POLISI RUKWA WAANZISHA OPARESHENI KUSAKA MASHAMBA YA BANGI.

Jeshi la Polisi katika wilaya ya Kipolisi ya Raela Mkoani Rukwa limeanzishaa Oparesheni ya Kuyasaka mashamba yanayolima zao haramu ya bangi katika safu ya milima ya Lyamba Lyamfipa kwenye bonde la ziwa Rukwa.
Mkuu wa Polisi katika wilaya hiyo ya kipolisi ya Raela Mrakibu mwandamizi wa polisi Aloyce Nyantola akizungumza leo wakati akishuhudia vijana kutoka kata ya Kapenta wilayani Sumbawanga wakivuna shamba la bangi lenye ukubwa wa heka 2 amesema walipata taarifa za kilimo hicho kutoka kwa raia wema na ndipo walipoanza kuzifanyia kazi.
Katika Oparesheni hizo Nyantola ametoa wito kwa wananchi kuwa wema kuendelea kutoa taarifa huku akiwtaka pia kuzingatia sheria za nchi  na kuachana na kilimo cha mazao haramu.
Kwa upande wake mkuu wa upelelezi wa wilaya hiyo ya kipolisi ya Raela mrakibu msaidizi Beda Msola amesema wananchi hao wamekuwa wakiendesha kilimo cha madawa ya kulevya ikiwemo bangi katika milima ya safu ya milima ya lyamba lyamfipa kwa kigezo kuwa maeneo ya msituni hayafikiki kirahisi.
Miongoni mwa maeneo ambayo Oparesheni imeanza leo ni pamoja na kata ya Ilemba,Kapenta na Kaoze kufuatia kilimo hicho kushamiri katika maeneo hayo.
Hata hivyo Aprili 7 mwaka huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt.John Magufuli akiwa ziarani Mkoani Arusha,alitoa agizo kwa vyombo vya ulinzi na usalama kutofyeka mashamba ya bangi badala yake watafutwe wahusika wa kilimo hicho ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA