Posts

Showing posts from January 25, 2018

MWANAFUNZI AUAWAWA KIKATIRI POLISI KATAVI WAMSAKA MUUWAJI

Image
Na.Issack Gerald-Katavi JESHI la polisi mkoani Katavi linamsaka mtu asijejulikana kwa tuhuma za kumbaka,kumchoma kisu,kumuua na kisha kukata sehemu za siri za mwanafunzi(14) wa  darasa la sita shule ya msingi  Vikonge wilaya ya  Tanganyika na kukimbilia kusiko julikana. Akitoa taarifa ya tukio hilo kamanda wa polisi Damas Nyanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 1;30 za asubuhi wakati marehemu akiwa anakwenda shule akiwa ameongozana na mdogo wake ambaye wanasoma shule moja. Alisema kuwa siku ya  tukio hilo marehemu  alitoka  nyumbani akiwa na mdogo wake wa kiume  mwenye  umri wa miaka 11  mwanafunzi wa   darasa  la  nne  ambaye waliongozana wakielekea  shule ya  msingi  vikonge ambayo wanasoma. Kamanda Nyanda alisema wakiwa  njiani  alitokea  mwendesha  pikipiki maarufu kwa jina bodaboda  ambae walikuwa  hawamfahamu  na  kusimamisha  pikipiki yake  na  kuwaambia anataka  awape  lifti ili wafike haraka shuleni  kwao. Alisema  baada ya  kuambiwa  hivyo  wana

BARAZA LA MADIWANI MPANDA LAONYA WATUMISHI WANAOSABABISHA MIGOGORO YA ARDHI

Image
Na.Issack Gerald Baraza la Madiwani Halamshauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,limesema litachukua hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafukuza kazi watumishi wa idara ya ardhi watakaosababisha migogoro ya ardhi baina ya wananchi. Mstahiki Meya wa Manispaa Mpanda Mh.Willium Mbogo Tamko hilo ambalo limtolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mh.Willium Mbogo kupitia kikao maalumu cha bajeti cha baraza hilo ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa hiyo. Amesema kumeanza kujitokeza migogoro ya ardhi kuhusiana na kiwanja kimoja kuuzwa kwa watu wawili tofauti suala ambalo limetajwa kufanywa na watumishi wa idara ya ardhi wasio waaminifu na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mh.Willium Mbogo amelazimika kuagiza migogoro hiyo isuluhishwe wao kwa wao kabla ya tatizo kuwa na baraza kupewa taarifa. Aidha amesema hatua za kisheria zitachukuliwa pia kwa watumishi wa idara mbalimbali ambao wamesababisha Manispaa ya Mpanda Kukosa mapato kutokana na uzembe wao katika uwajibikaji