Posts

Showing posts from August 19, 2017

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA FUNGUZI WA MKUTANO WA 37 WA SADC MJINI PRETORIA-Agosti 19,2017

Image
Viongozi wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa  mkutano wa  37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika mjini Pretoria, Afrika ya Kusini .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan leo amehudhuria  ufunguzi rasmi wa Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika – SADC mjini Pretoria Afrika Kusini akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli.

SERIKALI YA TANZANIA YASEMA UJIO WA NDEGE MPYA UKO PALEPALE-Agosti 19,2017

Image
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bibi. Zamaradi Kawawa  Serikali imethibitisha na kuwahakikishia Watanzania kuwa ujio wa ndege mpya ya tatu aina ya Bombardier Q400-Dash 8 upo pale pale licha ya baadhi ya wanasiasa wasio wazalendo kutumia kila njia kukwamisha ujio huo.

WANAFUNZI 22 WA SHULE YA SEKONDARI MIRAMBO MKOANI TABORA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUFANYA VURUGU-Agosti 19,2017

Image
JUMLA ya wanafunzi 22 wa shule ya sekondari Mirambo Mkoani Tabora,wamefikishwa na kusomewa mashtaka 12 yanayowakabili ikiwemo kufanya vurugu katika kata ya Chemchemi.