Posts

Showing posts from March 26, 2018

MKUU WA SHULE AJINYONGA OFISINI KWAKE AKIMTAJA MKURUGENZI

Image
MKUU wa Shule ya Sekondari Kakonko wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Peter Rubonya amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kamba ofisini kwake mapema leo asubuhi. Akielezea tukio hilo,Mwalim wa zamu wa shule hiyo Isaac Japhet amesema yeye alifika shuleni hapo saa 12:30 asubuhi ili kuwafundisha wanafunzi wa kidato cha nne masomo ya ziada baada ya kufunga shule wiki iliyopita na baada ya kufika aligundua kuwa hana chaki ambapo mkuu huyo wa shule alimpatia chaki mlinzi ili awape wananfunzi. Amesema baada ya muda,Mratibu elimu kata pamoja na mmoja wa wazazi walifika ofisini hapo wakiwa na shida na mkuu wa shule na baada ya kuelezwa yupo ndani ofisini lakini baada ya kugonga mlango hawakuweza kujibiwa na ndipo wakaamua kufungua mlango na kukuta mwili wa marehemu ukining’inia dalini. Mwalim Isaac amesema Mwalimu aliyejinyonga alikuwa akifundisha masomo ya Kemia na Fizikia shuleni hapo hawakuwahi kusikia mgogoro wowote wa kifamilia au kijamii na mkewe ambaye ni mkufunzi katika Chuo Kiku

UYOGA WAUA MWINGINE KATAVI

Image
Mtu mwingine mkazi wa kijiji cha Sitalike wilayani Mpanda Mkoani Katavi amefariki dunia akiwa hospitali ya Manispaa ya Mpanda akipatiwa matibabu na hivyo kufikisha idadi ya watu watatu waliofariki kutokana na kula uyoga unaosadikiwa kuwa na sumu. Mwenyekiti wa kijiji cha Sitalike Bw.Christopher   Anjero amemtaja mwanamke aliyefariki leo kuwa ni Mariana Gerald Sanane ambaye ni Mama wa marehemu wawili waliofariki siku ya jana. Waliofariki jana kutokana na kula uyoga huo ni Frenki Mayaga   ambaye alifariki akipatiwa huduma ya kwanza katika kijiji cha Stalike huku   Erizabeth George ambaye alikimbizwa hospitali ya Manispaa ya Mpanda akiaga dunia baada ya kufikishwa katika mlango wa Daktari. Mganga wa zamu wa hospitali ya Manispaa ya Mpanda ambaye alitakiwa kueleza zaidi kuhusu suala hilo amekana kuzungumza kwa madai ya kutokuwa msemaji kwa sasa. Kisa hicho   ambacho kimeacha simanzi kwa jamii kutokana na vifo vya watu watatu wa familia moja kinatajwa kuwa ni kuwa cha kwanza kati

RAIS MAGUFULI APOKEA NA KUZINDUA MAGARI 181 YA MSD,MIKOA MIPYA YATAJWA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.John Magufuli amesema serikali inaendelea kupanga   mikakati yake kuhakikisha inakarabati na kujenga vituo na Hospitali zinazotoa huduma za afya nchini ikiwemo mikoa mipya ya Katavi,Songwe,Geita,Simiyu na Njombe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo katika hafla fupi ya ugawaji wa magari 181 ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya kusambaza dawa maeneo mbalimbali nchini,uzinduzi ambao umefanyika eneo la Keko jijini Dar es Salaam. Aidha Rais Magufuli mbali na kuwashukuru Global Fund kwa msaada wa magari 181 yasiyokuwa na   masharti amesema yatarahisisha huduma mbalimbali katika maeneo ya Tanzania katika sekta ya afya. Awali Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya dawa Nchini MSD Laurean Rugambwa Bwanakunu,amesema magari ya bohari ya dawa MSD sasa yatakuwa 213 kutoka magari 32 yaliyokuwepo ambapo magari hayo ya Land Cruiser 104,Malori 77 ambayo kwa ujumla yamegarimu shilingi Bilioni 20.75. Kwa upande wake Leindan Moris mwakailishi wa Global Fund