Posts

Showing posts from February 9, 2018

WAZIRI AAGIZA WALIONYANG’ANYWA PIKIPIKI NA POLISI KURUDISHIWA

Image
WAZIRI wa Mambo ya Ndani,Dkt.Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi nchini kuziachia pikipiki ambazo wamezishikilia kwa mda mrefu na zina makosa madogo. Dkt.Nchema amesema waziachie na wasikae nazo kwa mda mrefu mpaka zikawa vyuma chakavu. Dkt.Mwigulu amesema zile zenye makosa makubwa kama uhalifu wa kivita,madawa ya kulevya na wale wanaotelekeza wabaki nazo na wafanye utaratibu wa kuwapeleka mahakamani au kuziteketeza huku akisema zenye makosa madogo wazitatue haraka na kuwarudishia na kuwapa elimu wamekosea wapi.

MAGAIDI WAWILI HATARI WA IS WAKAMATWA

Image
Raia wawili wa Uingereza wanaodhaniwa kuwa wanachama wa kikundi cha wapiganaji wa Kiislam cha IS wanashikiliwa na kundi la wapigaji wa Kikurd. Alexanda Kotey(34) na mwenzake El Shafee Elsheikh(29) ni miongoni mwa vijana wawili waliokuwa wanasakwa kati ya wenzao ambao walikwisha kukamatwa. Image caption Magaidi Alexanda Kotey na El Shafee Elsheikh Kundi hili la vijana wanne kutoka raia wa Uingereza ndani ya kundi la IS walikuwa ni kundi hatari linalofahamika kama Beatles hiyo ikiwa ni kutokana na lafudhi yao wanapozungumza.

CHADEMA WAZUNGUMZIA KIFO CHA KADA WAKE MKONGWE

Image
Mwenekiti wa Chadema taifa Mh.Freeman Mbowe ameeleza kusikitishwa na taarifa ya kifo cha Tambwe Richard Hizza. Amesema kuwa Hizza alipotoka CCM na kwenda upinzani kwake yeye ni kama alikuwa anatubu kwani hakutaka kufa akiwa ndani ya CCM. Mbowe amesema hayo jana Februari 8 baada ya kusikia taarifa ya kifo cha Tambwe Richard Hizza ambaye amefariki ghafla usiku wa kuamkia jana. Kufuatia kifo cha Hizza Mwenyekiti wa CHADEMA amedai wao ili kumuenzi kamwe hawawezi kurudi nyuma bali watasimamia yale wanayoyaamini ili kumuenzi na kufikia matamanio ambayo kiongozi huyo alikuwa akiyatamani.