Posts

Showing posts from October 19, 2017

TANZANIA NA KAMPUNI YA BARRICK WAFIKIA MWAFAKA SUALA LA MADINI

Image
Majadiliano kati ya Tanzania na timu ya wawakilishi wa kampuni ya Barrick Gold inayomiliki migodi ya madini hapa nchini,yamekamilika na makubaliano kati ya pande hizo yametiwa saini leo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli Ikulu,Jijini Dar es Salaam. Timu ya Barrick Gold Corporation ilikuwa imeongozwa na Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni hiyo Prof.John Thornton wakati timu iliyowakilisha Serikali ya Tanzania imeongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi. Miongoni mwa mambo waliyokubaliana ni kutekeleza mwelekeo mpya wa biashara ya madini ambapo kutakuwa na mgawanyo sawa wa faida ( yaani Tanzania kupata asilimia 50 na Barrick Gold Corporation kupata asilimia 50 ya faida ) na kuundwa kwa kampuni ya ubia wa usimamizi wa migodi ya madini iliyopo Tanzania ambayo itakuwa na makao makuu yake Mwanza na ofisi ndogo Dar es Salaam nchini Tanzania badala ya nchini Uingereza. Mengine ni kufunga ofisi za uhasibu n

WAKURUGENZI MANISPAA YA SUMBAWANGA KIKAANGONI FEDHA ZA WAKANDARASI

WAKURUGENZI wa halmashauri ya wilayani ya Sumbawanga na Manispaa mkoani Rukwa wameingia matatani kwa kitendo cha kuhamisha fedha za malipo ya wakandarasi na kuzipeleka kutengeneza madawati.

CWT NKASI-TUMECHOKA KUWAKINGIA KIFUA WALIMU WASIOKUWA NA NIDHAMU

Image
CHAMA Cha Walimu  Tanzania (CWT) wilayani Nkasi mkoani Rukwa kimewanusuru walimu 19 kufukuzwa kazi kutokana na utovu wa nidhamu.

MANISPAA YA MPANDA YATOA ELIMU KWA WATU WENYE ULEMAVU

Image
Na.Issack Gerald-Katavi HALMASHAURI ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imeendesha semina kwa watu wenye ulemavu,ili kuwaelekeza njia sahihi wanazotakiwa kutumia ili kukidhi vigezo vya kupewa mikopo kwa ajili ya kufanya shughuli za maendeleo.

RPC KATAVI:WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI HAIKUBALIKI

Image
Na.Issack Gerald-Katavi Kamanda wa polisi Mkoa wa katavi Damasi Nyanda ametoa wito kwa wananchi katika halimashauri ya wilaya ya Mlele kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi dhidi ya watuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati wanapowakamata.

SEKTA YA UCHIMBAJI MADINI MKOANI KATAVI,VIJANA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA

Vijana mkoani Katavi wametakiwa kutumia fursa ya machimbo ya madini ya dhahabu yaliyopo mkoani Katavi katika kujiinua kiuchumi.

WATU WENYE ULEMAVU MKOANI KATAVI KESHO KUPATIWA ELIMU YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Na.Issack Gerald-Katavi IDARA ya maendeleo ya ustawi wa jamii Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,kesho inatarajia kuendesha semina kwa watu wenye ulemavu ili kuwapatia elimu ya namna ya kujikwamua na umaskini kwa kufanya shughuli za maendeleo.

WAKURUGENZI NCHINI WAPEWA AGIZO KALI KUHUSU MAFAO YA WATUMISHI

Image
Na.Issack Gerald Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh.Suleman Jafo,amewaagiza wakurugenzi watendaji wa Halmashauri na maafisa utumishi hapa nchini, kuwasilisha michango ya watumishi katika mifuko ya hifadhi ya jamii. Waziri Jafo ametoa kauli hiyo leo kupitia Clouds tv kufuatia malalamiko kutoka kwa baadhi ya watumishi hapa nchini wakiwemo walimu wakilalamika kutopata mafa o yao kwa wakati wanapostaafu. Hata hivyo siyo mara ya kwanza serikali kuagiza mafao ya watumishi yawasilishwe katika mifuko ya hifadhi ya jamii suala ambalo waziri Jafo amesema kama ulikuwa ni uzembe wa waajiri hautaendelea wala kuvumiliwa. Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  au ukurasa P5Tanzania Limited