AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA UCHOMAJI NYUMBA MPANDA


Na.Mgeni Shabaani-Mpanda
MTU mmoja mkazi wa tambukareli Kata ya Mpanda Hoteli Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuchoma moto nyumba na mali ya Anatalia Golikondwe mkazi wa tambuka reli.

Akisoma shitaka hilo mbele  hakimu mwandamizi  Bw. David |Mbembela,askari wa jeshi la polisi Bi.Elineema amemtaja mshtakiwa huyo kuwa ni Bw Michael Damas (40) ambaye alitenda kosa hilo Desemba 19 mwaka jana, majira ya saa 9 usiku.
Amesema mshtakiwa alichoma nyumba hiyo na kuteketeza mali zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo zenye thamani ya shilingi laki tano kumi na nne elfu.
Aidha mahakama imepitia ushahidi kutoka upande wa mlalamikaji na imejilidhishana kuona mshitakiwa ana kesi ya kujibu kwa kanuni na sheria
Hata hivyo,mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na mahakama imeahirisha kesi hiyo mpaka itakapo tajwa tena tarehe 29 machi mwaka huu kwa ajili ya kusikiliza ushahidi  kutoka upande wa mshtakiwa, na mshtakiwa huyo yupo nje kwa dhamana.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA