TAMKO LA RAIS KUHUSU MITA 60 ZA MTONI, VIONGOZI ELIMU WAMEENDELEA KUTOA UFAFANUZI

Na.Issack Gerald

Mwenyekiti wa bonde la mto Mpanda Bw.Mikidadi  Marubaro Mbuganzito amewataka wakazi wote waishio kando na mto huo, kutii sheria ya kutofanya shughuli zozote  za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka katika kingo za mto.

Pamoja na mambo mengine Bw.Mikidadi  Mbuganzito amesema agizo la rais kuhusu shughuli za kibinadamu kama kilimo kufanyika kandokando ya mto lilihusu eneo la Kagera pekee na siyo mito yote nchini.

Kauli hiyo imekuja baada ya mkulima mmoja Bundala Sweya wa kijiji cha Itenka B kudai kukamatwa na kudaiwa faini ya shilingi laki mbili baada ya kulima kando ya mto huo akidai kutekeleza agizo la rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli.

Kwa upande wake diwani wa kata ya itenka Joseph Laurent amewataka wananchi kushirikiana na serikali ili kama kuna mambo hayaendi sawa wawataarifu viongozi husika ili wasaidiwe.

Novemba 7 mwaka huu rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli akiwa Kyaka mkoani kagera alisema mamlaka zinazosimamia mazingira yafaa ziangalie namna ya kutekeleza sheria ya mazingira nchini

HABARI ZAIDI NI P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA