WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA WAKITUHUMIWA WIZI WA FEDHA KWA KUTUMIA SIMU


Na.Issack Gerald-Mpanda
Watu wawili wakazi wa kijiji cha Ikaka  kata ya Mnyagala wilayani Mpanda mkoani Katavi,wamefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda wakikabiliwa na shtaka la wizi wa fedha kwa njia ya simu  ambayo ni mali ya Charles Lubasha mkazi wa Kakese.

Akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu mwandamizi Bw David Mbembela,askari wa jeshi la polisi WP8940 PC Shakira  amewataja washtakiwa hao kuwa ni Bw.Emmanuel Makopo (23) na Cosmas Faustene(33) waliotenda kosa hilo Machi 7 mwaka huu majira ya saa kumi jioni.
PC Shakira amesema washtakiwa hao waliiba pesa zenye thamani ya shilingi laki sita na elfu tano kwa kutumia simu mali ya Lubasha.
Hata hivyo washtakiwa wamekana kosa hilo ambapo pia polisi imeweka pingamizi ya dhamana dhidi yao kutokana na kuwa na kesi nyingine mahakamani.
Kufuatia hatua hiyo,mahakama imeahirisha kesi mpaka itakapo tajwa tena machi  18 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA