Posts

Showing posts from November 29, 2017

MAKAMU WA RAIS MH.SAMIA SULUHU AMEMJULIA HALI MH.TUNDU LISSU

Image
Na.Issack Gerald Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana amemjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki Mhe.Tundu Lissu anayepata matibabu katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya. Mhe.Samia Suluhu Hassan amemfikishia salamu za pole kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli ambaye amemtakia matibabu mema na kupona haraka ili arejee nyumbani na kuendelea na majukumu yake. Mhe.Tundu Lissu amemshukuru Mhe.Rais Magufuli na Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kumjulia hali na amewatakia heri katika majukumu yao. Habari zaidi na P5TANZANIA LIMITED

RAIS KENYATTA AMEANZA SAFARI YA PILI MUHULA WA PILI WA URAIS

Image
Na.Issack Gerald Hatimaye jana Rais Uhuru Kenyatta ameapishwa rasmi kwa muhula wa pili wa miaka mitano katika sherehe zilizofana kwenye Uwanja wa Kasarani mwezi mmoja baada ya kuibuka mshindi wa uchaguzi uliosusiwa na mpinzani mkuu Raila Odinga. Kulikuwa na nderemo na shangwe katika uwanja huo kutoka kwa maelfu ya wananchi wengi wao wafuasi wa muungano wa chama tawala cha Jubilee waliojaa kwenye Uwanja wa Michezo wa Kimataifa wa Moi, Kasarani. Uwanja huo unaingiza watu 60,000 lakini habari zinasema walioingia walikuwa 100,000. Wageni waalikwa na watu mashuhuri wapatao 40 walihudhuria sherehe hizo wakiwemo zaidi ya viongozi wakuu wa nchi 10. Kenyatta,55,alishinda uchaguzi mkuu wa marudio wa Oktoba 26 kwa asilimia 98.Uchaguzi huo ulifanyika baada ya matokeo ya ushindi wa Agosti 8 kufutwa na Mahakama ya Juu kwa maombi ya Odinga aliyewasilisha ushahidi wa dosari na ukiukwaji wa katiba. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  ni miongoni viongozi w

KASI YA KUMNASUA MTOTO WA KIKE HASA MIMBA ZA UTOTONI YAZIDI KUSHIKA KASI

Na.Issack Gerald WATOTO wa kike mkoani Rukwa wamepewa mafunzo maalumu ya namna ya kuzitambua changamoto mbalimbali zinazowakwamisha kuzitumia fursa zilizopo katika kutekeleza matarajio yao ili waweze kujitegemea. Akizungumza katika uzinduzi wa mradi uitwao U-report unaotekelezwa na Tanzania Girl Guides Association mkufunzi wa mradi huo,Emiliana Stanslaus amesema wahitimu wapatao 20 katika kila halmashauri wamewezeshwa namna ya kuwasaidia wasichana wenzao katika kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi yao. Amesema wasichana hao walipata mafunzo ya siku mbili ambapo watawasaidia wanafunzi wenzao wa kike katika shule za msingi na sekondari na wasichana waliopo vijijini katika kukabiliana na changamoto mbalimbali katika maisha yao ikiwa ni pamoja na kubakwa na pia kupata mimba za utotoni. Emiliana amesema mradi huo utatekelezwa katika halmashauri za Sumbawanga vijijini,Kalambo,Nkasi na Sumbawanga Manispaa kwa njia ya kutuma ujumbe wa maandishi ya simu kwenda namba maalumu ya 150