Posts

Showing posts from April 12, 2018

RAIS AWAPANDISHA VYEO MAAFISA WA JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA (JWTZ)

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli leo Aprili 12,2018 amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ ) katika vyeo mbalimbali. Taarifa iliyosomwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo,Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa Mhe.Rais Magufuli amempandisha cheo Meja Jenarali Peter Paul Massao kuwa Luteni Jenerali.

WANANCHI KATAVI WATAKA VIONGOZI WA SERIKALI WAMUENZI SOKOINE KWA KUPELEKA HUDUMA MUHIMU ZA JAMII KWA WANANCHI

Wananchi Mkoani Katavi wamewashauri viongozi wa serikali wa serikali ya awamu ya tano kuenzi kifo cha Wazairi Mkuu hayati Edward Moringe Sokoine kwa kupeleka huduma muhimu za kijamii kwa wananchi ikiwemo maji. Wakizungumza na P5TANZANIA kwa nyakati tofauti kuhusu kumbukumbu ya miaka 34 ya kifo cha waziri mkuu hayati Edward Moringe Sokoine aliyefariki Apriki 12,1984 wamesema kuna maeneo mengi mkoani Katavi ambayo bado yanakosa huduma muhimu kama maji huku hata sehemu zenye zikipata kwa mgao. IAidha wametaka hata miradi ya maji iliyoanzishwa enzi za ukoloni ifufuliwe huku wakisema bado kuna hali ngumu ya kimaisha ambayo serikali inatakiwa iyatatue kama sehemu ya kumuenzi Sokoine. Aidha wamesema ni kiongozi aliyechukia uhujumu uchumi,rushwa,ufisadi huku akishiriki vema kuandaa majeshi wakatio wa vita vya Kagera baina ya Tanzania na Uganda mwaka 1978. Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine aliwahi kuwa Waziri Mkuu mara mbili Februaei 13 mwaka 1977 hadi Novemba 7 mwaka 1980 na   Febr

RAIS MAGUFULI ATAKA WATANZANIA WAMUEZI SOKOINE KWA KUIGA MEMA ALIYOYAFANYA

Image
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.John Magufuli ametoa rai kwa watanzania kumuenzi Waziri Mkuu wa Zamani hayati Edward Moringe Sokoine kwa kujenga umoja,kupiga vita rushwa na kuchapa kazi. Rais ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa twitter ikiwa leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Edward Moringe Sokoine aliyefariki dunia Aprili 12,1984 kwa ajali ya gari. Ajali hiyo ilitokea eneo la Dakawa nje Kidogo ya Mji wa Morogoro wakati akitokea Bumgeni Dodoma Kuelekea Jijini Dar es salaam. Amesema watanzania wanapoazimisha siku hii ya kifo chake, watanzania waige mfano wake kwani alikuwa msema kweli, asiyeogopa,mpiga vita rushwa,ufisadi,unyonyaji,mzalendo wa kweli na aliyechukia rasilimali za watanzania kuibwa. Rais amesema kwa upande wake anamkumbuka kiongozi huyo enzi za uhai wake na mchango wake katika Taifa la Tanzania na anasema alipata taarifa za kifo cha Sokoine   tarehe 12 Aprili 1984 akiwa Mpwapwa JKT nikitumikia jes

SPIKA AAGIZA MWANDISHI NA WAHARIRI WA GAZETI LA RAIA MWEMA WAHOJIWE KWA KULIDHALILISHA BUNGE

Image
Kamati ya Maadili,Haki na Madaraka ya Bunge,inatarajia kuwahoji mwanahabari Paschal Mayallah na wahariri wa gazeti la kila wiki la Raia Mwema kwa madai ya kuchapisha habari inayodhalilisha bunge,Aprili 9 wiki hii. Hayo yameelezwa leo Aprili 12 bungeni na Spika wa Bunge,Job Ndugai aliyesema kuwa habari iliyochapishwa Aprili 9 ilidhamiria kuchafua hadhi ya bunge. Hayo yamekuja baada ya mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga kuomba mwongozo wa Spika juzi Aprili 9, akihoji iwapo habari iliyoandikwa na gazeti hilo yenye kichwa cha habari “Bunge linajipendekeza?”haidhalilishi bunge. Spika Ndugai leo Aprili 12,ameliambia bunge kuwa mwandishi huyo na wahariri watatakiwa kuhojiwa na kamati hiyo ya bunge. Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

LEO NI KUMBUKUMBU YA MIAKA 34 YA KIFO EDWARD SOKOINE HISTORIA YAKE IKO HAPA

Image
Edward Moringe Sokoine  ( 1938  -  12 Aprili   1984 ) alikuwa  mwanasiasa  kutoka nchi ya  Tanzania . Aliwahi kuwa  Waziri Mkuu  mara mbili,tangu tarehe  13 Februari   1977  hadi  7 Novemba   1980 ,tena tangu tarehe  24 Februari   1983  hadi  kifo  chake,alipofariki kufuatana na  ajali  ya gari. Uongozi wake ulionekana kuwa wa mfano kwa jinsi alivyokuwa na  uadilifu  na kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulaji  rushwa  na  ubadhirifu  wa  mali za umma . Upande wa  dini ,alikuwa  Mkristo  wa  Kanisa Katoliki ,tena mwanachama wa  Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko . Sokoine alifariki kwa ajali ya gari wakati akitoka kwenye kikao cha  bunge   Dodoma  kuelekea  Dar es Salaam . Wengi wanashuku ajali hiyo kuwa ilipangwa. Kifo chake kilileta majonzi makubwa kwa Watanzania wa kawaida ambao walikuwa wanamtarajia kuwatetea wanyonge na kuinua hali ya maisha yao. Mwili  wa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwao  Monduli ,mkoani  Arusha . Chuo cha Kilimo na Mifugo Morogoro  k