Posts

Showing posts from March 22, 2018

WAVUVI RUKWA WAIPONGEZA ZAMBIA KUONDOA ZUIO BIASHARA YA SAMAKI

Image
WAVUVI wa samaki katika ziwa Tanganyika wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameishukuru serikali ya Zambia kwa kuondoa marufuku ya biashara ya samaki katika nchi hiyo. Marufuku hiyo ilikuwa imewekwa kwa takribani wiki mbili zilizopita kutokana na kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindu pindu nchini humo.

WANAFUNZI WAKUMBWA UGONJWA WA AJABU

Image
WANAFUNZI wa kike katika Shule ya Msingi Kabwe  mwambao mwa Ziwa Tanganyika  wilayani Nkasi mkoani Rukwa,wanaugua ugonjwa wa ajabu unaosababisha wapige kelele hovyo,kutetemeka na kisha kuanguka. Mkuu wa Shule hiyo,Amon Kawana alisema ugonjwa huo ulianza kutokea shuleni hapo tangu mwishoni mwa mwaka jana ambapo mpaka sasa ni wanafunzi wapatao 20 wa kike wameshakumbwa na ugonjwa huo na kusababisha taharuki  shuleni hapo.

RAIS MAGUFULI AFYANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA ULINZI WA ISRAEL IKULU

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Israel Mhe.Avigdor Lieberman Ikulu Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Ali Mwinyi,Balozi wa Israel hapa nchini Mhe.Noah Gal Gendler,viongozi wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Polisi.

WATU WAWILI MIKONONI MWA POLISI KATAVI KWA KUHAMASISHA MAANDAMANO

Image
Na.Issack Gerald-Katavi Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi ACP Damas Nyanda amesema jeshi hilo linawshikilia watu wawili wakituhumiwa kuhamasisha maandamano kwa njia ya Mtandaoni. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi ACP Damas Nyanda Kamnada Nyanda ametoa kauli wakati akizungumza na mtandao huu Ofisini kwake kuhusu namna ambavyo jeshi hilo limejipanga kudhibiti maandamano hayo. Aidha Kamanda Nyanda ametoa onyo kali kwa watu watakaohamasisha au kuandamana ambapo amesema watakaoandamana watakabiliwa na hatua kali za kisheria. Baadhi ya wananchi Mkoani Katavi wakiwemo Said Rashid Mdemela,Juma Bairon Mwanda,Jonathan John Midende,Paul Makelele na Wenseslaus Obed wamesema maandamano hayo hayana tija kwa watanzania na hawatashiriki kwa sababu ni wakati wa kufanya kazi za maendeleo na kuepuka mkono wa sheria kwa mambo yasiyokuwa na maana. ‘ ’Majina ya watuhumiwa hayakuwekwa wazi kwa sababu za kiuchunguzi na upelelezi utakapokamilika wanatarajiwa kufikishwa mahakamani