Posts

Showing posts from April 23, 2018

MANISPAA YA MPANDA YATANGAZA KUUWA MIFUGO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Bw.Michael Francis Nzyungu ametangaza kuwa kuanzia Aprili 25 mwaka 2018 itakuwa ni oparesheni ya kuuwa mifugo inayozurura ovyo mitaani hususani Mbwa. Katika taarifa yake mahususi kwa ajili ya Oparesheni hiyo itakayofanyika eneo lote la manispaa ya Mpanda,amewataka   wafugaji wote katika Manispaa hiyo kufungia mifugo yote ikiwemo Ng’ombe, mbuzi, Kondoo, nguruwe na mbwa. Katika Manispaa ya Mpanda imekuwa hali ya kawaida mifugo kuzurura ambapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamika kuharibikiwa na mazao au mali za nyumbani. Tangazo la Mkurugenzi linakuwa na aina yake kwa kuwa mara nyingi imezoeleka maonyo ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakitolewa na Maafisa watendaji wa mitaa,kata na mitaa bila mafanikio ambapo zaidi wamekuwa wakipigwa faini wenye mifugo.   Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  

RADI YAUA MWANAFUNZI RUKWA

MWANAFUNZI wa darasa la pili shule ya msingi Kipundu James Kandege (8) amefariki dunia baada ya kupigwa radi juzi jioni akiwa nyumbani kwao na wenzake. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na afisa mtendaji wa kijiji cha Mabatini kata ya Namanyere Ibrahimu Adriano alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi jioni majira ya saa 10 alipokuwa ameketi nyumbani na wenzie walipokuwa wakila chakula cha mchana. Alisema kuwa marehemu akiwa na wenzie sambamba na waza zi wake wakila chakula katika kitongoji cha Katowa kijiji cha Mabatini walipigwa na radi wakiwa ndani ya nyumba yao na mwanafunzi huyo alifariki dunia papo hapo huku wengine wakisalimika. Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kipundu Josephat Laban athibitisha kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo ambapo alisema kuwa shule hiyo iliwaruhusu Wanafunzi wote walishiriki katika msiba huo sambamba na mazishi huku akidai kuwa shule imempoteza mtu muhimu. Diwani wa kata ya Namanyere Evarist Mwanisawa alisema kuwa Mwanafunzi huyo alikua ni mka

AACHIWA MKE KWA LAKI 8 BAADA YA KUFUMANIWA

MKAZIwa kijiji cha Ntumba kilichpo wilayani Tanganyika katika mkoa wa Katavi,Charles Sabuni (37)  amepwa  viboko 30 hadharani baada ya kushikwa ugoni na mke wa jirani yake Ntema Mwiwela,juzi usiku wa manane kijijini hapo. Kwa mujibu wa Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa adhabu hiyo  alipewa mgoni huyo ili iwefundisho kwake na  kwa wanaume wengine wenye tabia kama hiyo. Akisimulia tukio hilo mwenyekiti wa Kitongoji cha Ntumba Samwel Mbuya alisema lilitokea saa tisa usiku, juzi nyumbani kwa Mwiwela ambaye anaishi jirani na Sabuni. Akifafanua alisema kuwa mchana wa siku hiyo ya tukio hilo Mwiwela alimuaga mkewe kuwa ana safiri ambapo alirejea nyumbani kwake ghfla usiku wa manane na kumkuta Sabuni akiwa amelala chumbani kwake. “Mwenye mke alimthibiti mgoni wake huyo asitoroke huku akimwamuru apige mayowe huku akisema anaomba msaada kwani amefumaniwa na mke wa mtu ….. kele hizo ziliwaamsha wanakijiji wenzake ambao walikimbilia eneo la tukio na  walipigwa na kutwaa kumkut

RAIS MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI BODI YA WAKURUGENZI BENKI YA POSTA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt.Edmund Bernard Mndolwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Posta Tanzania ( TPB ). Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,Ikulu Gerson Msigwa,Uteuzi wa Dkt.Mndolwa umeanza tarehe 23 Aprili, 2018. Dkt.Mndolwa anachukua nafasi ya Prof.Lettice Rutashobya ambaye amemaliza muda wake. Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com