Posts

Showing posts from March 17, 2018

MWENYEKITI JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA ABWAGA MANYANGA

Image
Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF) Bw.Theophil Makunga amejiuzulu nafasi hiyo. Taarifa ya kujizulu kwa Bw.Makungu imetolewa leo katika vyombo vya habari na Jukwaa la   wahariri   Tanzania (TEF) na kueleza kuwa mwenyekiti huyo amejiuzulu tangu jana. Kwa mjibu wa TEF,Bw.Makungu amechukua hatua hiyo kwa kutumia uhuru wake binafsi kama mwanachama hai ambapo mkutano wa dharura umefanyika leo na kuridhia kujiuzulu kwake. Pamoja na jukwaa kusema litakosa busara za Bw.Makungu katika taaluma ya habari pia limemtakia kila la heri katika majukumu yake mengine. Habari zaidi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

TANZANIA YATAKIWA KUUNGA MKONO MGOGORO WA URUSI NA UINGEREZA

Image
Serikali ya Uingereza imeitaka Tanzania na Jumuiya ya Kimataifa kuiunga mkono katika kupinga kitendo cha Urusi kutumia sumu aina ya novichok katika jaribio la kumuua jasusi wa Kirusi Sergei Skripal na binti yake Yulia. Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, Balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke alisema nchi yake haitavumilia majaribio yoyote ya mauaji ya watu wasio na hatia ndani ya ardhi yake. Cooke alisisitiza kuwa ni wazi Urusi ilihusika katika jaribio hilo na walipewa nafasi ya kueleza kwa nini waliamua kutumia sumu hiyo ndani ya Uingereza licha ya kwamba matumizi ya kemikali kama silaha ni kinyume cha sheria za kimataifa. Hata hivyo,alisema mpaka sasa hawajatoa maelezo kuhusu suala hilo. Alipoulizwa kuhusu msimamo wa Tanzania kuhusu suala hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje,Dk Susan Kolimba alisema hawezi kulizungumzia kwa sasa ambapo hata Waziri wa Mambo ya Nje,Dk Augustine Mahiga hakupatikana ili kuzungumzia suala hilo . Mpaka sasa Uingereza

SERIKALI YAKANUSHA SUKARI YA ZANZIBAR KUZUIWA KUUZWATANZANIA BARA

Image
Serikali imekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba imekizuia Kiwanda cha Sukari Zanzibar,ZSFL kuuza Sukari yake Tanzania Bara. Msemaji Mkuu wa Serikali Dk.Hassan Abbas Akizungumza jana jijini Arusha,Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dk.Hassan Abbas amesema, kiwanda hicho kinapaswa kukidhi soko la Zanzibar la tani elfu 10 badala ya kulalamika kimezuiwa kuuza Sukari nje. Dk.Abbas amesema mahitaji ya kawaida Zanzibar ya sukari ni Tani elfu 17 mpaka elfu 20 kwa mwaka lakini kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha tani elfu 10 japo kwa sasa uzalishaji umeshuka hadi tani elfu 8 hivyo kufanya Zanzibar kuwa na upungufu wa tani elfu 9 hadi elfu 12. Mapema wiki hii,Kaimu Mkurugenzi Mkuu Kiwanda hicho cha Sukari Zanzibar,Bi. Fatma Salum Ali,alisema kiwanda hicho kinapata hasara ya zaidi ya shilingi laki tatu kwa kila tani moja ya Sukari inayozalishwa kutokana na kushindwa kupata kibali cha kuuza Sukari Tanzania Bara