Issack Gerald-KATAVI Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ramadhani Charles (40) Mkazi wa Kasimba anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoani Katavi kwa kosa la kumnyanyasa mtoto wake anayeitwa Adam Ramadhani (17) ambaye ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kashaulili sambamba na kumnyima mambo mengine ya msingi kama chakula.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MABALOZI WAWILI NCHI TOFAUTI-P5 TANZANIA MEDIA INAKUJUZA

Na.Issack Gerald WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekuatana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili kutoka nchi za Qatar na Kuwait.

MAFURIKO YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI NSEMULWA MANISPAA YA MPANDA

Na.Issack Gerald-MPANDA Shule ya Msingi Nsemulwa iliyopo kata ya Nsemulwa Manispaa ya Mpanda,mpaka sasa imesajili   Jumla ya wanafunzi   513 wa darasa la kwanza na Chekechea na hatimaye kukabiliwa na changamoto ya upungufu wa madarasa,madawati na matundu ya vyoo.

JAMII MWANZA YATAKIWA KUTAWANYANYAPAA WAATHIRIKA WA DAWA ZA KULEVYA

Na.Issack Gerald-Mwanza. Jamii nchini imetakiwa kutowanyanyapaa waathirika wa dawa kulevya badala yake iwasaidie kuondokana na matumizi ya dawa hizo ikiwemo kuwafikisha katika vituo vya utimamu wa akili (Sobar House).

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMTEMBELEA MAMA MARIA NYERERE AMPA POLE

Na.Issack Gerald WAZIRI MKUU,Kassim Majaliwa amemtembelea na kuampa pole  mke wa Baba wa Taifa,  Mama Maria Maria Nyerere kwa kufiwa na mkwewe  Leticia Nyerere.

AFISA ELIMU WILAYANI NKASI AELEZA MIKAKATI YA KUINUA KIWANGO CHA UFAULU WILYANI HUMO

Na.Issack Gerald-SUMBAWANGA HALMASHAURI   ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imeazimia kuongeza kiwango cha ufaulu     kwa mwaka wa 2016.

JESHI LA POLISI KATAVI LASHAURIWA KUZUIA UHARIFU BADALA YA MATUKIO

Na.Issack Gerald-Katavi Jeshi la polisi mkoani Katavi limeshauriwa kujenga desturi ya kuzuia uharifu kabla haujatokea badala ya kupambana na matukio Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Katavi, Dr. Ibrahim Msengi wakati wa maadhimisho ya siku ya Polisi nchini iliyofanyika Juzi katika viwanja vya Polisi Wilayani Mpanda.

ASHIKILIWA NA POLISI KATAVI KWA KUKAMATWA NA METO YA TEMBO KILOGRAM 50 YENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.120.

Image
Na.Issack Gerald-Katavi Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nzuri Ndizu (44) mkazi wa kijiji cha mbede anashikiliwa   na Jeshi la Polisi akiwa na meno 08 ya tembo vyenye uzito wa kg 50 ikiwa na thamani ya Tshs 120,000,000/= ambapo ni sawa na tembo 4 waliouawa kinume cha sheria. Mtuhumiwa bw.Nzuri Ndizu akiwa Polisi kwa Mahojiano baada ya kukamatwa na meno ya tembo(PICHA na.Issack Gerald)                                                                   Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi akifafanua kuhusu kukamatwa kwa mtuhumiwa wa meno ya tembo                                                                                      Meno ya tembo yaliyokamatwa haktika hatua ya kusubiri kuuzwa

MRAJISI VYAMA VYA MSINGI TANZANIA APEWA SIKU 14 KUUNDA TIMU YA UKAGUZI MALALAMIKO YA WAKULIMA WA TUMBAKU MPANDA

Image
Na.Issack Gerald-Mpanda,Katavi Naibu Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh. William Tate Ole Nasha,amemwagiza Mrajishi wa vyama vya ushirika Tanzania,kuhakikisha anaunda timu ya ukaguzi ndani ya Siku 14 ili kuchunguza malalamiko ya wakulima wa zao la tumbaku katika chama cha msingi cha ushirika cha Mpanda Kati kilichopo Wilayani Mpanda.                                                   Wa-tatu kutoka kushoto aliyeshika kifuani mwake ni Naibu waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi akipata maelezo kutoka kwa viongozi wa Wilaya ya Mpanda Muda mfupi kabla ya kuanza kikao na wakulima Chama cha Msingi Mpanda Katati,aliyevaa kaunda suti ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Pazza Mwamlima na wengine katika picha ni wakuu wa idara Wilayani Mpanda                                             

CUBA YAENDELEA KUSAIDIA TANZANIA KUPAMBANA NA MALARIA

Image
Na.Issack Gerald-Katavi WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini, Bwana Jorge Luis Lopez Tormo ambaye ameahidi kuendelea kusaidia Tanzania katika mapambano dhidi ya malaria.                                                                           Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo,  ofisini kwake jijini Dar es slaam Januari 11, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

HALI YA USALAMA BURUNDI HUENDA IKACHUKUA SURA MPYA

Image
Na. Issack Gerald-Katavi Hali ya kisiasa nchini Burundi huenda ikachukua sura mpya baada ya serikali na upinzani kutoafikiana juu ya yatakayozungumzwa kwenye mkutano ili kutatua mzozo nchini humo.                                                      Jaji Augustine Mahiga Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimatifa akiwa ni miongoni mwa viongozi wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki wanaoshuruhisha mgogoro wa kisiasa nchini Burundi

SERIKALI YATOA MILIONI 999,376,000/= KUGHARIMIA ELIMU BURE MKOANI MWANZA

Na.Issack Gerald-Mwanza. Serikali   ya awamu   ya Tano chini ya Raisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Josefu Magufuri Imetoa kiasi cha shilingi milioni 999,376,000 kwa ajiri ya kughalimia elimu kwa shule za msingi na Sekondari   kwa mwezi januari.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AAGANA NA BALOZI WA NAMIBIA,AKUTANA NA BALOZI WA FINLAND NCHINI.

Image
Na.Issack Gerald-Katavi WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekuatana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Namibia ambaye anamaliza muda wake, Bwana Japhet Isaack.                                                                            Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na balozi Namibia nchini, Mhe. Japhet Isaack ambaye alikwenda Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Januari 8, 2016

MATUKIO YA WIKI KUANZIA JUMATATU JANUARI 04— IJUMAA JANUARI 09,2015 MKOANI KATAVI NA TANZANIA KWA UJUMLA

NA.ISSACK GERALD BATHROMEO WAWILI MPANDA WAUAWA,WAUAJI WATOKOMEA KUSIKOJULIKANA NAO POLISI WASEMA HAPA KAZI TU Posted By: Issack Gerald | At: Monday, January 04, 2016 Na.Issack Gerald-MPANDA Watu wawili wamekutwa wakiwa wameuawa na watu wasiojulikana Wilayani Mpanda Mkoani Katavi baada ya kukatwa na vitu vyenye ncha kali Januari Mosi Mwaka huu.

TUME YA ARDHI MPANDA YATOA TAARIFA YA UCHUNGUZI MIGOGORO YA ARDHI KWA BAADHI YA VIJIJI

Na.Issack Gerald-Mpanda TUME ya uchunguzi wa migogoro ya ardhi imetoa taarifa baada ya kufanya uchunguzi katika vijiji vya Ikaka, Nkungu na Kapalamsenga wilayani Mpanda.

ASKARI 15 KATAVI WATUNUKIWA VYETI VYA HESHIMA POLICE FAMILY DAY,WAPANGA MIKAKATI YA KUKOMESHA UHARIFU

Na.Lutakilwa-Lutobeka-Katavi MAAFISA 15 wa jeshi la polisi mkoani Katavi wametunukiwa vyeti maalum vya utendaji kazi katika maadhimisho ya siku ya polisi yaliyofanyika leo mjini Mpanda.

AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA UHARIBIFU WA MALI NA KUTELEKEZA FAMILIA.

Na.Issack Gerald-MPANDA Mtu mmoja mkazi wa mtaa wa Kasimba manispaa ya Mpanda jana amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuharibu mali na kutelekeza familia.

BREAKING NEWS: DAR ES SALAAM JENGO LA WIZARA YA MAMBO YA NDANI MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI TANZANIA LANUSURIKA KUTEKETEA KWA MOTO

Image
Na.Issack Gerald-Dar es Salaam Jengo la Wizara ya mambo ya ndani makao makuu ya jeshi la Polisi,limenusulika kuteketea kwa moto na kusababisha kazi za jeshi hilo kusimama kwa muda,kutokana na wafanyakazi na viongozi wa jeshi hilo kutoka nje ya jengo kufuatia ya tahadhari ya moto kutolewa.                                                Msemaji wa jeshi la Polisi Tanzania Advera Bulimba

WAZIRI MKUU ASEMA SERIKALI HAIJARIDHIA VIWANGO VIPYA VYA NAULI YA MABASI YAENDAYO KASI

Image
Na.Issack Gerald-Dar es Salaam Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali haijaridhia viwango vipya vya nauli ya mabasi yaendayo kasi vilivyopendekezwa na waendeshaji wa huduma ya mabasi yaendayo kasi Dar es salaam (UDART).                                                                                                                                                      

UELEWA MDOGO WA WATU WAISHIO NA VIRUSI VYA UKIMWI,BADO CHANGAMOTO KUUDHIBITI UGONJWA WA UKIMWI

Na.Issack Gerald-Mwanza Muuguzi wa Kituo kinacho toa huduma kwa watu wanaoishi na maambukizi ya Virus Vya UKIMWI na Yatima Shalom Care House Jijini Mwanza   Bi Edna Evarist amesema uelewa mdogo   wa watu wanaoishi Na VVU ni changamoto katika kudhibiti UKIMWI nchini.

WAWILI AKIWEMO ASKARI WA JESHI LA POLISI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MWANZA KWA TUHUMA ZA MAUAJI

Image
Na.Issack Gerald-Mwanza Watu wawili   akiwemo askari wa Jeshi la Polisi wanashikliwa   na jehi la polisi kwa makosa ya mauaji katika maeneo tofauti Mkoani Mwanza.                                                          Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza Justus Kamgisha

WATATU WAUAWA WILYANI MLELE KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI,LIMO LA BABA NA MWANAWE KULIWA NYAMA NA SIMBA

Image
Na.Issack Gerald-Mlele Katavi Watu watatu wamekufa katika matukio mawili tofauti Wilayani Mlele Mkoani Katavi likiwemo tukio la baba na mwanae kuliwa na samba jike mzee.                                           Baadhi ya Simba katika Hifadhi ya taifa ya wanayama ya Katavi

VIONGOZI WA CHAMA CHA USHIRIKA CHA SONAMCU MKOANI RUVUMA WASIMAMISHWA KAZI NA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

Image
Na.Issack Gerald-Ruvuma Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha kusindika  tumbaku  cha mkoani Ruvuma na kuwasimamisha kazi viongozi wa Chama Cha Kikuu Cha Ushirika cha SONAMCU.                                                                          Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa (Picha kwa hisani ya Ofisi ya Waziri Mkuu)                                                                                Moja ya mashamba ya tumbaku Mkoani Ruvuma

MKURUGENZI WA MIPANGO WA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA (TFS) NA MAOFISA MISITU WA MIKOA YOTE NCHINI WASIMAMISHWA KAZI

Image
Na.Issack Gerald Waziri wa Maliasili na Utalii Prof.Jumanne Maghembe amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi Endelevu ya Rasilimali za Misitu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Bw.Mohammed Kilongo na Maofisa wa Misitu wa Mikoa nchi nzima kupisha uchunguzi wa upotevu wa mapato ya Serikali.                                                                               Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza katika kikao na Idara ya Misitu na Nyuki pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika ukumbi wa Ngorongoro Makao Makuu wa Wizara hiyo Mpingo House Jijini Dar es Salaam jana  05 Januari, 2016.

BREAKING NEWS : WALIMU 120 MIKOA YA RUKWA,KATAVI NA KIGOMA WAPATIWA MAFUNZO KUINU KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI

Na.Issack Gerald- MPANDA JUMLA ya Walimu   120 wa Shule za msingi kutoka halmashauri 8 za   Mikoa ya Rukwa, Kigoma na Katavi wanashiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu na wanafunzi katika ufundishaji na ujifunzaji ili kuboresha taaluma na kuongeza kiwango cha   Ufaulu kitaifa.

KAMANDA WA POLISI RUKWA AZUNGUMZIA HALI YA USALAMA SIKUKUU ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA,ASEMA MATUKIO MAKUU MAWILI YALITIKISA MWAKA 2015

Image
Na.Issack Gerald-SUMBAWANGA Jeshi la Polisi Mkoani Rukwa limesema kuwa,hakuna matukio matukio ya uharifu yaliyotokea katika kipindi chote cha msimu wa sikukuu za kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha mwaka 2016.                                                          Ramani inayoonesha mahali Mkoa wa Rukwa unapopatikana pia maeneo yanayopakana na mkoa huo yanaonekana

VIONGOZI MKOANI GEITA WATAKIWA KUTOWAONEA AIBU WAFANYABIASHARA WASIOFUATA KANUNI ZA USAFI ILI KUPAMBANA NA KIPINDUPINDU

Na.Issack Gerald-Geita Viongozi wa Mkoa wa Geita wametakiwa wasiwaonee aibu kuwafungia wafanyabiashara wasiofuata kanuni za usafi wa mazingira na hivyo kupelekea mlipuko wa kipindupindu.

SIKU YA PILI ZIARA YA WAZIRI MKUU, AKAGUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Image
Na.Issack Gerald-Ruvuma Chanzo cha habari :Ofisi ya mawasiliano ya Waziri Mkuu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekagua jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wialaya ya Songea lilipo katika kijiji cha Lundusi, Wilaya ya Peramiho mkoani Ruvuma.                                                                        Makao makuu ya Halmashauri aya Wilaya ya Songea

JELA SIKU 14,KWA KUMCHANACHANA KWA NYEMBE MTOTO WAKE WA MIAKA 6

Na.Issack Gerald-MPANDA Mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda imemhukumu Bi. Agnes George (30) mkazi wa Kawajense mjini Mpanda kwenda jela kwa siku kumi na nne,   baada ya kupatikana na hatia ya kumkatakata kwa nyembe nyuma ya viganja mtoto wake mwenye umri wa miaka sita, akimtuhumu kuiba fedha.

MLELE NAKO MAUJI KAMA MPANDA,MMOJA AUAWA,WAUAJI WATOKOMEA POLISI MSHIKEMSHIKE KUWASAKA WAUAJI

Na.Issack Mlele-Katavi Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Chalya Kichosha(60) mkazi wa mkazi wa kijiji cha Ibindi alikutwa akiwa ameuawa na watu wasiojulikana kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kichwani na shingoni .