Posts

Showing posts from October 30, 2017

UHURU KENYATA NA URAIS MWAKA 2017

Image
Rais Uhuru Kenyatta ametangazwa mshindi wa urais wa marudio nchini Kenya akiwa na kura 7,483,895 sawa na 98%. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC Wafula Chebukati amesema kiongozi wa upinzani Raila odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa na asilimia 0.96. Bw Chebukati amesema jumla ya wapiga kura 7,616,217 kati ya jumla ya wapiga kura 19.6 milioni ambao wamejiandikisha kuwa wapiga kura nchini humo walishiriki uchaguzi huo wa Alhamisi wiki iliyopita. Hiyo ni asilimia 38.84. Rais Kenyatta, akihutubu baada ya kutangazwa mshindi, amewashukuru waliompigia kura. Amesema uchaguzi uliomalizika ni ishara ya uthabiti wa demokrasia na uthabiti wa taasisi za Kenya pamoja na Wakenya wenyewe. "Agosti 8, na sitachoka, Wakenya walirauka kupiga kura. Na siku hiyo walinichagua bila shaka. Ushindi wangu ulipopingwa Mahakama ya Juu, kwenye hukumu, mahakama haikupinga ushindi wangu wa 54%. Takwimu hazikupingwa. Kilichokosolewa ni utaratibu uliopelekea ushindi wangu,&quo

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA

Image
Lazaro Nyalandu alizaliwa Agosti 18, 1970 mkoani Singida, hivyo atafikisha miaka 45 Agosti mwaka huu. Kwa sasa yeye ni Waziri wa Maliasili na Utalii. Historia yake Lazaro Nyalandu alizaliwa Agosti 18, 1970 mkoani Singida. Nyalandu alipata elimu ya msingi katika shule za Pohama na Mrumba zilizoko kijijini kwao huko mkoani Singida na kuhitimu mwaka 1987. Aliendelea na masomo ya kidato cha kwanza mpaka cha nne katika Shule ya Sekondari Kibaha mkoani Pwani (1988 –1991) na alifaulu vizuri na kujiunga na Shule ya Sekondari Ilboru ambako alisoma kidato cha tano na sita. Wakati akiwa mwanafunzi wa sekondari,Nyalandu alikuwa kiongozi wa juu wa Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania(Ukwata) 1991–1993 na baadaye alikuwa miongoni mwa vijana wa Kitanzania walioteuliwa kuzuru jiji la Rio De Janeiro,Brazil na kushuhudia mkutano wa Mazingira mwaka 1993. Nyalandu alipata elimu yake ya Chuo Kikuu nchini Marekani ambako alihitimu Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Usimamizi wa Biashar

ZITTO AMEMPONGEZA NYALANDU KUJIUDHURU NDANI YA CCM NA KUACHA UBUNGE

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo),Zitto Kabwe amempongeza Mbunge wa Singida Kaskazini(CCM), Lazaro Nyalandu kuwa ameonyesha uongozi uliokomaa. Zitto ametoa maoni yake hayo baada ya Nyalandu kuamua kujiondoa CCM na kuachia nafasi yake ya ubunge. Zitto ameandika, "Lazaro Nyalandu,umeonyesha uongozi. Kwa namna haki za watu zinavyovunjwa na uchumi wa nchi unavyoporomoka, unahitaji roho ngumu sana kuwa CCM.Umefanya maamuzi sahihi,wakati sahihi na kwa sababu sahihi. Kila la kheri." Lazaro Nyalandu leo ametangaza kujivua nafasi zake ndani ya Chama Cha Mapinduzi na kuandika barua yake ya kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kwa kile alichodai kuwa Chama Cha Mapinduzi na Bunge vimekuwa vikishindwa kuisimamia serikali na badala yake kutumiwa na serikali jambo ambalo yeye anaona halina afya katika maendeleo ya nchi na linadidimiza haki mbalimbali.  Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  au ukurasa P5Tanzania Limited

WANAFUNZI KIDATO CHA NNE KATAVI WAMESEMA WATAFAULU MTIHANI

Image
Na.Issack Gerald-Katavi Baadhi ya watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne katika shule mbalimbali za manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameeleza matumaini ya kufaulu mtihani wao ulioanza leo nchi nzima. Wakizungumza kwa nyakati tofauti,wanafunzi hao wakiwemo wa shule ya sekondari Mwangaza na Kashaulili wamesema maandalizi yao katika mtihani huo yako vizuri huku wakiwaomba wenzao kuondoa hofu ya mtihani. Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Mwangaza Mwl.Simoni Lubange amewataka wanafunzi wake kujiamini na kumtanguliza mungu katika ujibuji wa mitihani yao kwa alichokisema hakuna kitu kigeni watakachokutana nacho. Jumla ya watahiniwa 385,938 wa kidato cha nne nchini wameanza mtihani leo huku baraza la mitihani likitoa onyo kwa na tahadhari kwa wamiliki wa shule watakaofanya udanganyifu. Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  au ukurasa P5Tanzania Limited

SERIKALI KUFUNGUA UTALII KANDA YA KUSINI

Image
Na.Issack Gerald-Rukwa Serikali imesema imedhamiria kufungua utalii wa Kanda ya Kusini ili kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini na hatimaye kuongeza idadi ya watalii na kipato kwa Serikali na jamii kwa ujumla. Hatua hiyo imeelezwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga katika kijiji cha Kapozwa Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa,wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea Maporomoko ya Mto Kalambo ambayo ni ya pili kwa kina kirefu barani Afrika. Amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo benki ya Dunia kupitia mradi wa REGROW imepanga kuboresha miundombinu ya vivutio vya utalii vya Kanda ya Kusini na kuvitangaza,ili kuimarisha sekta hiyo muhimu ambayo inachangia asilimia 25 ya mapato yote ya kigeni na asilimia 17.5 ya pato la taifa. Aidha,ametoa wito kwa wananchi wa kijiji cha Kapozwa wanaoishi jirani na hifadhi kushirikiana na Serikali katika uhifadhi wa uoto wa asili pamoja na kudumisha tamaduni zao. Vivutio vingine ni p

WATU WENYE ULEMAVU MKOANI KATAVI WARIDHISHWA NA HATUA ZA SERIKALI KATIKA KUWAKWAMUA NA UMASKINI

Na.Issack Gerald-Katavi WATU wenye ulemavu Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamesema wameridhika na hatua zinazochukuliwa na Manispaa ya Mpanda katika kushughulikia mahitaji yao ikiwemo suala la mikopo. Hayo yamebainishwa leo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika shule ya msingi Azimio ukihusisha watu wenye ulemavu na wataalamu wa idara ya maendeleo ya mjamii Manispaa ya Mpanda kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kupata mikopo na uundaji vikundi vya kijasiliamali. Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Mpanda Linus Kalindo pamoja na mambo mengine amewataka watu wenye ulemavu kutoona ulemavu ni mwisho wa maisha na badala yake waendelee kufuata nmna wanayoelekezwa ili wapatiwe mikopo. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya watu wenye Ulemavu SHIVYAWATA Mkoani Katavi Issack Mlela amesema watazingatia yote wanayoshauriwa na wataalamu ikiwemo kuunda vikundi,kusajili vikundi na hatimaye kupatiwa mikopo. Hii ni mara ya pili katika kipindi cha mwezi huu w