Posts

Showing posts from March 29, 2018

MKOANI KATAVI AMUUA MKEWE NA KUZIKA MWILI WAKE

Image
Jeshi   la   Polisi mkoani Katavi   linamshikilia mkazi   wa   Kijiji   cha   Songambele   Kata ya   Sibwesa   Tarafa ya   Karema Wilaya ya   Tanganyika   jina   lake   limehifadhiwa(45) kwa   tuhuma za kumuua mke   wake(31) kwa sababu ya wivu wa kimapenzi na   kisha mzika huku   mtoto wake mwenye   umri wa miaka tisa akishuhudia tukio. Kamanda wa   Jeshi la   Polisi wa   mkoa   wa   Katavi    Damas    Nyanda     alisema tukio   la kupatikana   kwa   mwili   wa   marehemu   huyo lilitokea juzi majira ya saa 6;00 mchana   katika Kijiji   hicho. Alisema   marehemu aliuawa   na   mumewe huyo siku ya   januari 15   kwa   kupigwa na   mumewe   kwa   kutumia silaha   zajadi ambazo ni fimbo na   mpini   wa    jembe baada ya   kumtuhumu kuwa   anamahusiano wa   kimapenzi na wanaume   wengine   Kijijini   hapo. Kamanda    Nyanda alisema wakati mtuhumiwa   huyo akitenda kosa hilo    ambalo   lilishuhudiwa   na   mtoto   wake wa kiume hadi    baba   yake   alivyomuuawa   mama   yake   na

WATOTO WA KANISA KATOLIKI WATOA MSAADA KWA WAGONJWA HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA

Image
Katika kuadhimisha Alhamisi kuu kuelekea sikukuu ya pasaka,Watoto wa shirika la mtoto yesu kutoka jumuiya mtakatifu Filomena kigango cha Kawajense Majengo Mapya jimbo katoliki la Mpanda Mkoani Katavi,wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa waliopo katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda. Wakizungumza kwa niaba ya watoto wenzao Sesilia John Enock na Samweli wamesema wameamua kutoa msaada kwa wagonjwa wenye uhitaji ikiwa ni kuadhimisha Alhamisi kuu katika kuelekea sikukuu ya pasaka. Jimbo Katoliki la Mpanda Katavi(PICHA NA.Issack Gerald) Kwa upande wake Katekista Joseph Paul Kansato ambaye pia ni mwalimu wa parokia ya kanisa kuu jimbo la Mpanda amesema watoto hao wametoa misaada mbalimbali ikiwemo sabuni, mafuta na sukari kama ishara ya upendo walionao kwa watu wenye shida mbalimbali. Kwa upande wao baadhi ya wagonjwa wakiwemo Mussa Paul na Magreth Peter Ndekeja wametoa shukrani zao kwa watoto hao waliotoa msaada huo huku wakiomba jamii kuiga mfano uliooneshwa na wato