Posts

Showing posts from February 11, 2018

ANC CHAADHIMISHA MIAKA 100 YA KUZALIWA KWA NELSON MANDELA

Image
Chama tawala cha Africa Kusini ANC kimeanza maadhimisho ya kumbukumbu za miaka mia moja tangu kuzaliwa kwa Raisi wa kwanza mweusi nchini humo shujaa Nelson mandela. Nelson Mandela Kiongozi wa sasa wa ANC ,Cyril Ramaphosa anatarajiwa kutoa hotuba huko medani mwa Freedom square mjini Cape Town, ambako marehemu Mandela alitoa hotuba yake ya kwanza alipoachilia huru kutoka gerezani miaka ishirini na nane iliyopita.

DR. SHEIN AAGIZA WIZARA YA ELIMU KULIPA MADENI YOTE YA WALIMU KABLA 2019

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein amesema sera ya elimu bure  kwa wanafunzi wa sekondari itaanza ifikapo  mwezi june  mwaka huu. Akizungumza  katika Mkutano Mkuu wa Sita wa chama cha walimu Zanzibar zatu amesema serikali imeamua  kuondoa ada  kwa wanafunzi  kwa lengo la kuendeleza sera ya rais wa awamu ya kwanza Shekh Abeid Amani Karume.