Posts

Showing posts from November 15, 2017

MKAZI MMOJA NSIMBO KATAVI AMEJINYONGA KWA KUTUMIA MKANDA WA SURUALI IKIELEZWA ANAKIMBIA MADENI

Image
Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi Aliyekuwa Afisa Mtendaji katika kata ya Litapunga halmashauri ya Wilaya ya nsimbo mkoani Katavi Augastino Wangabo(52) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kile kilichoelezwa kuwa amekimbia madeni. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Smith Pangani amethibitisha mtumishi wake kujinyonga akisema tukio hilo limetokea jana. Amesema   Marehemu Wangabo inasemekana alikuwa na madeni mengi pamoja na kutuhumiwa kula michango mbalimbali ikiwemo fedha ya maandalizi ya kuupokea mwenge wa uhuru miaka ya hivi karibuni hali iliyopelekea kuondolewa katika kituo cha awali cha kazi alichokuwa amepangiwa na kurejeshwa Ofisini makao Makuu ya Halmashauri. Kwa upande wake kamanda wa polisi Mkoani Katavi ACP Damasi Nyanda amethibitisha marehemu kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali ambapo amesema uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha marehemu kujinyonga. Kamanda Nyanda amesema mara baada ya marehemu kufuatwa nyumbani kwake kwa ajili ya

HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA KUNUNUA GARI LA KUZOA TAKA,WAMESUBIRI KUBALI CHA WAZIRI MKUU

Image
Na.Issack Gerald Mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani katavi Michael Nzungu amesema wamedhamiria kununua gari kwa ajili ya uzoaji taka wanachosubiri ni kibali kutoka kwa ofisi ya waziri mkuu. Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu Amesema kwa sasa wanakodi gari ambalo bado halikidhi mahitaji ya mkoa hivyo wameanza kujihada za kununua gari ambalo mwaka huu litakuwa limeanza kazi. Aidha amewataka wanan chi kuwa wavumilivu katika kipindi kifupi kilichobaki ili watatue kero ya kuzagaa kwa taka kwani gari dogo la manispaa linalotumika kwa sasa halitoshi kubeba taka zote . Wananchi katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Mpanda wakiwemo waliopo katika kata za Mpanda Hoteli na Makanyagio wamekuwa wakilalamikia gari kutokuzoa taka hali inayosababisha mrundiano wa taka katika makazi ya watu na watu kuhofia kukumbwa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu hasa msimu wa masika. Hata Mkurugenzi Michael Nzyungu amewataka wananchi kutoa taarifa kwa maml

MBUNGE MPANDA VIJIJINI:-SERIKALI INA MPANGO GANI WA KUJENGA HOSPITALI ZA WILAYA KATIKA WILAYA MPYA?

Image
Na.Issack Gerald WIZARA ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) hapa nchini,imeziagiza Halmashauri zote nchini ambazo hazina Hospitali za wilaya kutenga maeneo na kuanza kujenga kulingana na uwezo walionao wakati serikali kuu ikiendelea na Mkakati wa kuoneza nguvu katika ujenzi wa Hosiptali hizo. Agizo hilo limetolewa leo bungeni Dodoma na Naibu waziri  wa Wizara hiyo Joseph Sinkamba Kandege wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpanda vijijini Mh.Suleiman Moshi Kakoso aliyetaka kujua mpango wa serikali katika ujenzi wa Hosiptali katika wilaya hususani Mpaya ambazo hazina hosiptali hizo. Waziri Kandege amesema,serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 imeongeza bajeti na kufikia Zaidi ya Shilingi Bilioni 200 kutoka zaidi ya shilingi bilioni 30 kwa mwaka wa fedha uliopita. Mh.Kakoso katika swali lake la nyongeza,amebainisha kuwa kukosekana kwa Hospitali za Wilaya kwa baadhi ya wilaya hapa nchini ikiwemo Wilaya ya Tanganyika iliyopo Mkoani Katavi k

MTOTO WA KAMANDA MTAAFU SULEIMAN KOVA AMEHUKUMIWA JELA MWAKA MMOJA MKOANI KATAVI KWA UTAPELI,ALIJITAMBULISHA NI MWAKILISHI WA STAR TV MKOANI KATAVI

Image
MAHAKAMA ya mwanzo wilayani Mpanda mkoani Katavi imemuhukumu aliyekuwa akijitambulisha kuwa ni mwakilishi wa  televisheni ya Star Tv mkoani Katavi pia  mtoto wa  Kamanda mstaafu wa Jeshi la polisi  Sulemani Kova anaejulikana kwa  jina la  Gerald  Kova mkazi wa mkoa wa  Mwanza kifungo cha mwaka   mmoja  jela kwa kosa la uapateli. Hukumu hiyo ilitolewa na hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo Marko  Pagyo  baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na  upande wa  mashtaka. Awali mwendesha mashtaka wa jeshi  la  Polisi Wp Salma alidai Mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo februari  8 mwaka huu katika   eneo la hotel ya Madina katika Manispaa ya Mpanda. Alidai  kuwa  mshitakiwa  huyo alijipatia kwa  njia ya udanganyifu  Kamera  moja  aina  ya  Canoni yenye thamani ya shilingi 3,500,000 pia computer aina ya  Laptop pamoja na stendi ya Kamera ya video  mali ya Elias Mlugala. Alisema mtuhumiwa  baada ya  kujipatia  mali  hizo kwa  njia ya   udanganyifu alitoroka wilayani Mpand

MAMBO YAMECHACHA NCHINI ZIMBABWE,JESHI LADHIBITI KITUO CHA UTANGAZAJI CHA TAIFA

Image
Mkuu wa jeshi la Zimbabwe Constantino Chiwenga alitahadharisha uwezekano wa jeshi kuchukua nchi Jeshi nchini Zimbabwe limekidhibiti kituo cha utangazaji cha shirika la habari la taifa hilo ZBC ambapo Sauti za milipuko mikubwa zimesikika mji mkuu wa Zimbabwe Harare. Wanajeshi wakiwa na silaha nzito wameoneakana wakirandaranda mjini Harare Rais Robert Mgabe akiwa na mkewe Bi.Grace Mugabe  Hali hiyo ya wasi wasi wa lolote imetanda nchini humo kuweza kuweza kutokea ambapo wasiwasi huo ulianza jana jioni ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa pamoja na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe ZBC. Hata hivyo taarifa zinasema wafanyakazi wa shirika la utangazaji ZBC,wameambiwa na wanajeshi hao wasiwe na wasiwasi kwamba uwepo wa vikosi hivyo ni kwa lengo la kulinda eneo hilo. Milipuko mizito imeendelea kusikika pia huku Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yakionekana maeneo ya mjini Harare. Chama tawala nchini Zi

MASHA AMEJIVUA UANACHAMA CHADEMA

Image
Aliyekuwa mwanachama CCM, ambaye baadaye alihamia Chadema,Lawrance Masha amejivua uanachama katika chama hicho akidai  upinzani wa sasa umeridhika na hali ya kuendelea  kuwa wakosoaji ili kukisaidia chama tawala kujirekebisha. Masha ameeleza hayo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana Jumanne Novemba 14. Masha ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, katika Serikali ya awamu nne, amesema upinzani hauwezi kutegemea kushika dola kwa kutegemea madhaifu ya CCM badala uwezo wake kama mbadala. Amesema  kazi kubwa ya chama chochote cha siasa ni kujiandaa na hatimaye kushinda uchaguzi ili uweze kuunda na kuendesha Serikali na dola kama njia ya maono yaliyo kwenye ilani ya uchaguzi kwa lengo la kuleta maendeleo na ustawi katika nchi. Masha ambaye aliwani kuwa Mbunge wa Nyamagama mwaka 2005-10,amesema siyo sahihi kwa vyama vya upinzani kuwekeza katika kumpinga Rais Magufuli ambaye ni mkuu wa nchi pekee anayetekeleza kwa vitendo mambo ambayo upinzani iliku