MKAZI MMOJA MKOANI KATAVI AMENUSURIKA KUUWAWA USIKU WA KUAMKIA LEO

Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi
Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la James Modest mkazi wa Kijiji cha Mnyaki A kata ya Katumba Wilayani Mpanda  amenusurika kuuwawa baada ya watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kuvamia nyumbani kwake  usiku wa kuamkia leo.
Kwa mjibu wa James Modest ambaye ni Mhanga wa tukio hilo amesema ameporwa fedha taslimu shilingi 730,000 vifaa vya sola za umeme vyenye thamani ya shilingi 70,000.
Aidha amesema ndani waliingia watu watatu na kuanza kumshambulia kwa vitu vizito ambapo walichukua kiasi hicho cha fedha na kumuamru awakabidhi simu ya Smartphone yenye thamani ya 220,000 pamoja,simu ndogo yenye thamani ya shilingi 40000.
Shuhuda wa tukio hilo Yadunia Modest ambaye pia ni kaka wa aliyejeruhiwa na kuporwa mali zake,amesema mdogo wake amekatwakatwa kwa mapanga na kujeruhiwa puani na kichwani hali ambayo imemsababishia maumivu makali.
Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyaki A Bw.Kisele Meshack amethibitisha tukio hilo na kusema kuwa tukipo hilo limetokea usiku wa kuamka leo,majira ya saa 7 ambapo amesema majeruhi alipatiwa matibabu katika kituo cha afya Katumba na kuruhusiwa.
Tukio hilo linatajwa kuwa miongoni mwa matukio manne ya kutoka katika kijiji cha Mnyaki kata ya Katumba ambapo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Oktoba mwaka huu hakuna mauaji yaliyotokea bali uporaji wa mali na watu kujeruhiwa.
Kwa takribani wiki mbili zilizopita,kumekuwa na mfululizo wa watu kuvamiwa majumbani na kuibiwa mali ikiwemo wengine kuuwawa.
Miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na tukio lililotokea Oktoba 12 mwaka huu ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jila la Suzani Chales (40) mkaazi wa Kata ya Katuma wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi alikufa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA