WATOTO 400 WAKOSA ELIMU WILAYANI SUMBAWANGA

JUMLA ya watoto wa wavuvi wapatao 400 waliopo katika kambi ya wavuvi ya Nankanga wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa ambao wamefikia umri wa kuanza darasa la kwanza wameshindwa kupata haki yao ya elimu kutokana na kutokuwa shule.
Diwani wa kata ya Nankanga wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, Anyisile Kayuni alimwambia hayo mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo wakati akiwa katika ziara ya kukagua makambi ya wavuvi katika suala la kukabiliana na ugonjwa wa kipindu pindu.
Alisema kuwa watoto hao wanaishi na wazazi wao katika kambi hiyo ya Nankanga iliyopo katika kijiji cha Nankanga,kata ya Nankanga na wamefikia umri wa kuanza shule ya msingi lakini wameshindwa kutokana na kuwa katika eneo walilopo hakuna shule.
Diwani huyo alisema kuwa shule ya msingi ipo umbali wa kilomita tisa kutoka yalipo makambi hayo umbali ambao ni mkubwa huku ukikabiliwa na changamoto ya barabara kitendo kinachosababisha washindwe kwenda shule.
alisema kuwa kwa kuliona hilo yeye kupitia uongizi wa makambi hayo walikubaliana kujenga shule ambapo mbapa sasa wamejenga vyumba viwili vya madarasa na kufikisha usawa wa lenta ambapo wanaiomba serikali ya mkoa iwasaidie bati 100 wapaue vyumba hivyo na kuwapelekea walimu ili watoto hao waanze kusoma.
Alisema kuwa katika kambi hiyo wavuvi waliopo wanajitahidi kuzingatia huduma za afya bora ikiwamo ni pamoja na kuchimba vyoo, pia wanapata huduma za dawa za kufubaza virusi vya ukimwi ambapo wapo watu 270 wanaotumia dawa hizo na wameweka mkakati kuhakikisha kuwa hawaachi kutumia ili waishi maisha yenye afya na marefu.
Kwaupande wake mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alifurahishwa na hatua ya wananchi hao kuanzisha suala la ujenzi wa shule ili watoto hao wapate elimu ambapo aliahidi ofisi yake itatoa bati 50 na aliigiza halmashauri ya wilaya hiyo kutoa bati nyingine 50 ili vyumba hivyo vya madarasa vipauliwe na watoto hao waanze  shule mara moja.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA