Posts

Showing posts from March 24, 2018

BARAZA LA MAASKOFU KUTEMA CHECHE KESHO KUHUSU HALI YA USALAMA WA TANZANIA NA WATU WAKE

Image
Baraza la maaskofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri chini Tanzania (KKKT) linasema umoja na amani ya Tanzania viko hatarini. Katika waraka wa ujumbe wa pasaka unaosambaa katika mitandao ya kijamii na kutarajiwa kusomwa kesho katika makanisa mbali mbali ya KKKT nchini Tanzania, baraza hilo limeorodhesha mambo kadhaa ambayo wameyataja kuwa ndio tishio la umoja na amani ya nchi hiyo. Waraka umeyataja baadhi ya mambo hayo kuwa ni pamoja na utekaji,utesaji,kupotea kwa watu, mashambulizi ya silaha dhidi ya viongozi wa kisiasa,mauaji yenye mwelekeo wa kiitikadi,vitisho, ubambikiziaji wa kesi na matumizi mabaya ya vyombo vya dola dhidi ya wananchi. Waraka umeongeza pia kwamba uhuru wa kujieleza,kutoa na kupokea habari umeendelea kutoweka nchini huku ukionya kubanwa na hatimaye kuelekea kupungua kwa uhuru wa Bunge,Mahakama, na Tume ya Uchaguzi, ukisema hatua hii ni pamoja na kudhoofishwa kwa serikali za Mitaa. jumbe huu kutoka baraza la maaskofu wa KKKT umekuja siku chache tu baada

KAULI YA WAZIRI ISIPOFAFANULIWA VIZURI INAWEZA KUSABABISHA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU SHULENI

Image
Miaka michache baada ya serikali yenyewe kufuta adhabu ya viboko shuleni,Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Dk.Mwigulu Nchemba,amewataka walimu kuendelea kutoa elimu bora kwa wanafunzi kwa kuwafundisha maadili mema na na inapobidi matumizi ya fimbo yatumike. Waziri Nchemba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika harambee ya ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari   Lulumba Wilayani Iramba mkoani Singida ambapo amesema walimu wanatumia fimbo kunyoosha nidhamu za wanafunzi ili kutengeneza hatma ya nchi. Katika hatua nyingine amesisitiza kuwa ni lazima kuendelea kulinda hadhi za walimu kwa kuwapatia miundombinu bora ya ofisi na vyumba vya madarasa. Mbali na hayo Dk.Nchemba amesema majengo ya taasisi za serikali yanapaswa kuwa bora zaidi na sio kutumia ramani za awali pekee kwani zinapaswa kuboreshwa kulingana na maendeleo yaliyopo. Imekuwa ikishuhudiwa baadhi ya walimu wakiwachapa wanafunzi mpaka kusababisha majeraha hata baadhi ya walimu hao kufukuzwa kazi,je,kauli ya Waziri M

SERIKALI YAFUNGUKA KUHUSU KUFUNGIA MITANDAO

Image
Serikali ya awamu ya tano ya Rais Dkt.John Magufuli imekanusha taarifa ya kufungia mitandao ya kijamii kama inavyoelezwa na baadhi ya watu na kuitaka jamii kuzipuuza endapo watakutana nazo mitandaoni. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa asubuhi ya leo katika ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema taarifa hizo ni uzushi mtupu hazina ukweli wowote ambayo imetengenezwa na wahalifu wa mtandao. Leo (Machi 24, 2018) imesambazwa barua iliyokuwa inaonesha kutoka Ikulu ambayo imeandika taarifa za kuwa serikali inawaasa watanzania wote wanaotumia mitandao ya kijamii kuitumia kwa uangalifu na tija ili kujiletea maendeleo yao na Taifa kwa ujumla. Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

ZANZIBAR YAPAA MAAMBUZI YA KIFUA KIKUU

Image
Wizara ya Afya Zanzibar imesema kasi ya Ugonjwa wa kifua kikuu imekuwa ikiengezeka kwa kiwango kikubwa ambapo   katika mwaka 2017 jumla ya wagonjwa 948 waligundulika kuwa na ugonjwa huo. Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na siku ya kifua kikuu katika ukumbi Wizara hiyo Mnazi mmoja Mjini Zanzibar ,Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Muhammed amesema Ongezeko hilo limefikia idadi ya wagonjwa 225 ikilinganishwa na mwaka 2016. Amesema kutokana na ongezeko hilo Utafiti unaonesha bado Zanzibar inakabiliwa na tatizo la Uelewa mdogo juu ya Maradhi hayo jambo ambalo linapelekea wananchi kushindwa kuhudhuria katika vituo kwa wakati ili kupunguza maambukizi. Amesema   kutokana na Ugonjwa wa kifua kikuu kuwa ni ugonjwa wa tisa unaosababisha vifo kwa wagonjwa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itahakikisha inachukuwa jitihada mbalimbali ikiwemo   kuendelea kutoa elimu ya kujiepusha na viashiria vya maradhi hayo. Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Afya ulimwenguni takwimu zin

RAIS MAGUFULI ATEUA WAKURUGENZI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt.John Magufuli amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki(TAEC),Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC),Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa na Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma.