ROBO YA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA IMETUMIA SHILINGI MIL.50 KWA VIKUNDI VYA UJASILIAMALI



Na.Issack Gerald
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi,imefanikiwa kutoa mkopo shilingi milioni hamsini kwa vikundi vya wanawake na vijana katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/2018.
Hayo yamebainishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bi.Halima Kitumba wakati akizungumzia  kuhusu namna Halmshauri inavyotekeleza agizo la serikali kutumia asilimia 10 ya mapato ya ndani kuwawezesha wanawake na vijana.
Katika mgao wa fedha hizo jumla ya vikundi 8 vya wanawake ambavyo vimepata shilingi milioni 29,700,000 huku vikundi 6 vya vijana vikipata miluioni 20,300,000.
Aidha amesema katika robo ya pili inayoanzia mwezi Oktoba mwaka huu,wanatarajia kutumia shilingi milioni 50 kwa vikundi 19 ambapo mpaka sasa wametoa zaidi ya shilingi milioni 11,786,000/= zilizoelekezwa katika viwanda vidogo vidogo SIDO kwa ajili ya kununua vifaa vya uchakataji na kutoa mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali kwa wanawake na vijana waliopo Ikola na Isengule.
Ametaja miongoni mwa mafunzo yaliyofundishwa ni pamoja na namna ya kuchakata samaki na daga,kutengeneza dawa za kunguni,sabuni,batiki na vikoi,useketaji wa blanketi na masweta.
Katika mgao wa mikopo ya robo ya pili inayoanzia mwezi Oktba jumla ya vikundi vitakavyonufaika vipo 19 ambapo katika vikundi hivyo,vikundi 14 vya wanawake vitapata shilingi milioni 29,200,000 na vikundi 5 vya vijana vitapata shilingi milioni 11,600,000.
Kwa mjibu wa Bi.Kitumba mpaka sasa zaidi ya vikundi 90 vya ujasiliamali katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda vinanufaika na mikopo inayolewa na Halmshauri.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA