Posts

Showing posts from October 23, 2017

RAIS MAGUFULI AMETEUA GAVANA MPYA WA BENKI KUU YA TANZANIA(BOT) PIA ANGALIA ORODHA YA WAJUMBE WALIOPATA TUZO SUALA LA MAKINIKIA

Image
Na.Issack Gerald Prof.Frorens Luoga Gavana Mpya BOT Rais John Magufuli amemteua Profesa Florens Luoga kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) kuchukua nafasi ya Profesa Benno Ndullu anayemaliza muda wake. Rais Magufuli ametangaza uteuzi huo leo akiwa Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kutoa vyeti kwa kamati zilizohusika na ripoti za madini nchini. Akizungumza baada ya kutoa vyeti hivyo amesema atamteua gavana kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya mashauriano kuhusu madini kutokana na kuridhishwa na kazi yao. Gavana Beno Ndullu,ambaye amekuwa Gavana wa BOT tangu 2008 anamaliza muda wake ifikapo mwezi Januari mwakani. Huo ni uteuzi wa pili kwa Profesa Luoga,kwani Julai 11 mwaka huu Rais Magufuli alimteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA). Profesa Luoga alichukua nafasi ya Bernard Mchomvu ambaye bodi yake ilivunjwa na uteuzi wake kutenguliwa. ORODHA WALIOTUNUKIWA VYETI 1.Jobu Yusto Ndugai(Spika wa Bu

WAZIRI LUKUVI AFAFANUA ZAIDI KUHUSU BOMOABOMOA NCHINI

Image
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameyasema hayo ametoa ufafanuzi kuhusu uwekaji wa alama za X na kuvunja majengo yanayojengwa katika miji bila kibali. Waziri Lukuvi ametoa ufafanuzi huo leo ikulu wakati rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwatunuku vyeti wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa kiwango aina na thamani ya madini katika makinikia. Amesema zoezi hilo litakuwa sambamba na kuwaondoa wavamizi katika viwanja vya watu waliowadhulumu watu wengine walio na hati miliki za ardhi na kujenga nyumba zao. Aidha Lukuvi amesema viongozi wote wa wilaya na mitaa wahamasishe wananchi kushiriki kikamilifu katika urasimishaji wa makazi yao kwa faida yao na Taifa kwa jumla. Waziri Lukuvi alitoa agizo hilo jana Oktoba 22 2017 ambapo aliwaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri,Maafisa Ardhi,Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuweka alama za X na kuvunja majengo yote yanayojengwa katika miji yao bila kibali na yale yanayojengwa katika viwanja vya

MKAZI MMOJA MKOANI KATAVI AMENUSURIKA KUUWAWA USIKU WA KUAMKIA LEO

Image
Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la James Modest mkazi wa Kijiji cha Mnyaki A kata ya Katumba Wilayani Mpanda  amenusurika kuuwawa baada ya watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kuvamia nyumbani kwake  usiku wa kuamkia leo. Kwa mjibu wa James Modest ambaye ni Mhanga wa tukio hilo amesema ameporwa fedha taslimu shilingi 730,000 vifaa vya sola za umeme vyenye thamani ya shilingi 70,000. Aidha amesema ndani waliingia watu watatu na kuanza kumshambulia kwa vitu vizito ambapo walichukua kiasi hicho cha fedha na kumuamru awakabidhi simu ya Smartphone yenye thamani ya 220,000 pamoja,simu ndogo yenye thamani ya shilingi 40000. Shuhuda wa tukio hilo Yadunia Modest ambaye pia ni kaka wa aliyejeruhiwa na kuporwa mali zake,amesema mdogo wake amekatwakatwa kwa mapanga na kujeruhiwa puani na kichwani hali ambayo imemsababishia maumivu makali. Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyaki A Bw.Kisele Meshack amethibitisha tukio hilo na kusema kuwa tukipo hilo limetokea usiku

WAKAZI WAANGUA KILIO BOMOABOMOA MKOANI TABORA

Image
Serikali Mkoani Tabora Kwa Kushirikiana Na Halmashauri Ya  Manispaa Ya Tabora Imeendesha Zoezi La Bomoa Bomoa Kwenye Nyumba Zaidi Ya 60 Zilizojengwa Kinyume Cha Sheria Katika Maeneo Ya Shule Ya Sekondari Tabora Wasichana. Zoezi hilo limeibua Vilio,Majonzi Na Simanzi Miongoni Mwa Wananchi Waliobomolewa Nyumba Zao Huku Wengine Wakipoteza Fahamu Katika Kata Ya Ng’ambo Mjini Tabora. Zoezi La Kubomoa Nyumba Hizo Limefanyika Chini Ya Ulinzi Mkali Wa Askari Polisi Na askari mgambo. Wakizungumza Kwa Majonzi Baadhi Ya Wanachi wameiomba serikali kuwatizama kwa jicho la huruma. Baadhi ya maafisa Wa Serikali ambao wamesimamia zoezi La Kubomoa Nyumba Wamewatahadharisha Wananchi Kuacha Tabia Ya Kujenga Bila Kupata Kibali. Zaidi ya kaya sitini hazina makazi huku wananchi wakiwa hawajui hatima yao. Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  au ukurasa P5Tanzania Limited

UCHAGUZI MWENYEKITI HALMASHAULI YA BUHIGWE MIZENGWE MITUPU-HALMASHAURI IMEZUNGUMZA

Image
Baraza la madiwani wilayani Buhigwe mkoani kigoma, limeshindwa kumchagua mwenyekiti wa halmashauri hiyo, baada ya kikao kilichotakiwa kufanyika kwa ajili ya kumchaguwa mwenyekiti  kuahirishwa kutokana na kutokuzingatiwa kwa taratibu za uchaguzi.

WAJUMBE SAKATA LA MAKINIKIA KUIBUKA NA TUZO LEO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli leo anatarajia kuwatunuku vyeti wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa kiwango, aina na thamani ya madini katika makinikia na baadaye kufanya mazungumzo na kampuni ya Barrick Gold. Tanzania na Barrick Gold Corporation zilifikia makubaliano Oktoba 19 mwaka huu na kutiliana saini mkataba wa kutekeleza mwelekeo mpya wa namna kampuni hiyo itakavyoendesha biashara ya madini ya dhahabu yanayochimbwa katika migodi yake hapa nchini,. Aidha kutiliana saini huko kumekwenda sambamba na na kulipa Dola za Marekani Milioni 300 za kuonesha nia njema ya kufidia madai ya upotevu wa mapato yaliyotokana na biashara hiyo. Tukio hilo linalotarajiwa kufanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 5:00 asubuhi linatarajiwa kurushwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya redio, televisheni na mitandao mbalimbali.   Habari zaidi ni  www.p5tanzania.blogspot.com  au ukurasa P5Tanzania Limited