Posts

Showing posts from January 19, 2018

WAZIRI AVUNJA BODI

Image
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe hii leo amevunja Bodi za Wakurugenzi za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Jiji la Arusha na Musoma. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari ambayo imesainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiy Prof.Kitila Mkumbo imeonesha Waziri Kamwelwe amesema kuwa amefanya hivyo baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wa Bodi hizo. Aidha taarifa hiyo inaeleza kuwa tayari mchakato wa kuunda bodi mpya umeanza na zitatangazwa mara zitakapokamilika. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

WABUNGE 11 WAVULIWA UANACHAMA

Image
Chama tawala cha ZANU-PF nchini Zimbabwe jana kimetangaza kuwafukuza wabunge wake 11 ambao ni washirika wa Rais wa zamani wa nchi hiyo Robert Mugabe. Maamuzi ya kuvuliwa uanachama wabunge hao yalitolewa na kutangazwa Bungeni na Naibu Spika wa Bunge la Zimbabwe,Mabel Chinomona baada ya Bunge hilo kupokea barau kutoka kwenye chama cha ZANU PF iliyosema wabunge hao wamefukuzwa kwa mujibu wa Katiba ya Zimbabwe kupitia kifungu namba 129 (1) (k). Naibu Spika alisema kuwa wabunge waliofukuzwa ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani, aliyekuwa Waziri wa Nishati,aliyekuwa Waziri wa Michezo, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na wabunge wengine wa majimbo mbalimbali nchini humo.  Kufuatia zoezi hilo Bunge limetangaza nafasi wazi katika majimbo hayo 11 na kuijulisha Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe kuhusu uwepo wa nafasi za wazi katika majimbo hayo kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo ili zoezi la uchaguzi liweze kufanyika kupata wawakilishi wa Wanachi.  Habari zaidi ni P5TANZANIA L

MSIMAMO MPYA WA RAIS MSEVENI KUHUSU KUNYONGA WATU

Image
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema anatafakari uwezekano wa kuanza tena kuwanyonga wahalifu nchini humo. Rais Museveni amesema licha ya kwamba yeye ni "Mkristo" kuwa dini yake imemzuia kutekeleza hukumu ya kifo dhidi ya wale ambao wamehukumiwa kunyongwa, hata hivyo amesema hali hiyo imekuwa ikiwatia moyo wahalifu. Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo wakati wa sherehe za kuhitimu kwa askari wa idara ya magereza katika gereza la Luzira jijini Kampala. Mpaka sasa ni miaka 13 sasa tangu Uganda ilipotekeleza hukumu ya kifo dhidi ya wahalifu. Watetezi wa haki za kibinadamu wameshutumu tamko hilo la Rais Museveni na kusema adhabu ya kifo haikomeshi uhalifu. Mara ya mwisho kwa Rais Museveni kuidhinisha hukumu ya kifo itekelezwe ilikuwa katika gereza la Luzira mwaka 1999 na mwaka 2005 aliidhinisha mahakama ya kijeshi kutekeleza hukumu ya kifo Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

WAKAZI WILAYANI MPANDA WALALAMIKIA UBOVU WA MIUNDOMBINU YA RELI

Image
Wananchi wilayani Mpanda   mkoani Katavi wamelalamikia shirika la reli kwa kutorekebisha miundombinu ya reli kwa wakati   katika eneo la Ugala mpaka Rumbe. Wananchi hao wameeleza kuwa kumekua na ajali nyingi zikitokea kutokana na miundombinu ya eneo hilo kutokuwa salama kwa usafiri hali inayosababisha kupotea kwa mizigo. Mkuu wa kituo cha reli  Mpanda  Bw.Vivian Lyapembile amesema kuwa pamoja na changamoto wanazopata  kwa sasa  ila wana ufahamu na  tatizo hilo na tayari wameanza mchakato wa kukarabati eneo hilo. Hivi karibuni kumekuwa na changamoto ya usafiri kwa wasafiri wanaotumia usafiri wa treni hali inayosababishwa uchakavu wa miundo mbinu kwa baadhi ya maeneo pamoja na maeneo mengine reli kusombwa maji ya mvua zinazoendelea kunyesha.  Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

MKOANI WA RUKWA WAZINDUA KAMPENI YA UPANDANI MITI

Image
MKOA wa  Rukwa umezindua kampeni ya upandaji miche ya miti kwa lengo la kuhifadhi mazingira ambapo katika kipindi cha mwaka huu unatarajia kupanda jumla ya  miche milioni sita katika halmashauri zote nne za mkoa huo. Akizundua kampeni katika halmashauri ya wilaya ya Kalambo katika mji wa Matai,mkuu wa mkoa huo Joachim Wamgabo alisema kila halmashauri italazimika kupanda miche isiyopungua milioni 1.5 ambapo mpaka sasa tayari mkoa mzima umeotesha miche milioni 2,173,649 sawa na asilimia 36 ya miche itakayo pandwa. Alisema yeye  amezindua kampeni hiyo kinachofuata ni watendaji wa serikali kuhakikisha wanasimamia na kutekeleza na ambapo itakapofikia mwishoni mwa mwaka halmashauri ambayo haitafikia lengo itatozwa faini ya shilingi milioni moja na fedha hizo itakabidhiwa halmashauri ambayo imetekeleza kampeni hiyo kwa asilimia mia moja. Awali kabla ya kuzindua kampeni hiyo Wangabo alimuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Simon Ngagani amwajibishe Afisa mtendaji wa ki

WATOTO 400 WAKOSA ELIMU WILAYANI SUMBAWANGA

Image
JUMLA ya watoto wa wavuvi wapatao 400 waliopo katika kambi ya wavuvi ya Nankanga wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa ambao wamefikia umri wa kuanza darasa la kwanza wameshindwa kupata haki yao ya elimu kutokana na kutokuwa shule. Diwani wa kata ya Nankanga wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, Anyisile Kayuni alimwambia hayo mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo wakati akiwa katika ziara ya kukagua makambi ya wavuvi katika suala la kukabiliana na ugonjwa wa kipindu pindu. Alisema kuwa watoto hao wanaishi na wazazi wao katika kambi hiyo ya Nankanga iliyopo katika kijiji cha Nankanga,kata ya Nankanga na wamefikia umri wa kuanza shule ya msingi lakini wameshindwa kutokana na kuwa katika eneo walilopo hakuna shule. Diwani huyo alisema kuwa shule ya msingi ipo umbali wa kilomita tisa kutoka yalipo makambi hayo umbali ambao ni mkubwa huku ukikabiliwa na changamoto ya barabara kitendo kinachosababisha washindwe kwenda shule. alisema kuwa kwa kuliona hilo yeye kupitia uongizi wa makambi hayo wal

WILAYA YA NKASI YATANGAZA VITA DHIDI YA WANAUME WANAORUBUNI WANAFUNZI KUSHIRIKI MAPENZI.

Image
KATIKA kukabiliana na tatizo la mimba kwa wanafunzi wanaume wilayani Nkasi  Mkoani Rukwa wameonywa  kuacha mara moja tabia ya kuwaita watoto hao wa kike majina ya mahaba kwani yanawapelekea kujiona wamekua na kuanza kushiriki vitendo vya ngono. Wito huo umetolewa jana na afisa elimu Sekondari wilayani Nkasi Abel Ntupwa  kwenye kikao kazi kilichowajumuisha Wakuu wa shule 23 za sekondari wilayani Nkasi  kilichomshirikisha na afisa elimu wa mkoa Nestory Mloka kilicholenga kupeana mikakati namna ya kuboresha taaluma baada ya wilaya Nkasi kuporomoka sana kwenye mitihani ya kitaifa. Alisema hivi sasa watu wazima wamekua na tabia ya kuwaita watoto hao wa kike ambao ni Wanafunzi majina ya kimahaba kama  Baby kama mzaha na mwisho wa siku ujikuta Watoto hao wanajiingiza kwenye mtego huo mbaya na hivyo kuanza kushiriki vitendo vya mapenzi. Hivyo  kufuatia hari hiyo amedai kuwa ni marufuku kwa mtu yeyote  kumwita mtoto wa kike ambaye ni Mwanafunzi majina hayo ya Baby ili kuwaweka Watoto

WAMILIKI WAMABASI WAHITAJI KUKUTANA NA RAIS MAGUFULI

Image
Wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani,wameomba kukutana na Rais John Magufuli kumweleza matatizo yanayowakabili ikiwamo  vipengele wanavyodai kuwa ni kandamizi katika kanuni mpya za leseni za usafirishaji. Wamefikia hatua  hiyo baada ya kutofikia muafaka katika kikao kilichofanyika jana  jijini Dar es Salaam kati yao  na maofisa kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa  Usafiri wa Nchi kavu na Majini (Sumatra),Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, na Jeshi la  Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani. Akitangaza azimio hilo kwa niaba ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo,Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi hayo (Taboa),Enea Mrutu,alisema wataandika barua kuomba kukutana na Rais  Magufuli ili kumweleza matatizo yanayowasibu. Hata hivyo,Mwenyekiti wa Taboa,Mohammed Hood alisema kabla ya kuandikia barua ya kuomba kukutana na Rais, watafanya utaratibu wa kuonana na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa. Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Barabara,Johan

SERIKALI YATOA TAHADHARI KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA CHIKUNGUNYA

Image
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa tahadhari kuhusu ugonjwa wa homa ya Chikugunya ambao umeripotiwa na vyombo vya habari kutokea jijini Mombasa nchini Kenya. Mh.Dk.Ummy Mwalimu-Waziri wa Afya Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ugonjwa wa Chikunganya unasababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu wa aina ya Aedes. Taarifa ya wizara hiyo inaeleza kuwa ugonjwa huu si mgeni nchini Tanzania kwani ulishawahi kutokea. Dalili za ugonjwa wa Chikungunya ni homa kali,kuumwa kichwa,maumivu ya viungo,uchovu,kichefuchefu,kizunguzungu na wakati mwingine tumbo kuuma Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

CHADEMA WATEUA WAGOMBEA MAJIMBO YA SIHA NA KINONDONI

Image
Kamati Kuu ya Chama imemaliza Vikao vyake Leo Januari 19 imefanya uamuzi wa kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha unaotarajiwa kufanyika   Februari 19 mwaka huu. Baada ya uamuzi huu kufanyika,Kamati Kuu imewateua wagombea wa Majimbo hayo ambapo Mhe.Salum Mwalim Juma ameteuliwa kugombea jimbo la Kinondoni huku Bw. Elvis Christopher Mosi akiteuliwa kugombe jimbo la Siha. Kwa mjibu wa John Mrema ambaye ni Mkurugenzi wa Itikadi,Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, Wagombea wote wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo husika. Wagombea hao wanatajia kurejesha fomu hizo kesho jumamosi kwa ajili ya uteuzi. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED  

WAFANYABIASHARA MANISPAA YA MPANDA WAANDAMANA MPAKA KITUO CHA RADIO KUMPINGA MKURUGENZI WA MANISPAA

Image
Mmoja wa wafanyabiashara akizungumza kueleza kero(PICHA NA.Issack Gerald) Wafanyaboiashara wakiwa wamkusanyika ndani na nje ya uzio wa studio za Mpanda Radio(PICHA NA.Issack Gerald) Baadhi ya wafanyabiasahara wakizungumza na Mpanda Radio na kueleza kero zao(PICHA NA.Issack Gerald) Mamia ya wafanyabiasahara wadogo wadogo  katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameandamana mpaka katika kituo cha matangazo mpanda radio wakipinga agizo la mkurugenzi wa Manispaa hiyo Michael Nzyugu  kuyafunga masoko yasiyo rasmi. Wakizungumza na Mpanda radio mapema leo wamesema , kitendo hicho hakikubaliki kwani mpaka sasa serikali haijaandaa maeneo mbadala ya kufanyia biashara hizo. Miongoni mwao wamesikika wakisema maeneo mengi wanayo takiwa kwenda mara baada ya kuyahama maeneo yasiyo rasimi yanakabiliwa na miundombinu dhaifu ikiwemo na mlundikano wa wajasiliamali. Wiki iliyopita Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu  ameutangazia umma kuwa ifikapo tarehe 22 mwezi h