WAMILIKI WAMABASI WAHITAJI KUKUTANA NA RAIS MAGUFULI



Wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani,wameomba kukutana na Rais John Magufuli kumweleza matatizo yanayowakabili ikiwamo  vipengele wanavyodai kuwa ni kandamizi katika kanuni mpya za leseni za usafirishaji.

Wamefikia hatua  hiyo baada ya kutofikia muafaka katika kikao kilichofanyika jana  jijini Dar es Salaam kati yao  na maofisa kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa  Usafiri wa Nchi kavu na Majini (Sumatra),Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, na Jeshi la  Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani.
Akitangaza azimio hilo kwa niaba ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo,Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi hayo (Taboa),Enea Mrutu,alisema wataandika barua kuomba kukutana na Rais  Magufuli ili kumweleza matatizo yanayowasibu.
Hata hivyo,Mwenyekiti wa Taboa,Mohammed Hood alisema kabla ya kuandikia barua ya kuomba kukutana na Rais, watafanya utaratibu wa kuonana na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Barabara,Johansen Kahatano,alisema hakuna uadui kati ya Sumatra na wamiliki wa mabasi na kwamba suala la faini inayotozwa kuanzia Sh. 250,000 hadi 500,000  na haliwezi kuingiliwa kwa sasa kwa sababu ni la  kisheria.
Aidha Kahatano aliwataka Taboa kwenda Tume ya Ushindani kulalamika endapo wanaona kanuni au sheria hizo mpya zinawakandamiza.
Kuhusu  kuzuia gari kwa kosa la  dereva,Kahatano alisema sheria ya Sumatra inasema endapo gari litakamatwa, mmiliki wa gari atapewa siku 14 za kulipa faini hiyo na endapo siku hizo zikipita bila kulipa,mmiliki anaweza kufika Polisi au Sumatra na kutaka kesi iende mahakamani.
Alisema hakuna gari lolote litakalozuiwa kwa kosa alilofanya dereva na kwamba makosa ya dereva na mmiliki yametenganishwa.
Wakichangia katika mkutano huo,wajumbe wa Taboa wengi wao  walilamikia kanuni zilizokuwapo katika leseni za usafirishaji kuwa zinawakandamiza huku wakipendekeza faini za viwango vipitiwe upya pamoja na makosa ya dereva na mmiliki yatenganishwe
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA