Posts

Showing posts from November 23, 2017

STENDI MPYA YA MABASI MPANDA KUANZA KUTUMIKA MWANZONI MWA 2018

Image
Na.Issack Gerald Mstahiki Meya wa M anispaa ya Mpanda mkoani katavi Willium Mbogo amesema stendi kuu ya mabasi ya kisasa inatarajiwa kuanza kufanya kazi mwanzoni wa mwaka 2018. Mh.Mbogo amesema hatua iliyobaki ni ujenzi wa vibanda na kukamilisha huduma ya maji na umeme. Aidha amesema stendi hiyo itakuwa na uwezo wa kuingiza mabasi 60 kwa wakati mmoja   ambapo ametoa wito kwa wamiliki wote wa mabasi kununua mabasi yanayoenda na hadhi ya stendi. Mkoa wa Katavi umefikisha miaka mitano toka kuanzishwa kwake huku ukipiga hatua kubwa ya kimaendeleo ukilinganisha na mikoa mingine michanga. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

ROBO YA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA IMETUMIA SHILINGI MIL.50 KWA VIKUNDI VYA UJASILIAMALI

Image
Na.Issack Gerald Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi,imefanikiwa kutoa mkopo shilingi milioni hamsini kwa vikundi vya wanawake na vijana katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/2018. Hayo yamebainishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bi.Halima Kitumba wakati akizungumzia  kuhusu namna Halmshauri inavyotekeleza agizo la serikali kutumia asilimia 10 ya mapato ya ndani kuwawezesha wanawake na vijana. Katika mgao wa fedha hizo jumla ya vikundi 8 vya wanawake ambavyo vimepata shilingi milioni 29,700,000 huku vikundi 6 vya vijana vikipata miluioni 20,300,000. Aidha amesema katika robo ya pili inayoanzia mwezi Oktoba mwaka huu,wanatarajia kutumia shilingi milioni 50 kwa vikundi 19 ambapo mpaka sasa wametoa zaidi ya shilingi milioni 11,786,000/= zilizoelekezwa katika viwanda vidogo vidogo SIDO kwa ajili ya kununua vifaa vya uchakataji na kutoa mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali kwa wanawake na vijana waliopo Ikola n

MKOANI KATAVI DIWANI JELA MIAKA 3 KWA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA

Image
Na. Issack Gerald Mahakama ya wilaya ya Mlele imemkumu kwenda jela diwani wa kata ya Katumba Senator  Jeriti Baraka kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa. Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo Timothy Swai, mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa katavi Bahati Haule amedai mtuhumiwa alitenda kosa hilo 12.05.2016 kwa kuomba rushwa ya shilingi 500,000/=ili asimuhamishe mfugaji mmoja kwenye eneo lililozuiliwa na mahakama kuendesha shughuli za ufugaji. Taarifa iliyotolewa na  taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoani katavi imesema mtuhumiwa amehukumiwa kwa makosa mawili tofauti ambapo kosa la kwanza ni kuomba rushwa na kosa la pili ni kupokea rushwa. Taarifa hiyo inaeleza kuwa kosa la kuomba rushwa mtuhumiwa amehukumiwa kutoa faini ya shilingi 500,000/= au kifungo cha miaka mitatu na kosa la kupokea rushwa mtuhumiwa amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela bila faini. Katika taaifa ya Takukuru inaeleza kuwa baada ya t

WAKAZI MKOANI KATAVI WAMESHAULIWA KUJIUNGA NA ASASI MBALIMBALI

Wananchi mkoani Katavi wameshauriwa kujiunga na asasi mbalimbali za kimaendeleo ili kujikwamua kiuchumi. Wito huo umetolewa na Emiliana Stanslaus, mkufunzi wa asasi isiyo ya kiserikali ya Tanzania Girl Guides Association wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya You Report kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali kwa njia ya ujumbe mfupi. Kwa upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoani Katavi  Bi Anna Shumbi amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ili waweze kuandaa maisha yao ya baadae kulingana na dhima ya chama ya kuwainua kiuchumi Tanzania Girl Guides Association imelenga kuwaendeleza wasichana na wanawake  katika masuala  mbalimbali ya kijamii na kiuchumi Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED