Posts

Showing posts from September, 2016

UKOSEFU WA FEDHA,WAZEE KATAVI WASHINDWA KUHUDHURIA MAADHIMISHO YA KESHO SIKU YA WAZEE DUNIANI YATAKAYOFANYIKA MKOANI MBEYA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo mashama-Katavi UMOJA wa wazee Mkoani Katavi umeshindwa kupeleka wawakilishi katika maadhimisho ya Siku ya wazee Duniani yanayotarajiwa kufanyika kitaifa kesho Mkoani Mbeya. Moja ya mikitano iliyokuwa ikijadili maslahi ya wazee(PICHA NA Issack Gerald )Septemba 2014                                            

MATATIZO MENGI BADO SOKO KUU LA WILAYA YA MPANDA

NA.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika Katavi SOKO kuu la Mpanda,mkoani Katavi linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo msongamano wa wafanyabiashara, mpangilio holela na ukosefu wa taa za kusaidia ulinzi.

MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA AONGOZA HARAMBEE KUWACHANGIA WAATHIRIKA TETEMEKO LA ARDHI KAGERA SHILINGI MIL.4,656,500 ZAPATIKANA.

Image
NA.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika Katavi MKUU wa Wlaya ya Tanganyika Bw.Saleh Mbwana Mhando ameongoza harambee ya kuwachangia waathirika wa tetetmeko la ardhi Mkoani Kagera ambapo Shilingi MIL.4,656,500/=zimepatikana ambapo kati ya hizo shilingi MIL.4,416,000/= ni fedha taslimu.                                                                               

MWALIMU WILAYANI MLELE AHUKUMIWA JELA MIAKA 30 KWA KUSABABISHA UJAUZITO KWA MWANAFUNZI WAKE

Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi MAHAKAMA ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi imemhukumu Mwalimu wa Shule ya Msingi Ukingwamizi, Une Thom kutumikia kifungo cha miaka 32 jela.

TANESCO NA UFAFANUZI WA TATIZO LA UMEME MPANDA KATAVI

Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi Uchakavu na ubovu wa mitambo ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa katavi ndiyo imeelezwa kuwa ndio chanzo kinachosababisha kutokuwa na umeme wa uhakika. Meneja mahusiano wa

MKUU WA WILAYA YA MPANDA AHAMASISHA HARAMBEE KUWACHANGIA WAATHIRIKA WA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA

Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama- Mpanda Katavi MKUU wa Wilaya ya Mpanda Bi. Lilian Charles Matinga,ametoa wito kwa wakazi wa Wilaya ya Mpanda kujitokeza kwa hiari katika harambee ya kuwachangia wakazi wa Mkoa wa Kagera walioathiriwa wa tetemeko la ardhi Septyemba 10 mwaka huu.

KAMATI TENDAJI MRADI ELIMU JUMUISHI MKOANI KATAVI NA UJUMBE WA UGENI KUTOKA MIKOANI WAFANYA KIKAO KUJADILI MAHITAJI YA WATOTO WENYE ULEMAVU

Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Katavi JAMII Mkoani Katavi imetakiwa kushiriki ipasavyo kuwafichua watoto wenye Ulemavu ili wapatiwe elimu kama watoto wengine wasio na ulemavu.

KUTOKA WILAYANI MLELE KATAVI -TUKIO LA NYUMBA KUCHOMWA MOTO

Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama –Mlele Katavi NYUMBA za wakazi ambazo idadi yake haijafahamika eneo la Namba moja lililopo Kata na Tarafa ya Inyonga Wilayani Mlele Mkoani Katavi,leo zimeteketezwa kwa moto na baadhi ya mali zilizokuwemo kuteketezwa katika nyumba hizo. Kwa mjibu wa baadhi ya wakazi ambao mali zao zimeteketea ,wakizungumza na Mpanda Radio Kwa njia ya Simu kwa masikitiko makubwa akiwemo Bi.Tatu M asanja wamesema kuwa, tukio hilo ambalo wameliita la kushtukiza asubuhi ya leo,wamedai limetekelezwa na askari Mkoani Katavi kuanzia majira ya asubuhi. Wametaja baadhi ya mali zao ambazo zimechomwa kwa moto mbali na nyumba zao kuwa ni pamoja na Vyakula na mavazi huku watoto wakizagaa ovyo katika eneo hilo bila wazazi wao baada ya wazazi kukimbilia kusikojulikana kufuatia wengine kupigwa na askari hao. Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi ACP damasi Nyanda,akizungumza na Mpanda Radio Kwa njia ya Simu mchana wa leo,amesema hajapata taarifa ya utekelezwaji wa

KUHUSU SIKU YA AMANI DUNIANI,WAKAZI MKOANI KATAVI WASEMA HIKI

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Katavi BAADHI ya wakazi Mkoani Katavi,wameshauri siku ya amani duniani itumike kutafakari namna ya kudumisha amani iliyopo hapa nchini.                                   

TAASISI YA TWAWEZA WAENDESHA KONGAMANO LA WADAU WA ELIMU MPANDA,WAZAZI WALEZI WATAKIWA KUTAMBUA UMUHIMU WA ELIMU KWA WATOTO

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda Katavi WAZAZI na WALEZI katika manispaa ya Mpanda Mkoani wameshauri jamii kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto ikiwa ni urithi kwa maisha bora. Wanafunzi mkoani Katavi                                                

NYUMBA ILIYOTEKETEA KWA MOTO JUZI ,CHUMBA CHA MPANGAJI HASARA NI ZAIDI YA MILIONI MOJA NA LAKI TANO(1,500,000).

Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda Imebainika kuwa janga la moto lililotokea juzi katika Mtaa wa Mpadeco Kata ya Mkananyagio Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,umesababisha Bi.Grace Emmanuel Mkazi wa mtaa wa Mpadeco kata ya Makanyagio kupata hasara ya Zaidi ya Shilingi Miloni moja na laki tano (1,500 ,000). B.Grace amesema Moto huo uliozuka mchana uliunguza Vitanda 2 vyenye thamani ya laki tano na elfu sitini(560,000),Magodoro mawili 5 kwa 6 yenye thamani ya Shilingi laki tatu(300,000),Maguni ya Mpunga 4 thamani yake zaidi ya Shilingi laki 2(200,000),Upotevu wa fedha taslimu Shilingi laki nne na nusu za mkopo zilizopotea wakati wa uokozi na nguo ambazo tahamani yake haijafahamika. Akizungumza akiwa nyumbani kwake muda mfupi baada ya kutoka hospitali ya Wilaya ya Mpanda,alikolazwa baada ya kuzimia kutokana mshtuko alioupata baada ya kupata hasara hiyo,amesema kuwa hata hivyo hajatambua kiasi alichotumia kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo amekwishafungua jarada Polisi ili ili kufany

NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO MPANDA

Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda Moto umeunguza nyumba ya Familia moja na kusababisha hasara ya mali ambayo thamani yake haijajulikana katika mtaa wa Migazini kata ya Makanyagio   Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.

MKUU WA WILAYA TANGANYIKA:ENEO LA LUHAFE SASA KUJENGWA MJI WA MAKAZI NA BIASHARA.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Bw.Salehe Mbwana Mhando,ametangaza wakazi wa eneo la Luhafe lililopo kata ya Majalila,kulitumia eneo hilo kwa makazi na shughuli za kibiashara baada ya mgogoro wa uhalali wa eneo hilo wa muda mrefu. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Bw.Saleh Mbwana Mhando akihutubia wakazi wa kitongoji cha Luhafe(PICHA NA.Issack Gerald)Septemba 16,2016                                                                           

VIJIJI ZAIDI YA 14 VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO KUPATA UMEME WA REA AWAMU YA III MWAKA 2016

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda,Katavi Meneja wa TANESCO mkoa wa Katavi Mhandisi Julius Sabu amesema katika awamu ya tatu ya umeme wa REA wanampango wa kusambaza umeme katika vijiji ambavyo havikupitiwa na mpango huo katika awamu zilizopita.                                    

WAKAZI WILAYANI TANGANYIKA WAAGIZWA KUONGEZA KASI YA KUJENGA SEKONDARI KILA KATA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika WAKAZI wilayani Tanganyika Mkoani Katavi kwa Kushirikiana na uongozi wa vijiji na kata   katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika,wameagizwa kuweka mikakati ya ujenzi wa shule za Sekondari kila kata ,ili kila mwanafunzi asome bila kuhangaika na badala yake apate elimu bora.                                       Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando akishiriki ujenzi Shule ya sekondari ya Bulamata  kata ya Bulamata(PICHA NA Issack Gerald)Septemba 16,2016                                          Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika akizungumza na wananchi eneo la kijiji cha Busongola kunakojengwa Shule ya Sekondari Bulamata(PICHA NA.Issack Gerald) Septemba 16,2016                                                       Wananchi wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Isubangala kijiji cha Isubangala kata ya Ilangu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya(hayupo pichani)(PICHA NA.iSSACK gERALD) Septemba 16,2016

MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA AAGIZA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 200 ZA WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU CHAMA CHA USHIRIKA TAMCOS KULIPWA NDANI YA SIKU 15.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Bw.Saleh Mbwana Mhando,ameuagiza uongozi wa bodi ya Chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS na Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bw.Luxford Mbunda,kuhakikisha wanalipa   zaidi ya Shilingi milioni 200 wanazodai wakulima wa zao la tumbaku wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa misimu 3 ya kilimo kuanzia mwaka 2011-2015 kabla ya Septemba 30 mwaka huu. Baadhi ya Wakulima wa Zao la Tumbaku wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(hayupo pichani) katika Ofisi za TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando Aliyesimama akihutubia wakulima wa tumbaku wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald)                                       Wakulima wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara uliofanyika Septemba 15,2016 kati

KIFO CHA MTU KUJINYONGA KATAVI,NDUGU,MASHUHUDA WASIKITIKA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi MTU mmoja anaekadiliwa kuwa na umri wa miaka 30 Innocent Milambo mkazi wa mtaa wa kigoma kata ya Makanyagio wilayani Mpanda   mkoani Katavi,amekutwa amekufa kwa kujinyonga   usiku wa kuamkia leo kwa kile kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi ACP Damasi Nyanda(PICHA NA.Issack Gerald)                                                             

MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA ATOA AGIZO KWA WATUMISHI WA WILAYA HIYO,ATAKA WAFANYE KAZI KWA WELEDI KWA MANUFAA YA WANANCHI NA KUIEPUKA RUSHWA.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo-Tanganyika Katavi MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Bw.Saleh Mbwana Mhando,amewaagiza watumishi wa umma Wilayani Tanganyika,kufanya kazi kwa weledi na kasi ili kufikia maendeleo yanayohitajika kwa wananchi. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(Mwenye tai) akiwa na baadhi ya watumishi wa Wilaya hiyo baada ya kikao(PICHA NA.Issack Gerald)Septemba 14,2016 Baadhi ya watumishi wa idara mbalimbali halmashauri ya wilaya ya Tanganyika katika kikao cha utumishi na mkuu wa Wilaya(Hayupo pichani)(PICHA NA.Issack Gerald)Septemba 14,2016                                           

MIFUGO KUZAGAA MITAANI KWAPIGWA WILAYANI KIBONDO

Na.Mwandishi wetu- Jastini Cosmas-Kibondo Kigoma HALMASHAURI ya wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma,imewaagiza wananchi katika Halmshauri hiyo kutoachia mifugo yao ovyo katika kipindi hiki cha msimu wa kilimo,kutokana na mifugo hiyo kuwa waharibifu wa mazao.

KINACHOIGUSA MIKOA YA KATAVI,RUKWA NA KIGOMA KUTOKA VIKAO VYA BUNGENI DODOMA LEO SEPTEMBA 8,2016

Image
Na.Issack Gerald-Dodoma Serikali imesema,inaendelea kuweka mikakati ya kuwa na kiwanda cha kutengeneza pikipiki za bodaboda ili kuwajengea vijana kuwa na uwezo wa kununua pikipiki zao,kuliko kuendelea kuwatumikia matajiri wenye uwezo wa kumiliki pikipiki hizo. Wabunge wakiwa bungeni Mjini Dodoma leo Septemba 8,2016                                   

KUMEKUCHA BUNGENI TENA ,MISWADA 6 UKIWEMO WA HABARI KUWASILISHWA,WABUNGE WA UPINZANI MGUU SAWA BUNGENI

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo MKUTANO wa Nne wa Bunge la 11 unatarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, huku miswada sita ukiwemo wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ukitarajiwa kuchukua nafasi kubwa.