UHURU KENYATA NA URAIS MWAKA 2017

Rais Uhuru Kenyatta ametangazwa mshindi wa urais wa marudio nchini Kenya akiwa na kura 7,483,895 sawa na 98%.
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC Wafula Chebukati amesema kiongozi wa upinzani Raila odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa na asilimia 0.96.
Bw Chebukati amesema jumla ya wapiga kura 7,616,217 kati ya jumla ya wapiga kura 19.6 milioni ambao wamejiandikisha kuwa wapiga kura nchini humo walishiriki uchaguzi huo wa Alhamisi wiki iliyopita.
Hiyo ni asilimia 38.84.
Rais Kenyatta, akihutubu baada ya kutangazwa mshindi, amewashukuru waliompigia kura.
Amesema uchaguzi uliomalizika ni ishara ya uthabiti wa demokrasia na uthabiti wa taasisi za Kenya pamoja na Wakenya wenyewe.
"Agosti 8, na sitachoka, Wakenya walirauka kupiga kura. Na siku hiyo walinichagua bila shaka. Ushindi wangu ulipopingwa Mahakama ya Juu, kwenye hukumu, mahakama haikupinga ushindi wangu wa 54%. Takwimu hazikupingwa. Kilichokosolewa ni utaratibu uliopelekea ushindi wangu," amesema.
Bw Odinga alikuwa ametarajiwa kutangaza mwelekeo kwa wafuasi wake baada ya tangazo la matokeo kufanywa na Bw Chebukati.
Taarifa zinasema ameamua kufanya hivyo hapo kesho.
Matokeo kamili ya wagombea wote kama yalivyotangazwa na Bw Chebukati
Mgombea
Chama
Kura
Asilimia
Uhuru Kenyatta
Jubilee
7,483,895
98.28
Raila Odinga (Alisusia)
ODM
73,228
0.96
Mohamed Abduba Dida
ARK
14,107
0.19
Japheth Kavinga Kaluyu
Mgombea wa kujitegemea
8,261
0.11
Michael Wainaina Mwaura
Mgombea wa kujitegemea
6,007
0.08
Joseph Nthiga Nyagah
Mgombea wa kujitegemea
5,554
0.07
John Ekuru Aukot
Thirdway Alliance
21,333
0.28
Cyrus Jirongo
UDP
3,832
0.05
Bw Chebukati amesema anaamini uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.
Mwenyekiti huyo amesema mambo aliyosema yalihitajika kufanyika kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki yalitimizwa.
Amesema walitaka kuhakikisha kila kitu kilikuwa sawa.
"Hata tulibadilisha tarehe kutoka 17 hadi 26 Oktoba kuhakikisha tuna muda wa kutosha," amesema.
Kadhalika, amesema alikuwa na kundi la kusimamia mradi wa uchaguzi wa urais kuondoa majukumu kutoka kwa makamishna ambao walituhumiwa na baadhi ya wadau.
"Naweza kusema kwa uhakika, kwamba 26 Oktoba kabla ya uchaguzi kuanza, nilikuwa nimeridhika kwamba tulikuwa tumefanya kila kitu kuhakikisha kila Mkenya angetekeleza haki yake kikatiba," amesema.
"Na haki hii mtu anafaa kuitekeleza bila kutishiwa au kuzuiwa."
Bw Chebukati anasema alishangaa kwamba watu waliotafuta wa kushambulia walimwendea yeye.
Hata hivyo, anasema ndani ya tume nao walimwogopa.
"Hatutaweza kufurahisa kila mtu. Nimedumisha na kuheshimu sheria, kama mwanasheria ziwezi kuvunja sheria niliyojitolea kuilinda," amesema.

Matokeo yalivyokuwa uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ambao ulifutwa na Mahakama ya Juu

Mgombea
Chama
Kura
Asilimia
Uhuru Kenyatta
Jubilee
8,203,290
54.27
Raila Odinga
ODM
6,762,224
44.74
Mohamed Abduba Dida
ARK
38,093
0.25
Japheth Kavinga Kaluyu
Mgombea wa kujitegemea
16,482
0.08
Michael Wainaina Mwaura
Mgombea wa kujitegemea
13,257
0.09
Joseph Nthiga Nyagah
Mgombea wa kujitegemea
42,259
0.28
John Ekuru Aukot
Thirdway Alliance
27,311
0.18
Cyrus Jirongo
UDP
11,705
0.08



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA