Posts

Showing posts from August 7, 2015

UNAMFAHAMU MAGUFULI NA MAISHA YAKE TANGU KUZALIWA HADI SIASA?ONGEZA CHAKULACHA UBONGO NA P5 TANZANIA

Image
Mhandisi John Pombe Magufuli JOHN POMBE MAGUFULI Magufuli ni Nani? Lakini je Daktari John Magufuli ni Nani? Mgombea wa urais wa chama cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2015 Daktari John Pombe Joseph Magufuli ni mbunge wa jimbo la Chato lililoko mkoa wa Geita na ni waziri wa ujenzi wa Tanzania. Alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 wilayani Chato Mkoani Kagera. Kielimu, daktari Magufuli ana Stashahada ya elimu ya sayansi akibobea kwenye masomo ya Kemia, Hisabati. Mgombea huyo wa urais ana shahada ya umahiri wa Sayansi na shahada ya uzamivu ya kemia. Aidha daktari Magufuli amewahi kufundisha katika shule ya sekondari Sengerema miaka ya themanini kisha akajiunga na mafunzo ya JKT . Alizaliwa Oktoba 1959 Mhandisi John Pombe Magufuli wakati akijiunga na ccm 1995  Alipohitimu, daktari Magufuli na aliaanza kufanya kazi katika kiwanda cha ‘Nyanza Cooperative Union akiwa Mkemia kabla ya kuondoka hapo na kuwania ubunge. Magufuli alianza mbio za ubunge mwaka 1995

WAKAZI MPANDA WANDELEA KUWA GIZANI UMEME KUKATIKA,VIWANDA VYAKOSA UMEME SHUGHULI ZASIMAMA KWA MWEZI SASA

NA.Issack Gerald TATIZO la kukatika Umeme mara kwa mara Mkoani Katavi   limesababisha kuzorota kwa biashara ya mchele, kutokana na kukwama kwa ukoboaji wa mpunga zao linalotegemewa na wakazi wengi   mkoani Katavi.

MGOGORO WA ARDHI MTAA WA NSEMULWA BADO MBICHI,MKURUGENZI ATOA JIBU BILA SULUHU

NA.Issack Gerald-Katavi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imesema haijapokea malalamiko ya wakazi wa mtaa wa Nsemulwa kutopimiwa viwanja vyao na kutozwa kiwango kikubwa cha pesa tofauti na kilichopangwa kupitia mikutano.