UYOGA WAUA MWINGINE KATAVI


Mtu mwingine mkazi wa kijiji cha Sitalike wilayani Mpanda Mkoani Katavi amefariki dunia akiwa hospitali ya Manispaa ya Mpanda akipatiwa matibabu na hivyo kufikisha idadi ya watu watatu waliofariki kutokana na kula uyoga unaosadikiwa kuwa na sumu.
Mwenyekiti wa kijiji cha Sitalike Bw.Christopher  Anjero amemtaja mwanamke aliyefariki leo kuwa ni Mariana Gerald Sanane ambaye ni Mama wa marehemu wawili waliofariki siku ya jana.
Waliofariki jana kutokana na kula uyoga huo ni Frenki Mayaga  ambaye alifariki akipatiwa huduma ya kwanza katika kijiji cha Stalike huku  Erizabeth George ambaye alikimbizwa hospitali ya Manispaa ya Mpanda akiaga dunia baada ya kufikishwa katika mlango wa Daktari.
Mganga wa zamu wa hospitali ya Manispaa ya Mpanda ambaye alitakiwa kueleza zaidi kuhusu suala hilo amekana kuzungumza kwa madai ya kutokuwa msemaji kwa sasa.
Kisa hicho  ambacho kimeacha simanzi kwa jamii kutokana na vifo vya watu watatu wa familia moja kinatajwa kuwa ni kuwa cha kwanza katika kipindi cha zaidi ya miaka 10 iliyopita.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA