Posts

Showing posts from March 14, 2018

RUKWA BADO WALIA NA UHABA WA VYUMBA VYA MADARASA

Image
MKOA wa Rukwa bado unakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa ambapo jumla ya vyumba 4,226 vinakitajika ili  kumaliza tatizo hilo. Afisa elimu mkoa huo Nestory Mroka alisema mahitaji hayo yamekuwa yakisababisha mkoa huo kutopiga hatua katika mafanikio ya elimu. Alisema ili wanafunzi wafanye vizuri katika masomo yao ni lazima kuwe na miundombinu mizuri,walimu wa kutosha,vitabu pamoja na walimu lakini kama kuna mapungufu kati ya hayo mambo hata ufaulu hauwezi kuwa mzuri. Aidha Mroka alisema kutokana na changamoto hizo jitihada za makusudi zinahitajika katika kulimaliza tatizo hilo pamoja na mengine ili kuinua ufaulu wa wanufunzi katika shule za msingi pamoja na sekondari ambapo mpaka sasa ufaulu katika kidato cha nne ni wastani wa daraja la nne. Wakati huo huo,Afisa elimu huyo alisema yeye binafsi amejitahidi kuhakikisha anawasimamia walimu ili watimize wajibu wao ipasavyo ikiwamo kuwepo kazini kwa muda mwafaka sambamba na kufundisha kwa juhudi zote ili idara ya eli

AUWAWA KWA SABABU YA MASHAMBA YAKE MJUKUU WAKE AHUSISHWA

Image
JESHI la Polisi mkoani  Rukwa,linawashikilia watu sita akiwemo mjukuu aliyekubalichukua hongo Shilingi milioni moja na kukubali babu yake auawe kwa kupigwa rungu kichwani kutokana na ugomvi wa ardhi. Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa,George Kyando alisema jana kuwa tukio la kuuawa kwa mzee huyo aliyefahamika kwa jina la Paul Kisiwa (72) mkazi wa kijiji cha Ng'ongo lilitokea machi 3 nyakati za jioni kwenye kijiji cha Kifinga Kata ya Mtowisa wilaya Sumbawanga. Taarifa kutoka eneo la tukio zilizothibitishwa na Diwani wa Kata ya Mtowisa, Edger Malinyi, zilieleza kuwa baada ya kuuawa kwa mzee huyo ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CCM ngazi ya kata alizikwa kinyemela shambani kwake. Inaelezwa kuwa taarifa za kupotea mzee huyo zilianza kuzagaa ndipo ndugu wa marehemu pamoja na majirani  wakishirikiana na polisi walianza kuchunguza tukio hilo ambapo ilipofika machi 8 mwaka huu,watu hao walimbana mjukuu wa mzee huyo aitwaye John Kisiwa (22) ambaye alikiri kushiriki kupanga njama za kumuua b

RAIS MAGUFULI AWAONYA TRA

Image
Rais Dkt.John Magufuli amemuagiza Kamishna wa TRA,Waziri wa Fedha na katibu mkuu kwenda kuishughulikia Shirika la Mapato Tanzania (TRA) ili iweze kuacha tabia zake chafu za kuwaongezea raia kodi za mapato pindi wanapokwenda kupata huduma hizo. Dkt.Magufuli ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anatoa hotuba yake kabla ya kuweka jiwe la msingi wa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa ya 'Standard Gauge' katika eneo la Ihumwa,Dodoma ambapo awamu ya kwanza ilizinduliwa mwezi Aprili mwaka 2017,katika maeneo ya PUGU, Jijini Dar es Salaam. Pamoja na hayo,Dkt. Magufuli ameendelea kwa kusema "TRA muangalie kodi zenu mnazozitoza, inawezekana nyingine ni kubwa mno kuliko miradi wanayotekeleza wananchi badala ya kuwa motisha kwa walipa kodi inakuwa kero kwao na badala yake wanabuni njia ya kukwepa kulipa kodi. Kwa upande mwingine,Dkt. Magufuli ameitaka TRA kuendelea kutoa elimu ya mlipa mkodi kwa wananchi ili kuweza kuwapa uelewa wanachi na waweze kulipa kodi kwa heshima kwa taifa

WAENDESHA PIKIPIKI WADAI KUPIGWA FIMBO NA ASKARI

Image
Baadhi ya waendesha pikpiki maarufu kama bodaboda Manispaa ya Mpanda wamewalalamikia baadhi ya askari wa usalama barabarani mkoani Katavi wanaowachapa viboko wanapokuwa wakisafirisha abiria. Wamesema tabia ya askari hao imedumu kuanzia mwaka 2016 ambapo licha ya kutoa malalamiko katika miktutano mbalimbali ya hadhara inayoitishwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani bado wameendelea kupigwa.

CHUO CHA UALIMU SUMBAWANGA HATIHATI KUSITISHA KUDAHILI WANAFUNZI

Image
CHUO cha ualimu cha Sumbawanga kilichopo mkoani Rukwa huenda kikasitisha kudahili wanafunzi ajili ya kujiunga na chuo hicho baada ya Kanisa katoliki jimbo la Sumbawanga kudai majengo yake baada ya serikali kutowapatia majengo mengine kama walivyoahidiana. Katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa RCC hivi karibuni alisema majengo yanayotumiwa na chuo hicho ni mali ya kanisa katoliki ambalo liliyatoa kwa serikali mwaka 1974 ili yatumike kama ofisi za mkoa wakati Mkoa huo ulipokuwa mpya na ukiwa hauna Ofisi.

BAVICHA WATOA NENO KWA SERIKALI KUHUSU AMANI NCHINI

Image
Baraza la vijana la Chadema (Bavicha) Mkoani Rukwa limeitaka Serikali kutumia gharama yoyote kulinda amani ya nchi inayoonesha dalili ya kutoweka kutokana na kukithiri kwa vitendo vya mauaji ya kinyama na utekaji unaofanywa watu wasiojulikana.

WANAWAKE WAMZIKA MWANAMKE MWENZAO ALIYETELEKEZWA NA MUMEWE KABLA NA BAADA YA KUFARIKI.

Image
Wanawake wa mtaa wa Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,hatimaye wamefanya mazishi ya mwanamke mwenzao Rosemary Robert Ismail makazi wa mtaa huo aliyefariki dunia siku sita zilizopita baada ya kutelekezwa na mumewe Bw.Abdalla Ibrahim akiwa mgonjwa. Wanawake hao wamesema wamefanya mazishi jana baada ya kupata kibali cha jeshi la Polisi Mkoani Katavi kinachowaruhusu kufanya hivyo baada ya ndugu zake kukosekana.

ACT-WAZALENDO WAINGILIA KATI MIGOGORO YA ARDHI KATAVI

Image
Viongozi wa Mkoa wa chama cha ACT-Wazalendo wakiwa na viongozi wa kata ya Sitalike,wamefika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga kwa ajili ya kutafuta mwafaka wa mashamba na mazao ya wananchi katika kata hiyo. Mwenyekiti wa chama hicho Bw.John Malack akiwa na Katibu wake Bw.Joseph Mona Mkuu wa Mkoa wakizungumzia hatua hiyo jana mara baada ya kutoka katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wamesema wamefikia hatua hiyo kama sehemu ya kusimamia maslahi ya wananchi kwa kuwa ni wajibu.