WAZIRI AAGIZA WALIONYANG’ANYWA PIKIPIKI NA POLISI KURUDISHIWA


WAZIRI wa Mambo ya Ndani,Dkt.Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi nchini kuziachia pikipiki ambazo wamezishikilia kwa mda mrefu na zina makosa madogo.
Dkt.Nchema amesema waziachie na wasikae nazo kwa mda mrefu mpaka zikawa vyuma chakavu.
Dkt.Mwigulu amesema zile zenye makosa makubwa kama uhalifu wa kivita,madawa ya kulevya na wale wanaotelekeza wabaki nazo na wafanye utaratibu wa kuwapeleka mahakamani au kuziteketeza huku akisema zenye makosa madogo wazitatue haraka na kuwarudishia na kuwapa elimu wamekosea wapi.

Alisema ipo haja ya vijana sasa kufundishwa zaidi kuhusu sheria ya usalama barabarani ili kupunguza ajali ya pikipiki na mlundikano wa pikipiki katika vituo vya polisi nchini kwani kila napopita vituo vya polisi hukuta pikipiki ni nyingi na makosa yao ni madogomadogo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA