WILAYA YA TANGANYIKA YAPIGA HATUA KIMAENDELEO KWA MIEZI 6



Na.Issack Gerald
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Salehe Muhando,amesema wilaya hiyo imepiga hatua za kimaendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu,afya,kilimo,umeme,Maji na miundombinu ya barabara katika kipindi cha mwezi Julai mpaka Desemba 2017.
Muhando amebainisha hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezwaji wa miradi ya maendeleo wilayani humo ikiwa ni kutekelezwa kwa ilani ya chama cha Mapinduzi CCM katika kipindi cha mwezi Julai mpaka Desemba mwaka jana.
Pamoja na mambo mengine amesema hatua mbalimbali ya uchimbaji visima 21 vitakavyokamilika mwaka huu unaendelea kama hatua ya kutatua tatizo la maji linalowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali ya vijiji vya wilaya hiyo.
Katika sekta ya nishati,Muhando amesema Usambazaji wa umeme kwa vijiji vyote 43 vilivyoainishwa utaendelea huku Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amesema,waanatarajia kufungua barabara kutoka kiji cha St.Maria—Kabage,Vikonge—Bugwe,Isengure-Bujombe,Kona Ikaka—Mnyagala na kutoka Mishambo kuelekea Ziwani Tanganyika.
Katika sekta ya Afya Muhando amesema,mpaka kufikia mwezi Aprili Mwaka huu ujenzi wa kituo cha Afya Cha Mishambo kitakuwa kimekamilishwa kuwa katika kiwango cha Hospitali huku juhudi nyingine kama hizo zikielekezwa katika Kituo cha Afya Mwese.
Kwa mwaka wa fedha ujao wa 2018/2019 vituo vya afya vinatarajia kujengwa kijiji cha Kasekese kitakchohudumia pia Sibwesa huku UJenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mnyagala na kituo cha afya kitakachohudumia kata za kitakachohudumia kata za Ilangu na Ipwaga navyo vikitarajiewa kujengwa kwa kasi ili kusogeza huduma kwa wananchi.
Aidha katika kuongeza ajira kwa vijana,wanawake na Wakazi wa Tanganyika kwa ujumla,wilaya hiyo inatarajia kujenga viwanda 7 vikiwemo viwanda vya kutengeneza chaki,kiwanda cha kufyatua tofali,kiwanda cha kusindika alizeti,kiwanda cha kuzalisha sabuni na kiwanda cha kuzalisha Blanketi na taulo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM wilayani Tanganyika Bw.Yasini Mohamed Kibiriti pamoja na ambo mengine amesisitiza viongozi wa chama na serikali kushirikiana kwa pamoja ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango kazi.
Utekelezwaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM ni matokeo ya kupata viongozi wa chama wanaoisimamia ilani na serikali ambapo viongozi wa kichama katika Wilaya ya Tanganyika walipatiakana hivi karibuni ambapo kwa upande wake Katibu wa CCM wilayani Tanganyika Warid Mngumi ametoa pongezi kwa wote waliochaguliwa katika chaguzi zilizopita.
Akizungumza kwa niaba ya mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Bw.Hamad Mapengo,Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bi.Theodora Romward Kisesa amesema baadhi ya changamoto zilizoibuliwa na zilizokuwa zimeshaibuliwa zote wamezipokea tayari kwa kuanza kuzifanyia kazi.
Kikao hicho maalumu ambacho kimefanyika katika ukumbi wa chama cha Mapinduzi CCM wilayani Mpanda,kimwashirikisha viongozi wa kichama na serikali wilaya ya Tanganyika.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA