Posts

Showing posts from October 27, 2017

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA VIONGOZI WAPYA NGAZI YA WIZARA NA MIKOA,ABADILISHA WAKUU WA MIKOA GHAFLA

Image
Na.Issack Gerald-Dar es Salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Wakuu wapya,Naibu Makatibu Wakuu wapya na Wakuu wa Mikoa wapya sita. Rais Mgaufuli mara baada ya kuwaapisha walioteuliwa ,amewaagiza walioapishwa kutatua matatizo ya wananchi kwa wakati bila kusubiri kusukumwa. Katika hatua nyingine,rais Magufuli amefanya mabadiliko ya ghafla akiwa ikulu wakati akiwaapisha walioteuliwa,ambapo Bi. Christine Solomon Mndeme aliyetakiwa kuwa mkuu wa Dodoma atakuwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma. Aidha aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Binilith Mahenge,ameteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa wa Dodoma akichukua nafasi ya Christine Solomon Mndeme aliyetakiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Wakati huo huo Rais Magufuli amesema shilingi bilioni 147 alizoidhinisha kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu,zitolewe kama inavyotakiwa kwa wakati na pia kwa wanafunzi wenye sifa. Habari  zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukura

RC KATAVI:UJENZI WA ZAHANATI YA KAKESE UKAMILIKE KABLA YA DESEMBA MOSI MWAKA HUU

Image
Na.Issack Gerald-Katavi MKUU wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya muhuga,ameagiza ujenzi wa wadi ya wazazi katika zahanati ya kata ya Kakese kukamilika kabla ya Desemba Mosi mwaka huu.

CWT NSIMBO WAMEFANYA UCHAGUZI WAWAKILISHI MAHALA PA KAZI,NAFASI YA WENYE ULEMAVU KAMA KAWAIDA

Na.Issack Gerald-Katavi WALIMU wanne akiwemo Onorine Boniface mwakilishi wa walimu wenye ulemavu katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoani Katavi,wamechaguliwa kuwakilisha walimu wenzao katika chama CWT ndani ya halmashauri hiyo wakitoka katika shule wanazofundisha.

HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA IMEFUNGUA SEMINA YA USINDIKAJI SAMAKI.

Image
Na.Issack Gerald-Tanganyika IDARA ya uvuvi Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi imezindua mafunzo ya siku kumi ya uvuvi,uchakataji na usindikaji wa mazao ya samaki.

MAJOPKOFU YA KUHIFADHIA MAITI MKOANI RUKWA ZAIDI YA WEZI HAYAFANYI KAZI.

MAJOKOFU ya chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Rukwa yameharibiribika kwa zaidi ya mwezi mmoja mpaka sasa. 

WALIMU WANAUSUBIRI MWEZI NOVEMBA KWA HAMU, MADARAJA, MISHAHARA NA MENGINE KEDEKEDE

Na.Issack Gerald-Nsimbo SERIKALI inatarajia kuanza kulipa madeni,kuajiri na kupandisha madaraja kwa walimu kuanzia mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu.

RAIS MAGUFULI KUWAAPISHA VIONGOZI 54 WA WIZARA NA MIKOA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo mchana anatarajia kuwaapisha Makatibu Wakuu wapya, Naibu Makatibu Wakuu wapya na Wakuu wa Mikoa wapya baada ya jana kufanya mabadiliko katika safu ya uongozi wa nyadhifa hizo. WATEULE 1.                    Ofisi ya Rais Ikulu. ·                      Katibu Mkuu – Bw. Alphayo Kidata 2.                  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. ·                      Katibu Mkuu ( Utumishi ) – Dkt. Laurian Ndumbaro ·                      Naibu Katibu Mkuu – Dorothy Mwaluko ( ATAAPISHWA ) 3.                  Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI ). ·                      Katibu Mkuu – Mhandisi Mussa Iyombe ·                      Naibu Katibu Mkuu( Afya ) – Dkt. Zainabu Chaula ·                      Naibu Katibu Mkuu( Elimu ) – Bw. Tixon Nzunda 4.                  Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira. ·                      Katibu Mk