Posts

Showing posts from February 13, 2018

CHAMA CHA ANC CHAAMUA ZUMA NI LAZIMA AONDOKE

Image
Chama tawala Afrika kusini African National Congress (ANC) kimemuomba rasmi rais Jacob Zuma ajiuzulu baada ya yeye kukataa kufanya hivyo mapema hii leo. Taarifa kuhusu uamuzi huo umefuata mfululizo wa mazungumzo ya maafisa wa juu wa chama hicho yalioendelea usiku kucha hadi kuamkia alfajiri ya leo. Haki miliki ya picha Muhula wa Zuma unamalizika mwaka ujao Iwapo Bw.Zuma(75) hatoteteleka atakabiliwana na kura ya kutokuwa na imani naye bungeni ambayo anatarajiwa kushindwa. Akiwa amehudumu madarakani tangu 2009, ameandamwa kwa tuhuma za rushwa. Haki miliki ya picha Imebainika kuwa mrithi wake Zuma atakuwa Cyril Ramaphosa kwasababu ndiye rais wa chama cha ANC. Chama cha ANC hakijathibitisha rasmi mipango yake lakini duru kutoka cham hicho zimetoa ufafanuzi katika vyombo vya habari nchini Afrika kusini na pia kwa shirika la habara la kimataifa la Reuters. Rais Zuma amekiuka shinikizo linaloongezeka la kumtaka ajiuzulu tangu Desemba wakati Cyril Ramaphosa alipoichukua nafa

MWANASHERIA MKUU WA KENYA PROFESA GITHU MUIGAI ABWAGA MANYANGA

Image
Mwanasheria mkuu wa Kenya Profesa Githu Muigai amejiuzulu baada ya kuhudumu kwa miaka sita na nusu ambapo kufuatia uamuzi huo Rais Uhuru Kenyatta amemshukuru Profesa Githu kwa huduma zake na sasa jaji Paul Kihara Kariuki atachukua mahala pake. Kabla ya uteuzi wake kuwa mwanasheria mkuu profesa Muigai alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya mawakili ya Mohammed Muigai na amekuwa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika kukabiliana na ubaguzi wa rangi. Haki miliki ya picha Mwanasheria mkuu wa Kenya Professa Githu Muigai Aidha alikuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha sheria cha Columbia mjini New York ambapo Kutoka 1984 alikuwa mwanfunzi katika chuo cha kusomea uanasheria nchini Kenya . Wakati huo huo alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi huku akiwa mshauri wa serikali katika maswala ya kisheria, Githu Muiga atakumbukwa kwa kuleta sheria za mageuzi katika timu ya uchaguzi nchini Kenya siku chache tu kabla ya uchaguzi kufanyika. Katika sheria hiyo kamishna yeyote yul

WANAFUNZI WA SEKONDARI WASOMEA KATIKA VYUMBA VYA MAABALA

Image
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kasokola iliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wanalazimika kusomea katika vyumba vya maabala vyenye kemikali za kisayansi zinazotumika kwa ajili ya masomo ya fikizikia,Kemia na baiolojia. Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameiomba serikali na wadau kujenga vyumba vya madarasa ili kuwaepusha na mazingira hatarishi walimu na wanafunzi. Kwa upande wake Kaimu mkuu wa shule ya sekondari Kasokola Joel Mwandwanda amesema wanafunzi kusomea katika vyumba vya maabala kunatokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo ambapo hata walimu wamegeuza maabala hizo na baadhi ya vyumba vya madarasa kuwa ofisi.