Posts

Showing posts from March 15, 2016

WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA WAKITUHUMIWA WIZI WA FEDHA KWA KUTUMIA SIMU

Na.Issack Gerald-Mpanda Watu wawili wakazi wa kijiji cha Ikaka   kata ya Mnyagala wilayani Mpanda mkoani Katavi,wamefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda wakikabiliwa na shtaka la wizi wa fedha kwa njia ya simu   ambayo ni mali ya Charles Lubasha mkazi wa Kakese.

WAKUU WAPYA WA MIKOA WAAPISHWA,HOTUBA YA RAIS MAGUFULI KITANZI KWAO

Image
Na.Issack Gerald Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli ametoa siku kumi na tano kwa Wakurugenzi wa halamshauri zote nchini Kufuta Majina ya Wafanyakazi hewa wanaolipwa Mishaha.                                             Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga kuwa mkuu wa mkoa wa Katavi,Hafla hiyo fupi ya kuwaapisha Wakuu hao wa Mikoa imefanyika leo Ikulu,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

WANANCHI WAIOMBA SERIKALI WILAYANI MPANDA KUSAJIRI SHULE WALIYOIANZISHA KWA AJILI YA WATOTO

Na.Vumilia Abel-Mpanda WANANCHI wa Kijiji cha Ikaka A Kata ya Ikaka Wilayani   Mpanda Mkoani Katavi wameiomba serikali   kusajiri   shule iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi pamoja na kutatua changamoto za kielimu zinazowakabili kijijini hapo.

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA UCHOMAJI NYUMBA MPANDA

Na.Mgeni Shabaani-Mpanda MTU mmoja mkazi wa tambukareli Kata ya Mpanda Hoteli Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuchoma moto nyumba na mali ya Anatalia Golikondwe mkazi wa tambuka reli.