WAKAZI WAANGUA KILIO BOMOABOMOA MKOANI TABORA

Serikali Mkoani Tabora Kwa Kushirikiana Na Halmashauri Ya  Manispaa Ya Tabora Imeendesha Zoezi La Bomoa Bomoa Kwenye Nyumba Zaidi Ya 60 Zilizojengwa Kinyume Cha Sheria Katika Maeneo Ya Shule Ya Sekondari Tabora Wasichana.
Zoezi hilo limeibua Vilio,Majonzi Na Simanzi Miongoni Mwa Wananchi Waliobomolewa Nyumba Zao Huku Wengine Wakipoteza Fahamu Katika Kata Ya Ng’ambo Mjini Tabora.
Zoezi La Kubomoa Nyumba Hizo Limefanyika Chini Ya Ulinzi Mkali Wa Askari Polisi Na askari mgambo.
Wakizungumza Kwa Majonzi Baadhi Ya Wanachi wameiomba serikali kuwatizama kwa jicho la huruma.
Baadhi ya maafisa Wa Serikali ambao wamesimamia zoezi La Kubomoa Nyumba Wamewatahadharisha Wananchi Kuacha Tabia Ya Kujenga Bila Kupata Kibali.

Zaidi ya kaya sitini hazina makazi huku wananchi wakiwa hawajui hatima yao.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA