Posts

Showing posts from November 18, 2017

MENEJA MPANDA RADIO FM ATOA NENO KWA WANASALAAM,LEO KUCHEZA MECHI YA KIRAFIKI

Image
Na.Issack Gerald Wadau wa salaamu kupitia vyombo vya habari Mkoani Katavi,wameaswa kushiriki kwa kiasi kikubwa kuibua masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kuibua matukio yanayoiathiri jamii kama ukatiri. Baadhi ya watuma Salaamu Mkoani Katavi wakiwa katika kikao na watumishi Mpanda Radio katika Ukumbi wa Mpanda Radio(PICHA NA.Issack Gerald) Wito huo umetolewa leo na Meneja wa kituo cha Mpanda Radio Bw. Revocatus Msafiri,wakati akizungumza na viongozi wa vikundi vya wanasalaamu kuanzia ngazi ya kata hadi Mkoa kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa studio ya Mpanda Radio. Katika hatua nyingine, Bw.Msafiri amesema bonanza la leo la mchezo wa mpira wa miguu baina ya watumishi Mpanda Radio na watuma salaamu Mkoani Katavi linalenga kupanua wigo wa kufahamiana na kuongeza mahusiano yenye tija  kwa jamii. Baadhi ya wafanyakazi wa Mpanda Radio Kwa upande wao watuma salaamu mbali na kuipongeza Mpanda Radio kwa matangazo yanayozingatia  mahitaji ya jamii,pia wamekiomba cho

TAMKO LA RAIS KUHUSU MITA 60 ZA MTONI, VIONGOZI ELIMU WAMEENDELEA KUTOA UFAFANUZI

Image
Na.Issack Gerald Mwenyekiti wa bonde la mto Mpanda Bw.Mikidadi  Marubaro Mbuganzito amewataka wakazi wote waishio kando na mto huo, kutii sheria ya kutofanya shughuli zozote  za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka katika kingo za mto. Pamoja na mambo mengine Bw.Mikidadi  Mbuganzito amesema agizo la rais kuhusu shughuli za kibinadamu kama kilimo kufanyika kandokando ya mto lilihusu eneo la Kagera pekee na siyo mito yote nchini. Kauli hiyo imekuja baada ya mkulima mmoja Bundala Sweya wa kijiji cha Itenka B kudai kukamatwa na kudaiwa faini ya shilingi laki mbili baada ya kulima kando ya mto huo akidai kutekeleza agizo la rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli. Kwa upande wake diwani wa kata ya itenka Joseph Laurent amewataka wananchi kushirikiana na serikali ili kama kuna mambo hayaendi sawa wawataarifu viongozi husika ili wasaidiwe. Novemba 7 mwaka huu rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli akiwa Kyaka mkoani kagera alisema mamla

WANAFUNZI 15 WAMEHITIMU ELIMU YA BIBLIA

Image
Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi Baadhi ya wanafunzi wa shule ya biblia FPCT Katumba Wakiwa na baadhi ya watumishi Mpanda Radio Viongozi wa dini Mkoani Katavi wameaswa kutumia taaluma na karama zao katika kuunganisha jamii inayomtambua mungu mionyoni mwao na kuhimiza waumnini kutotenda matukio yanayoleta athari kwa jamii hapa nchini. Wito huo umetolewa jana na Mchungaji Zacharia Andrea kutoka chuo cha Biblia Bigabilo kilichopo mkoani Kigoma,aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kuhitimu wanafunzi wa shule ya biblia FPCT Katumba yaliyofanyika Misheni ya Katumba akisema viongozi wanatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa matendo mema. Kwa upande wake Mkuu wa shule ya biblia FPCT Katumba Mchungaji Elisha Musenda,katika taarifa yake amesema,shule ya biblia FPCT Katumba,imesaidia kupatikana viongozi wazuri wa kanisa wanaoshirikiana na jamii katika kuleta maendeleo hapa nchini. Katika risala ya wanafunzi ambayo imesomwa na mwinjilisti  Moris Samson,wameomba mafunzo yawe endelevu kati