Posts

Showing posts from October 18, 2017

MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI KENYA AMEWALAUMU WANASIASA

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati amewashutumu wanasiasa nchini humo akisema wanatatiza maandalizi ya uchaguzi wa marudio Alhamisi wiki ijayo.

FAHAMU MAISHA YA DKT ROSELYN WA TUME YA UCHAGUZI ALIYEJIUDHURU NCHINI KENYA

Image
Dkt Roselyn Akombe Kwamboka alizaliwa 1976 katika kaunti ya Nyamira , na kusomea katika chuo kikuu cha Nairobi kabla ya kuelekea nchini Marekani kwa masomo zaidi. Anamiliki shahada ya uzamifu katika maswala ya sayansi na kimataifa mbali na shahada nyengine kama hiyo katika somo hilo kutoka chuo kikuu cha Rutgers . Hadi uteuzi wake katika tume hiyo alifanya kazi kama katibu katika Umoja wa Mataifa mjini New York, wadhfa ambao anasema ulimwezesha kuwa na uzoefu katika maswala ya uchaguzi duniani. Uwezo wake mkuu alisema mbele ya kamati ya bunge nchini Kenya , ni kutatua migogoro na kwamba ameishi ng'ambo kwa takriban miaka 15, hatua iliomwezesha kuelewa zaidi mahitaji ya watu wanaoshi ughaibuni wakati wa uchaguzi. Kwamboka alielezea kwamba alichukua uamuzi huo kama Mkenya mzalendo aliyetaka kulihudumia taifa lake. Alichukua likizo katika Umoja wa Mataifa hatua inayomaanisha kwamba hatopokea hata shilingi kutoka Umoja wa mataifa wakati ambapo amekuwa akiifanyia kazi IEBC.

WATU WA TUME YA UCHAGUZI NCHINI KENYA WAANZA KUNG’ATUKA MADARAKANI

Image
Mmoja wa maafisa wakuu wa Tume ya Uchaguzi Kenya (IEBC) Dkt. Roselyn Akombe ametangaza kujiuzulu katika tume hiyo chini ya wiki moja kabla ya uchaguzi mpya wa urais kufanyika nchini humo. Dkt Akombe ametuma taarifa kutoka mjini New York anakoishi ambapo alikuwa akiufanyia kazi Umoja wa Mataifa kabla ya kujiunga na tume ya IEBC. Katika taarifa, Dkt Akombe alisema kuwa merejeleo ya uchaguzi utakaofanyika hayaafikii matarajio ya uchaguzi ulio huru na wa haki. Dkt Akombe alitarajiwa kuwa miongoni mwa kundi la maafisa waliokwenda Dubai kuchunguza uchapishaji wa makaratasi ya kupigia kura. Dkt Akombe alizuru Nyanza na maeneo ya Magharibi, ambayo ni ngome ya upinzani, wiki iliopita huku tume hiyo ikijaribu kuwafunza maafisa watakaosimamia uchaguzi huo.

HAYA MAMBO YA USALAMA WA TANZANIA NA WATU WAKE YANAHITAJI ZAIDI YA TAFAKARI

Image
Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe amesema gharama za matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya zimefikia Sh412.7 milioni.

MADIWANI WANAOTUHUMIWA KUNUNULIWA NA CCM WAHOJIWA NA TAKUKURU

Image
Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam, wamewahoji kwa zaidi ya saa sita,madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki,Joshua Nassari kuwa walipewa rushwa.