WAENDESHA PIKIPIKI WADAI KUPIGWA FIMBO NA ASKARI


Baadhi ya waendesha pikpiki maarufu kama bodaboda Manispaa ya Mpanda wamewalalamikia baadhi ya askari wa usalama barabarani mkoani Katavi wanaowachapa viboko wanapokuwa wakisafirisha abiria.
Wamesema tabia ya askari hao imedumu kuanzia mwaka 2016 ambapo licha ya kutoa malalamiko katika miktutano mbalimbali ya hadhara inayoitishwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani bado wameendelea kupigwa.

Kwa upande wake Afisa wa usalama barabarani kutoka jeshi la polisi Mkoani Katavi Samweli Shigera amekanusha waendesha bodaboda kupigwa na amewataka wanaotendewa vitendo hivyo waripoti polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahusika.
Mara kadhaa jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani limekuwa likituhumiwa kutumia nguvu kubwa kuwadhibiti waendesha bodaboda wanaokiuka sheria za usalama barabarani.
Habari zaidi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA